< Matendo 13 >

1 Katika kanisa la Antiokia kulikuwa na watu wengine waliokuwa manabii na walimu; miongoni mwao akiwa Barnaba, Simoni aitwaye pia Mweusi, Lukio wa Kurene, Manaeni ambaye alikuwa amelelewa pamoja na mfalme Herode, na Saulo.
在安提阿教会中有几名先知和教师:巴拿巴、西门(尼结)、古利奈人路求、马念(君王希律儿时的伙伴)和扫罗。
2 Walipokuwa wanafanya ibada yao kwa Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema: “Niteulieni Barnaba na Saulo kwa ajili ya kazi niliyowaitia.”
他们在膜拜主并进行禁食的时候,圣灵说:“让巴拿巴和扫罗为我做事。”
3 Basi, baada ya kusali na kufunga zaidi, wakawawekea mikono, wakawaacha waende zao.
教会成员禁食、祈祷并把手放在他们身上祝福之后,他们就送他们上路了。
4 Basi, Barnaba na Saulo walipokwisha tumwa na Roho Mtakatifu, walishuka hadi Seleukia, na kutoka huko walipanda meli hadi kisiwa cha Kupro.
巴拿巴和扫罗在圣灵的指引下去了西流基,从那里乘船去往塞浦路斯。
5 Walipofika Salami walihubiri neno la Mungu katika masunagogi ya Kiyahudi. Yohane (Marko) alikuwa msaidizi wao.
来到撒拉米后,他们就在犹太人的会堂中宣讲上帝之道,约翰担任他们的助手。
6 Walitembea toka upande mmoja wa kisiwa mpaka Pafo upande wa pili, na huko walimkuta mchawi mmoja Myahudi aitwaye Baryesu ambaye alijisingizia kuwa nabii.
他们走遍整个岛屿,最终来到了帕弗,遇见一位自称巴·耶稣的犹太人术士,是个假先知。
7 Huyu alikuwa pamoja na Sergio Paulo, mkuu wa kile kisiwa, ambaye alikuwa mtu mwelewa sana. Sergio Paulo aliwaita Barnaba na Saulo ili asikie neno la Mungu.
他与省长士求·保罗走的很近。这位省长非常睿智,特别邀请巴拿巴和扫罗来为他讲上帝之道。
8 Lakini huyo mchawi Elima (kama alivyokuwa anaitwa kwa Kigiriki), alijaribu kuwapinga ili kumzuia huyo mkuu wa kisiwa asije akaigeukia imani ya Kikristo.
但这位术士(希腊名字叫做以吕马)不接受他们,试图让省长不要相信上帝。
9 Basi, Saulo ambaye aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo mchawi,
但被注满圣灵的扫罗(又名保罗)定睛看着他,
10 akasema, “Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka.
说:“你这满心欺诈、万恶满盈之人,魔鬼之子,正义的敌人!你总是在阻碍主的真理之路,为什么你不肯放弃呢?
11 Sasa, mkono wa Bwana utakuadhibu: utakuwa kipofu na hutaweza kuuona mwanga wa jua kwa kitambo.” Mara kila kitu kikawa kama ukungu na giza kwake, akaanza kwenda huku na huku akitafuta mtu wa kumshika mkono amwongoze.
看,主的惩罚已经到来,你将成为盲人,暂时看不见阳光。”黑暗和迷雾立刻笼罩着这位术士,他不得不找人牵他的手,给他领路。
12 Yule mkuu wa kisiwa alipoona hayo, aliongoka akawa muumini; akastaajabia sana mafundisho aliyosikia juu ya Bwana.
省长看见眼前的一切,便信了上帝,主的教导让他惊讶不已。
13 Kutoka Pafo, Paulo na wenzake walipanda meli wakaenda hadi Perga katika Pamfulia; lakini Yohane (Marko) aliwaacha, akarudi Yerusalemu.
