< Matendo 13 >

1 Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
Now there were, in the Church at Antioch, prophets and teachers, among whom were Barnabas, and Simon, who was called the Black, and Lucius of Cyrene, and Manahen, who was the foster brother of Herod the tetrarch, and Saul.
2 Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: “Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia.”
Now as they were ministering for the Lord and fasting, the Holy Spirit said to them: “Separate Saul and Barnabas for me, for the work for which I have selected them.”
3 Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
Then, fasting and praying and imposing their hands upon them, they sent them away.
4 Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
And having been sent by the Holy Spirit, they went to Seleucia. And from there they sailed to Cyprus.
5 Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
And when they had arrived at Salamis, they were preaching the Word of God in the synagogues of the Jews. And they also had John in the ministry.
6 Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
And when they had traveled throughout the entire island, even to Paphos, they found a certain man, a magician, a false prophet, a Jew, whose name was Bar-Jesu.
7 Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
And he was with the proconsul, Sergius Paulus, a prudent man. This man, summoning Barnabas and Saul, wanted to hear the Word of God.
8 Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
But Elymas the magician (for so his name is translated) stood against them, seeking to turn the proconsul away from the Faith.
9 Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
Then Saul, who is also called Paul, having been filled with the Holy Spirit, looked intently at him,
10 akasema, “Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
and he said: “So full of every deceit and of all falsehoods, son of the devil, enemy of all justice, you never cease to subvert the righteous ways of the Lord!
11 Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo.” Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
And now, behold, the hand of the Lord is upon you. And you will be blinded, not seeing the sun for a length of time.” And immediately a fog and a darkness fell over him. And wandering around, he was seeking someone who might lead him by the hand.
12 Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
Then the proconsul, when he had seen what was done, believed, being in wonder over the doctrine of the Lord.
13 Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
And when Paul and those who were with him had sailed from Paphos, they arrived at Perga in Pamphylia. Then John departed from them and returned to Jerusalem.
14 Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
Yet truly, they, traveling on from Perga, arrived at Antioch in Pisidia. And upon entering the synagogue on the Sabbath day, they sat down.
15 Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: “Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni.”
Then, after the reading from the Law and the Prophets, the leaders of the synagogue sent to them, saying: “Noble brothers, if there is in you any word of exhortation to the people, speak.”
16 Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: “Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
Then Paul, rising up and motioning for silence with his hand, said: “Men of Israel and you who fear God, listen closely.
17 Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
The God of the people of Israel chose our fathers, and exalted the people, when they were settlers in the land of Egypt. And with an exalted arm, he led them away from there.
18 Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
And throughout a time of forty years, he endured their behavior in the desert.
19 Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
And by destroying seven nations in the land of Canaan, he divided their land among them by lot,
20 Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
after about four hundred and fifty years. And after these things, he gave them judges, even until the prophet Samuel.
21 Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
And later on, they petitioned for a king. And God gave them Saul, the son of Kish, a man from the tribe of Benjamin, for forty years.
22 Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
And having removed him, he raised up for them king David. And offering testimony about him, he said, ‘I have found David, the son of Jesse, to be a man according to my own heart, who will accomplish all that I will.’
23 Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
From his offspring, according to the Promise, God has brought Jesus the Savior to Israel.
24 Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
John was preaching, before the face of his advent, a baptism of repentance to all the people of Israel.
25 Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
Then, when John completed his course, he was saying: ‘I am not the one you consider me to be. For behold, one arrives after me, the shoes of whose feet I am not worthy to loosen.’
26 “Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
Noble brothers, sons of the stock of Abraham, and those among you who fear God, it is to you the Word of this salvation has been sent.
27 Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
For those who were living in Jerusalem, and its rulers, heeding neither him, nor the voices of the Prophets that are read on every Sabbath, fulfilled these by judging him.
28 Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
And although they found no case for death against him, they petitioned Pilate, so that they might put him to death.
29 Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
And when they had fulfilled everything that had been written about him, taking him down from the tree, they placed him in a tomb.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
Yet truly, God raised him up from the dead on the third day.
31 Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
And he was seen for many days by those who went up with him from Galilee to Jerusalem, who even now are his witnesses to the people.
32 Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
And we are announcing to you that the Promise, which was made to our fathers,
33 Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
has been fulfilled by God for our children by raising up Jesus, just as it has been written in the second Psalm also: ‘You are my Son. This day I have begotten you.’
34 Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
Now, since he raised him from the dead, so as to no longer return to corruption, he has said this: ‘I will give to you the holy things of David, the faithful one.’
35 Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
And also then, in another place, he says: ‘You will not allow your Holy One to see corruption.’
36 Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
For David, when he had ministered to his generation in accordance with the will of God, fell asleep, and he was placed next to his fathers, and he saw corruption.
37 Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
Yet truly, he whom God has raised from the dead has not seen corruption.
38 Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
Therefore, let it be known to you, noble brothers, that through him is announced to you remission from sins and from everything by which you were not able to be justified in the law of Moses.
39 na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
In him, all who believe are justified.
40 Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
Therefore, be careful, lest what was said by the Prophets may overwhelm you:
41 Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.”
‘You despisers! Look, and wonder, and be scattered! For I am working a deed in your days, a deed which you would not believe, even if someone were to explain it to you.’”
42 Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
Then, as they were departing, they asked them if, on the following Sabbath, they might speak these words to them.
43 Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
And when the synagogue had been dismissed, many among the Jews and the new worshipers were following Paul and Barnabas. And they, speaking to them, persuaded them to continue in the grace of God.
44 Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
Yet truly, on the following Sabbath, nearly the entire city came together to hear the Word of God.
45 Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
Then the Jews, seeing the crowds, were filled with envy, and they, blaspheming, contradicted the things that were being said by Paul.
46 Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios g166)
Then Paul and Barnabas said firmly: “It was necessary to speak the Word of God first to you. But because you reject it, and so judge yourselves unworthy of eternal life, behold, we turn to the Gentiles. (aiōnios g166)
47 Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.”
For so has the Lord instructed us: ‘I have set you as a light to the Gentiles, so that you may bring salvation to the ends of the earth.’”
48 Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios g166)
Then the Gentiles, upon hearing this, were gladdened, and they were glorifying the Word of the Lord. And as many as believed were preordained to eternal life. (aiōnios g166)
49 Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
Now the word of the Lord was disseminated throughout the entire region.
50 Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
But the Jews incited some devout and honest women, and the leaders of the city. And they stirred up a persecution against Paul and Barnabas. And they drove them away from their parts.
51 Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
But they, shaking the dust from their feet against them, went on to Iconium.
52 Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.
The disciples were likewise filled with gladness and with the Holy Spirit.

< Matendo 13 >