< Matendo 11 >

1 Mitume na ndugu kule Yudea walisikia kwamba watu wa mataifa mengine pia walikuwa wamelipokea neno la Mungu.
Los apóstoles y los hermanos que estaban en Judea oyeron que también los gentiles habían recibido la palabra de Dios.
2 Basi, Petro aliporudi Yerusalemu, wale Wayahudi waumini waliopendelea watu wa mataifa mengine watahiriwe, walimlaumu wakisema:
Cuando Pedro subió a Jerusalén, los que eran de la circuncisión discutieron con él,
3 “Wewe umekwenda kukaa na watu wasiotahiriwa na hata umekula pamoja nao!
diciendo: “¡Te acercaste a los incircuncisos y comiste con ellos!”
4 Hapo Petro akawaeleza kinaganaga juu ya yale yaliyotendeka tangu mwanzo:
Pero Pedro comenzó, y les explicó por orden, diciendo:
5 “Siku moja nikiwa nasali mjini Yopa, niliona maono; niliona kitu kama shuka kubwa likishushwa chini kutoka mbinguni likiwa limeshikwa pembe zake nne, likawekwa kando yangu.
“Yo estaba en la ciudad de Jope orando, y en trance vi una visión: un cierto recipiente que descendía, como si fuera una gran sábana bajada del cielo por cuatro esquinas. Llegó hasta mí.
6 Nilichungulia ndani kwa makini nikaona wanyama wenye miguu minne, wanyama wa mwituni, wanyama watambaao na ndege wa angani.
Cuando lo miré atentamente, consideré y vi los cuadrúpedos de la tierra, los animales salvajes, los reptiles y las aves del cielo.
7 Kisha nikasikia sauti ikiniambia: Petro amka, chinja, ule.
También oí una voz que me decía: “¡Levántate, Pedro, mata y come!”
8 Lakini mimi nikasema: La, Bwana; maana chochote kilicho najisi au kichafu hakijapata kamwe kuingia kinywani mwangu.
Pero yo dije: “No, Señor, porque en mi boca nunca ha entrado nada impuro o inmundo.
9 Ile sauti ikasikika tena kutoka mbinguni: Usiviite najisi vitu ambavyo Mungu amevitakasa.
Pero una voz me respondió por segunda vez desde el cielo: ‘Lo que Dios ha limpiado, no lo llames impuro’.
10 Jambo hilo lilifanyika mara tatu, na mwishowe vyote vilirudishwa juu mbinguni.
Esto se hizo tres veces, y todos fueron llevados de nuevo al cielo.
11 Ghafla, watu watatu waliokuwa wametumwa kwangu kutoka Kaisarea waliwasili kwenye nyumba niliyokuwa nakaa.
He aquí que en seguida se presentaron tres hombres ante la casa donde yo estaba, enviados desde Cesarea a mí.
12 Roho aliniambia niende pamoja nao bila kusita. Hawa ndugu sita waliandamana nami pia kwenda Kaisarea na huko tuliingia nyumbani mwa Kornelio.
El Espíritu me dijo que fuera con ellos sin discriminar. Me acompañaron también estos seis hermanos, y entramos en la casa de aquel hombre.
13 Yeye alitueleza jinsi alivyokuwa amemwona malaika amesimama nyumbani mwake na kumwambia: Mtume mtu Yopa akamwite mtu mmoja aitwaye Simoni, kwa jina lingine Petro.
Nos contó cómo había visto al ángel de pie en su casa, diciéndole: “Envía a Jope y trae a Simón, que se llama Pedro,
14 Yeye atakuambia maneno ambayo kwayo wewe na jamaa yako yote mtaokolewa.
que te hablará palabras por las que te salvarás tú y toda tu casa”.
15 Na nilipoanza tu kuongea, Roho Mtakatifu aliwashukia kama alivyotushukia sisi pale awali.
Cuando comencé a hablar, el Espíritu Santo cayó sobre ellos, como sobre nosotros al principio.
16 Hapo nilikumbuka yale maneno Bwana aliyosema: Yohane alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.
Me acordé de la palabra del Señor, que había dicho: “Juan bautizó en agua, pero vosotros seréis bautizados en el Espíritu Santo.
17 Basi, kama Mungu amewapa pia watu wa mataifa mengine zawadi ileile aliyotupa sisi tulipomwamini Bwana Yesu Kristo, je, mimi ni nani hata nijaribu kumpinga Mungu?”