然后保罗和同伴从帕弗乘船来到旁非利亚的别加,约翰则离开他们返回耶路撒冷去了。
14 Lakini wao waliendelea na safari toka Pisga hadi mjini Antiokia Pisidia. Siku ya Sabato waliingia ndani ya Sunagogi, wakakaa.
他们一路前行,经过别加后抵达彼西底的安提阿,在安息日这天进入会堂,然后坐下来。
15 Baada ya masomo katika kitabu cha Sheria ya Mose na katika maandiko ya manabii, wakuu wa lile sunagogi waliwapelekea ujumbe huu: “Ndugu, kama mnalo jambo la kuwaambia watu ili kuwapa moyo, semeni.”
他们朗读了律法和先知的书籍,会堂首领派人传来口信,说:“兄弟们,如果你们有什么鼓励之语,就说说吧!”
16 Basi, Paulo alisimama, akatoa ishara kwa mkono, akaanza kuongea: “Wananchi wa Israeli na wengine wote mnaomcha Mungu, sikilizeni!
保罗站起来,伸手示意大家看过来,然后开始说:“以色列人和所有敬畏上帝之人,听我说。
17 Mungu wa taifa hili la Israeli aliwateua babu zetu na kuwafanya wawe taifa kubwa walipokuwa ugenini kule Misri. Mungu aliwatoa huko kwa uwezo wake mkuu.
我们的祖先寄居在埃及的土地时,以色列人民的上帝选中了他们,凭其伟大力量带领他们走出埃及,
18 Aliwavumilia kwa muda wa miaka arobaini kule jangwani.
然后他在旷野耐心地照顾他们四十年。
19 Aliyaangamiza mataifa ya nchi ya Kanaani akawapa hao watu wake ile nchi kuwa mali yao.
上帝在消灭了迦南七国后,就把那片土地分给以色列人的祖先,让他们代代继承,这样又过了 450 年。
20 Miaka mia nne na hamsini ilipita, halafu akawapatia waamuzi wawaongoze mpaka wakati wa nabii Samweli.
后来上帝又为他们派来首领,一直持续到撒母耳先知的时刻。
21 Hapo wakapendelea kuwa na mfalme, na Mungu akawapa Saulo, mtoto wa Kishi wa kabila la Benyamini, awe mfalme wao kwa muda wa miaka arobaini.
人们请求上帝为他们送来国王,上帝就把便雅悯部落中一个人派来为王,他是基士的儿子扫罗,统治了四十年。
22 Baada ya kumwondoa Saulo, Mungu alimteua Daudi kuwa mfalme wao. Mungu alionyesha kibali chake kwake akisema: Nimemwona Daudi mtoto wa Yese; ni mtu anayepatana na moyo wangu; mtu ambaye atatimiza yale yote ninayotaka kuyatenda.
之后上帝又废去扫罗,选择大卫为王。在为大卫作证时,上帝说:‘我找到耶西的儿子大卫,他符合我的心意,将遵行我的一切旨意。’
23 Kutokana na ukoo wake mtu huyu, Mungu, kama alivyoahidi, amewapelekea watu wa Israeli Mwokozi, ndiye Yesu.
耶稣是大卫的后裔,是上帝之前承诺带给以色列的救世主。
24 Kabla ya kuja kwake Yesu, Yohane alimtangulia akiwahubiria watu wote wa Israeli kwamba ni lazima watubu na kubatizwa.
耶稣来临之前,约翰便昭告所有以色列人应该进行忏悔洗礼。
25 Yohane alipokuwa anamaliza ujumbe wake aliwaambia watu: Mnadhani mimi ni nani? Mimi si yule mnayemtazamia. Huyo anakuja baada yangu na mimi sistahili hata kuzifungua kamba za viatu vyake.
