< Waefeso 3 >

1 Kutokana na hayo, mimi Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu kwa ajili yenu, namwomba Mungu.
For this cause, I Paul, the prisoner of Christ Jesus for you the nations,
2 Bila shaka mmekwisha sikia kwamba Mungu, kwa neema yake, alinikabidhi kazi hii niifanye kwa faida yenu.
if, indeed, you heard of the dispensation of the grace of God that was given to me in regard to you,
3 Mimi nilijulishwa kwa njia ya ufunuo mpango wake uliofichika. (Nimeandika kwa ufupi juu ya jambo hili,
that by revelation He made known to me the secret, according as I wrote before in few [words]—
4 nanyi mkiyasoma maneno yangu mtaweza kujua jinsi ninavyoielewa siri hiyo ya Kristo.)
in regard to which you are able, reading [it], to understand my knowledge in the secret of the Christ,
5 Zamani watu hawakujulishwa siri hiyo; lakini sasa Mungu amewajulisha mitume na manabii wake watakatifu kwa njia ya Roho.
which in other generations was not made known to the sons of men, as it was now revealed to His holy apostles and prophets in the Spirit—
6 Siri yenyewe ni hii: kwa njia ya Habari Njema watu wa mataifa mengine wanapata sehemu yao pamoja na Wayahudi katika zile baraka za Mungu; wao ni viungo vya mwili uleule, na wanashiriki ahadi ileile aliyofanya Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
that the nations are fellow-heirs, and of the same body, and partakers of His promise in the Christ, through the good news,
7 Mimi nimefanywa kuwa mtumishi wa Habari Njema kwa neema ya pekee aliyonijalia Mungu kwa uwezo wake mkuu.
of which I became a servant, according to the gift of the grace of God that was given to me, according to the working of His power;
8 Mimi ni mdogo kuliko watu wote wa Mungu; lakini amenijalia neema yake, ili niwahubirie watu wa mataifa utajiri wake Kristo usiopimika,
to me—the less than the least of all the holy ones—was given this grace, among the nations to proclaim good news—the untraceable riches of the Christ,
9 tena niwaangazie watu wote waone jinsi mpango wa Mungu uliofichika unavyotekelezwa. Mungu aliye Muumba wa vitu vyote alificha siri hiyo yake tangu milele, (aiōn g165)
and to cause all to see what [is] the fellowship of the secret that has been hid from the ages in God, who created all things by Jesus Christ, (aiōn g165)
10 kusudi, sasa kwa njia ya kanisa, wakuu na wenye enzi wa mbinguni wapate kuitambua hekima ya Mungu iliyo ya namna nyingi.
that there might be made known now to the principalities and the authorities in the heavenly [places], through the Assembly, the manifold wisdom of God,
11 Mungu alifanya jambo hilo kufuatana na azimio lake la milele ambalo amelifanya kwa njia ya Kristo Bwana wetu. (aiōn g165)
according to a purpose of the ages, which He made in Christ Jesus our Lord, (aiōn g165)
12 Basi, katika kuungana na Kristo, na kwa njia ya imani katika Kristo, sisi tunathubutu kumkaribia Mungu kwa uhodari.
in whom we have the freedom and the access in confidence through the faith of Him,
13 Kwa hiyo, nawaombeni msife moyo kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, maana hayo ni kwa ajili ya utukufu wenu.
for this reason, I ask [you] not to faint in my tribulations for you, which is your glory.
14 Kwa sababu hiyo, nampigia magoti Baba,
For this cause I bow my knees to the Father of our Lord Jesus Christ,
15 aliye asili ya jamaa zote duniani na mbinguni.
of whom the whole family in the heavens and on earth is named,
16 Namwomba Mungu, kadiri ya utajiri wa utukufu wake, awajalieni kwa uwezo wa Roho wake, nguvu ya kuwa imara ndani yenu,
that He may give to you, according to the riches of His glory, to be strengthened through His Spirit with might, in regard to the inner man,
17 naye Kristo akae mioyoni mwenu kwa imani. Namwomba mpate kuwa na mzizi na msingi katika mapendo
that the Christ may dwell through the faith in your hearts, having been rooted and founded in love,
18 kusudi muweze kufahamu pamoja na watu wote wa Mungu jinsi upendo wa Kristo ueneavyo kwa mapana na marefu, kwa kimo na kina.
that you may be in strength to comprehend, with all the holy ones, what [is] the breadth, and length, and depth, and height,
19 Naam, mpate kujua upendo wa Kristo upitao elimu yote, mjazwe kabisa utimilifu wote wa Mungu.
to know also the love of the Christ that is exceeding the knowledge, that you may be filled—to all the fullness of God;
20 Kwake yeye ambaye kwa nguvu yake ifanyayo kazi ndani yetu, aweza kufanya mambo makuu zaidi ya yale tuwezayo kuomba au kufikiria;
and to Him who is able to do exceedingly [and] abundantly above all things that we ask or think, according to the power that is working in us,
21 kwake Mungu uwe utukufu katika kanisa na katika Kristo Yesu, nyakati zote, milele na milele! Amina. (aiōn g165)
to Him [is] the glory in the Assembly in Christ Jesus, to all the generations of the age of the ages. Amen. (aiōn g165)

< Waefeso 3 >