< Wakolosai 2 >

1 Napenda mjue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya watu wa Laodikea na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona kwa macho.
Så vill jag att I veta skolen, hvilken kamp jag hafver om eder, och om dem som äro i Laodicea, och om alla dem som min person i köttet icke sett hafva;
2 Nafanya hivi kusudi mioyo yao ifarijiwe na kuvutwa pamoja katika upendo, ili wajazwe uthabiti mwingi uletwao na elimu ya kweli. Hapo wataijua siri ya Mungu ambayo ni Kristo mwenyewe.
På det deras hjerta måga få någon hugnad, och sammanfogade varda i kärlekenom, till all rikedom uti fullkomligit förstånd, till att kunna besinna Guds hemlighet, både Fadrens och Christi;
3 Ndani yake zimefichika hazina zote za hekima na elimu.
Uti hvilkom fördolda ligga alla visdoms och förstånds håfvor.
4 Basi, nawaambieni, msikubali kudanganywa na mtu yeyote kwa maneno ya uongo hata kama ni ya kuvutia sana.
Men detta säger jag, på det ingen skall bedraga eder med klok ord.
5 Maana, ingawa mimi niko mbali nanyi kwa mwili, lakini niko pamoja nanyi kwa roho, na ninafurahi kuona uthabiti kamili mnaosimama nao pamoja katika imani yenu kwa Kristo.
Ty ändock jag är ifrån eder efter köttet, är jag dock när eder i Andanom, fröjdar mig, och ser edor skickelse, och edar tros stadighet på Christum.
6 Maadamu ninyi mmemkubali Kristo Yesu kuwa Bwana, basi, ishini katika muungano naye.
Såsom I nu anammat hafven Herran Christum Jesum, så vandrer i honom;
7 Mnapaswa kuwa na mizizi ndani yake, kujijenga juu yake na kuwa imara katika imani yenu kama mlivyofundishwa. Muwe na shukrani tele.
Och varer rotade och uppbyggde i honom, och varer faste i trone, såsom I lärde ären, och varer i henne rikeliga tacksamme.
8 Angalieni basi, mtu asiwapotoshe kwa udanganyifu mtupu wa hekima ya kibinadamu, ambayo chanzo chake ni mafundisho ya mapokeo ya watu na ya pepo watawala, na wala si Kristo mwenyewe!
Ser till, att eder icke någor bortröfvar med Philosophia och fåfängt bedrägeri, efter menniskors stadgar, och efter verldenes stadgar, och icke efter Christum;
9 Maana, ndani yake Kristo katika ubinadamu wake, umo ukamilifu wote wa Mungu,
Ty i honom bor all Gudomsens fullhet lekamliga.
10 nanyi mmepewa uzima kamili katika kuungana naye. Yeye yuko juu ya pepo watawala wote na wakuu wote.
Och I ären i honom fullkomne, hvilken är hufvudet öfver all Förstadöme och väldighet;
11 Katika kuungana na Kristo ninyi mlitahiriwa, lakini si kwa tohara ifanywayo na watu, bali inayofanywa na Kristo mwenyewe, na ambayo inahusikana na kukombolewa kutoka katika utu wa dhambi.
I hvilkom I ock omskorne ären med den omskärelse, som sker utan händer, då I afladen syndakroppen i köttet, nämliga med Christi omskärelse;
12 Maana, mlipobatizwa mlizikwa pamoja na Kristo, na katika ubatizo, mlifufuliwa pia pamoja naye kwa imani yenu katika nguvu ya Mungu ambaye alimfufua Kristo kutoka wafu.
I det, att I med honom begrafne ären genom dopet; i hvilkom I ock uppståndne ären genom trona, den Gud verkar, hvilken honom uppväckt hafver ifrå de döda.
13 Wakati mmoja nanyi mlikuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kwa sababu ninyi mlikuwa watu wa mataifa mengine. Lakini Mungu amewapa ninyi uzima pamoja na Kristo. Mungu ametusamehe dhambi zetu zote;
Han hafver ock gjort eder lefvande med honom, då I döde voren i synderna, och uti edars kötts förhud; och hafver förlåtit oss alla synder;
14 alifutilia mbali ile hati ya deni iliyokuwa inatukabili na masharti yake, na kuifuta kabisa kwa kuipigilia msalabani.
Och afplånat den handskrift, som oss emot var; hvilken af stadgarna kom, och var oss emot; och den hafver han tagit oss af vägen, och naglat vid korset;
15 Juu ya msalaba Kristo aliwapokonya nguvu zao hao pepo watawala na wakuu; aliwafanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuwaburuta kama mateka katika msafara wa ushindi wake.
Och hafver blottat Förstadömen, och väldigheterna, och fört dem uppenbarliga, och gjort en härlig seger af dem, genom sig sjelf.
16 Kwa hiyo, basi, msikubali kupewa masharti na mtu yeyote kuhusu vyakula au vinywaji, siku za sherehe, sikukuu ya Mwezi mpya au Sabato.
Så låter nu ingen göra eder samvet öfver mat, eller dryck, eller öfver bestämda helgedagar, eller nymånader, eller Sabbather;
17 Mambo ya aina hiyo ni kivuli tu cha yale yatakayokuja; ukweli wenyewe ndiye Kristo.
Hvilket är skuggen af det som tillkommande var; men kroppen sjelf är i Christo.
18 Msikubali kuhukumiwa na mtu yeyote anayejitakia kuwa wa maana kwa sababu ya maono ya pekee na ambaye anasisitiza juu ya unyenyekevu wa uongo na ibada kwa malaika. Mtu wa namna hiyo amepumbazika kwa fikira danganifu za kidunia
Låter ingen taga eder lönen ifrå, den som vandrar efter egen godtycko i Änglaödmjukhet och andelighet, i de ting han aldrig sett hafver, och är förgäfves uppblåst i sitt köttsliga sinne;
19 na amejitenga na Kristo aliye kichwa cha huo mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili wote unalishwa na kuunganishwa pamoja kwa viungo na mishipa yake, nao hukua kama atakavyo Mungu.
Och håller sig icke vid hufvudet, af hvilko hele lekamenen genom leder och ledamot kraft får och tillsammans hänger, och tillväxer i den förökelse som Gud gifver.
20 Ninyi mmekufa pamoja na Kristo na kukombolewa kutoka nguvu za pepo watawala wa ulimwengu. Kwa nini, basi, kuishi tena kama vile mngekuwa wa ulimwengu huu? Ya nini kuwekewa masharti:
Efter I nu döde ären med Christo, ifrå de verldsliga stadgar; hvi låten I eder då begripas med beskrefna stadgar, lika som I ännu lefden i verldene?
21 “Msishike hiki,” “Msionje kile,” “Msiguse kile!”
De der säga: Du skall icke komma vid det; icke smaka det; icke handtera det;
22 Mambo hayo yote yanahusika na vitu vyenye kuharibika mara tu vinapotumiwa; hayo ni maagizo na mafundisho ya kibinadamu tu.
Hvilket dock allt förgås i brukningene, och är efter menniskors bud och lärdom;
23 Kweli, masharti hayo yaonekana kuwa ya hekima katika namna ya ibada ya kujitakia wenyewe, unyenyekevu wa uongo na kuutendea mwili kwa ukali; lakini kwa kweli, haifai chochote kuzuia tamaa za mwili.
Hvilke hafva väl ett sken af visdom, genom sjelftagen andelighet och ödmjukhet, och derigenom att de icke skona kroppen, och göra icke köttena dess äro till dess nödtorft.

< Wakolosai 2 >