约翰即将完成他的使命时说:‘你们以为我是谁?我不是你们所寻找的那个人。但在我之后来的那个人,我就是给他解鞋带都不配。’
26 “Ndugu, ninyi mlio watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wengine wote mnaomcha Mungu! Ujumbe huu wa wokovu umeletwa kwetu.
兄弟们、亚伯拉罕的子孙以及敬畏上帝的众人,这救赎之道已传授给我们。
27 Kwa maana wenyeji wa Yerusalemu na wakuu wao hawakumtambua yeye kuwa Mwokozi. Wala hawakuelewa maneno ya manabii yanayosomwa kila Sabato. Hata hivyo, waliyafanya maneno ya manabii yatimie kwa kumhukumu Yesu adhabu ya kifo.
住在耶路撒冷的众人和他们的长官,他们不认识基督,也不理解安息日所读的先知之语。事实上,他们为耶稣定罪恰好应验了先知的预言。
28 Ingawa hawakumpata na hatia inayostahili auawe, walimwomba Pilato amhukumu auawe.
尽管他们无法找到宣判他死刑的罪状,但还是要求彼拉多杀害他。
29 Na baada ya kutekeleza yote yaliyokuwa yameandikwa kumhusu yeye, walimshusha kutoka msalabani, wakamweka kaburini.
预言中关于他们会对耶稣所做的一切,都应验了。然后他们把耶稣从十字架上取下并埋葬在坟墓中。
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
但上帝却使他死而复活。
31 Naye, kwa siku nyingi aliwatokea wale waliofuatana naye kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu. Hao ndio walio sasa mashahidi wake kwa watu wa Israeli.
多日后,他显现在那些从加利利到耶路撒冷一路跟随他的人面前,那些人现在就成了他在民众面前的见证者。
32 Sisi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu amelitimiza sasa kwa ajili yetu sisi tulio wajukuu wao kwa kumfufua Yesu kutoka wafu.
我们来此是向你们传递福音,通过耶稣的复活,上帝向我们祖先的承诺
33 Kama ilivyoandikwa katika zaburi ya pili: Wewe ni Mwanangu, mimi leo nimekuwa baba yako.
都已向我们这些子孙应验了。就如《诗篇》第二篇所记:‘你是我子,今日我成为你父。’
34 Na juu ya kumfufua kutoka wafu, asipate tena kurudi huko na kuoza, Mungu alisema hivi: Nitakupa baraka takatifu na za kweli nilizomwahidia Daudi.
上帝使他死而复生,不会再死去。他曾这样说:‘正如我向大卫所做的承诺,我所赐予你们的,神圣而值得相信。’
35 Naam, na katika sehemu nyingine za zaburi asema: Hutamwacha Mtakatifu wako aoze.
《诗篇》 还说:‘你不会允许圣者见到腐朽。’
36 Sasa, Daudi mwenyewe alitimiza mapenzi ya Mungu wakati wake; kisha akafa na kuzikwa karibu na wazee wake, na mwili wake ukaoza.
但大卫在自己的世界中完成了上帝派给他的使命后,就死去了,与他的祖先葬在一起,躯体也腐朽了。
37 Lakini yule ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu hakupata kuoza.
唯独上帝令其复活这一人,没有看到腐朽。
38 Jueni wazi, ndugu zangu, kwamba ujumbe kuhusu kusamehewa dhambi unahubiriwa kwenu kwa njia ya Yesu Kristo;
兄弟们,我希望你们理解我们正在讲述的一切,通过这个人,罪已经得到了宽恕。
39 na ya kwamba kila mmoja anayemwamini Yesu anasamehewa dhambi zote, jambo ambalo halingewezekana kwa njia ya Sheria ya Mose.
通过这个人,所有信他之人都会远离错误,实现道德正义, 但凭着摩西的律法,你永远都无法达到这种正义。
40 Jihadharini basi, msije mkapatwa na yale yaliyosemwa na manabii:
务必不能让先知在书上所说降临在你们身上:
41 Sikilizeni enyi wenye madharau, shangaeni mpotee! Kwa maana kitu ninachofanya sasa, nyakati zenu, ni kitu ambacho hamtakiamini hata kama mtu akiwaelezeni.”