Si, pues, Dios les concedió el mismo don que a nosotros, cuando creímos en el Señor Jesucristo, ¿quién era yo para resistir a Dios?”
18 Waliposikia hayo, waliacha ubishi, wakamtukuza Mungu wakisema, “Mungu amewapa watu wa mataifa mengine nafasi ya kutubu na kuwa na uzima!”
Al oír estas cosas, callaron y glorificaron a Dios, diciendo: “¡Entonces Dios también ha concedido a los gentiles el arrepentimiento para la vida!”
19 Kutokana na mateso yaliyotokea wakati Stefano alipouawa, waumini walitawanyika. Wengine walikwenda mpaka Foinike, Kupro na Antiokia wakihubiri ule ujumbe kwa Wayahudi tu.
Así pues, los que estaban dispersos por la opresión que surgió en torno a Esteban viajaron hasta Fenicia, Chipre y Antioquía, sin hablar a nadie más que a los judíos.
20 Lakini baadhi ya waumini waliotoka Kupro na Kurene, walikwenda Antiokia wakautangaza huo ujumbe kwa watu wa mataifa mengine wakiwahubiria ile Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
Pero hubo algunos de ellos, hombres de Chipre y de Cirene, que, cuando llegaron a Antioquía, hablaron a los helenistas, predicando al Señor Jesús.
21 Bwana aliwasaidia na idadi kubwa ya watu iliamini na kumgeukia Bwana.
La mano del Señor estaba con ellos, y un gran número creyó y se convirtió al Señor.
22 Habari ya jambo hilo ikasikika kwa lile kanisa la Yerusalemu. Hivyo wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
La noticia sobre ellos llegó a oídos de la asamblea que estaba en Jerusalén. Enviaron a Bernabé para que fuera hasta Antioquía,
23 Alipofika huko na kuona jinsi Mungu alivyowaneemesha wale watu, alifurahi na kuwahimiza wote wadumu katika uaminifu wao kwa Bwana.
el cual, cuando llegó y vio la gracia de Dios, se alegró. Los exhortó a todos, para que con propósito de corazón permanecieran cerca del Señor.
24 Barnaba alikuwa mtu mwema na mwenye kujaa Roho Mtakatifu na imani. Kundi kubwa la watu lilivutwa kwa Bwana.
Porque era un hombre bueno, lleno del Espíritu Santo y de fe, y se añadía mucha gente al Señor.
25 Kisha, Barnaba alikwenda Tarso kumtafuta Saulo
Bernabé salió a buscar a Saulo a Tarso.
26 Alipompata, alimleta Antiokia. Nao wote wawili walikaa na lile kanisa kwa mwaka wote mzima wakifundisha kundi kubwa la watu. Huko Antiokia, ndiko, kwa mara ya kwanza, wafuasi waliitwa Wakristo.
Cuando lo encontró, lo llevó a Antioquía. Durante todo un año estuvieron reunidos con la asamblea, y enseñaron a mucha gente. Los discípulos fueron llamados por primera vez cristianos en Antioquía.
27 Wakati huohuo, manabii kadhaa walikuja Antiokia kutoka Yerusalemu.
En aquellos días, los profetas bajaron de Jerusalén a Antioquía.
28 Basi, mmoja wao aitwaye Agabo alisimama, na kwa uwezo wa Roho akabashiri kwamba kutakuwa na njaa kubwa katika nchi yote (Njaa hiyo ilitokea wakati Klaudio alipokuwa akitawala).
Uno de ellos, llamado Agabo, se levantó e indicó por el Espíritu que habría una gran hambruna en todo el mundo, como también ocurrió en los días de Claudio.
29 Wale wanafunzi waliamua kila mmoja kwa kadiri ya uwezo wake apeleke chochote ili kuwasaidia wale ndugu waliokuwa wanaishi Yudea.
Como alguno de los discípulos tenía abundancia, cada uno determinó enviar socorro a los hermanos que vivían en Judea;
30 Basi, wakafanya hivyo na kupeleka mchango wao kwa wazee wa kanisa kwa mikono ya Barnaba na Saulo.
lo que también hicieron, enviándolo a los ancianos por medio de Bernabé y Saulo.

< Matendo 11 >