< Waefeso 3 >

1 Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
Por isso eu, Paulo, [sou] prisioneiro de Cristo Jesus, para o benefício de vós, gentios.
2 Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
Se é que já ouvistes da responsabilidade acerca da graça de Deus, que me foi dada para vós;
3 Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
que por revelação me foi dado a conhecer este mistério (conforme já [vos] escrevi um pouco;
4 nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
quando o ledes, podeis entender o meu entendimento deste mistério de Cristo).
5 Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
Esse mistério em outras gerações não foi dado a conhecer aos seres humanos, como agora foi revelado pelo Espírito aos seus santos apóstolos e profetas:
6 Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
[isto é, ] que os gentios são conjuntamente herdeiros, [membros] de um mesmo corpo, e participantes da promessa em Cristo Jesus por meio do evangelho.
7 Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
Eu fui feito servidor desse [evangelho] conforme o dom da graça de Deus, que me foi dada segundo a operação do seu poder.
8 Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
A mim, o menor de todos os santos, foi dada esta graça de anunciar aos gentios, por meio do Evangelho, as inimagináveis riquezas de Cristo,
9 tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn g165)
E para esclarecer qual é a administração do mistério que desde as eras passadas esteve oculto em Deus, que criou todas as coisas, (aiōn g165)
10 kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
para que a multiforme sabedoria de Deus seja agora manifestada pela igreja aos domínios e autoridades nos lugares celestes,
11 Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn g165)
conforme o eterno propósito que ele cumpriu em Cristo Jesus, nosso Senhor, (aiōn g165)
12 Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
no qual temos coragem e acesso confiante pela fé nele.
13 Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
Portanto, eu [vos] peço que não vos desanimeis em minhas aflições por vós. Elas são a vossa glória.
14 Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
Por causa disso me ponho de joelhos diante do Pai;
15 aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
do qual toda a família nos céus e na terra recebe nome.
16 Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
[Oro] para que, conforme a sua riquíssima glória, ele vos conceda que sejais fortalecidos com poder pelo seu Espírito no interior de cada um,
17 naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
para que Cristo habite em vossos corações pela fé. [Oro] para que vós estejais enraizados e firmados no amor,
18 kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
e assim possais compreender, com todos os santos, qual é a largura, comprimento, profundidade, e altura,
19 Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
e conhecer o amor de Cristo, que excede o entendimento, para que sejais cheios de toda a plenitude de Deus.
20 Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
E quanto àquele que é poderoso para fazer tudo muito mais abundantemente do que pedimos ou pensamos, segundo o poder que opera em nós,
21 kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
a ele seja a glória na Igreja, e em Cristo Jesus, por todas as gerações para todo o sempre, Amém! (aiōn g165)

< Waefeso 3 >