‘傲慢的人呐!你们会惊奇地看到,然后死去!因为我在你们生命中所做的事情,即使有人向你讲述,你也永远都无法相信!’”
42 Paulo na Barnaba walipokuwa wanatoka katika ile sunagogi, wale watu waliwaalika waje tena siku ya Sabato iliyofuata, waongee zaidi juu ya mambo hayo.
保罗和巴拿巴打算离开,众人请他们在下一个安息日再来讲述更多。
43 Mkutano huo ulipomalizika, Wayahudi wengi na watu wa mataifa mengine waliokuwa wameongokea dini ya Kiyahudi waliwafuata Paulo na Barnaba. Hao mitume waliongea nao, wakawatia moyo waendelee kuishi wakitegemea neema ya Mungu.
这次会堂的聚会结束后,许多犹太人和归信犹太教的虔诚教徒,都跟随了保罗和巴拿巴。两人和他们交流,鼓励他们始终紧随上帝的恩典。
44 Siku ya Sabato iliyofuata, karibu kila mtu katika ule mji alikuja kusikiliza neno la Bwana.
到了下一个安息日,几乎全城的人都赶来,希望聆听上帝之道。
45 Lakini Wayahudi walipoliona hilo kundi la watu walijaa wivu, wakapinga alichokuwa anasema Paulo na kumtukana.
犹太人看见这攒动人群,感到异常嫉妒,于是开始驳斥保罗所讲之道,诅咒他。
46 Hata hivyo, Paulo na Barnaba waliongea kwa uhodari zaidi, wakasema, “Ilikuwa ni lazima neno la Mungu liwafikieni ninyi kwanza; lakini kwa kuwa mmelikataa na kujiona hamstahili uzima wa milele, basi, tunawaacheni na kuwaendea watu wa mataifa mengine. (aiōnios g166)
保罗和巴拿巴却强有力地回应:“我们必须先向你们讲述上帝之道。既然你们拒绝这道,就代表你们觉得自己不配获得永生,所以我们现在要去异教徒那里去了。 (aiōnios g166)
47 Maana Bwana alituagiza hivi: Nimekuteua wewe uwe mwanga kwa mataifa, uwe njia ya wokovu kwa ulimwengu wote.”
主吩咐过我们说:‘我让你们成为异教徒的光,你们将把拯救带到世界的尽头。’”
48 Watu wa mataifa mengine waliposikia jambo hilo walifurahi, wakausifu ujumbe wa Mungu; na wale waliokuwa wamechaguliwa kupata uzima wa milele, wakawa waumini. (aiōnios g166)
异教徒听见这个消息分外欢喜,赞美主之道,所有被选为永生之人都相信了上帝。 (aiōnios g166)
49 Neno la Bwana likaenea kila mahali katika sehemu ile.
上帝之道就这样传遍那个地区。
50 Lakini Wayahudi waliwachochea wanawake wa tabaka ya juu wa mataifa mengine ambao walikuwa wacha Mungu, na wanaume maarufu wa mji huo. Wakaanza kuwatesa Paulo na Barnaba, wakawafukuza kutoka katika eneo lao.
但犹太人教唆虔诚的尊贵女性和城中的首领,煽动大家迫害保罗和巴拿巴,把他们驱逐出境。
51 Basi, mitume wakayakung'uta mavumbi yaliyokuwa katika miguu yao kama onyo, kisha wakaenda Ikonio.
于是两人当众跺掉脚上的尘土以示抗议,向以哥念走去。
52 Lakini hao wafuasi walikuwa wamejaa furaha na Roho Mtakatifu.
而信徒们继续满心欢喜并被圣灵充满。

< Matendo 13 >