< Matendo 1 >

1 Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
Pierwszą księgę napisałem, Teofilu, o wszystkim, co Jezus zaczął czynić i [czego] nauczać;
2 mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
Aż do dnia, w którym został wzięty w górę po tym, jak przez Ducha Świętego udzielił poleceń apostołom, których wybrał.
3 Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
Im też po swojej męce objawił się [jako] żywy w wielu niewątpliwych dowodach, przez czterdzieści dni ukazując się im i mówiąc o królestwie Bożym.
4 Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: “Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
A gdy byli zebrani razem, nakazał im: Nie odchodźcie z Jerozolimy, ale oczekujcie obietnicy Ojca, o której słyszeliście ode mnie.
5 Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
Jan bowiem chrzcił wodą, ale wy po niewielu dniach będziecie ochrzczeni Duchem Świętym.
6 Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, “Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?”
Tak więc zebrani pytali go: Panie, czy w tym czasie przywrócisz królestwo Izraelowi?
7 Lakini Yesu akawaambia, “Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
Lecz on im odpowiedział: Nie do was należy znać czasy i pory, które Ojciec ustanowił swoją władzą.
8 Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia.”
Ale przyjmiecie moc Ducha Świętego, który zstąpi na was, i będziecie mi świadkami w Jerozolimie, w całej Judei, w Samarii i aż po krańce ziemi.
9 Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
Kiedy to powiedział, a oni patrzyli, został uniesiony w górę i obłok zabrał go sprzed ich oczu.
10 Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
A gdy się wpatrywali w niebo, jak wstępował, oto stanęli przy nich dwaj mężowie w białych szatach;
11 wakasema, “Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni.”
I powiedzieli: Mężowie z Galilei, dlaczego stoicie, wpatrując się w niebo? Ten Jezus, który został od was wzięty w górę do nieba, przyjdzie tak samo, jak go widzieliście wstępującego do nieba.
12 Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
Wtedy wrócili do Jerozolimy z góry zwanej Oliwną, która leży blisko Jerozolimy, w odległości drogi szabatowej.
13 Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
A gdy przyszli, weszli do sali na górze, gdzie przebywali Piotr i Jakub, Jan i Andrzej, Filip i Tomasz, Bartłomiej i Mateusz, Jakub, [syn] Alfeusza, i Szymon Zelota oraz Juda, [brat] Jakuba.
14 Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
Ci wszyscy trwali jednomyślnie w modlitwie i prośbach [razem] z kobietami, z Marią, matką Jezusa, i jego braćmi.
15 Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
W tych dniach Piotr stanął pośród uczniów (a było zgromadzonych około stu dwudziestu osób) i powiedział:
16 akasema, “Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
Mężowie bracia, musiało się wypełnić [słowo] Pisma, w którym Duch Święty zapowiedział przez usta Dawida o Judaszu, który był przewodnikiem tych, którzy schwytali Jezusa.
17 Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
Zaliczał się on bowiem do nas i miał udział w tym posługiwaniu.
18 (“Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
On nabył pole za zapłatę za nieprawość i spadłszy głową w dół, pękł na pół i wypłynęły wszystkie jego wnętrzności.
19 Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
Rozniosło się to wśród wszystkich mieszkańców Jerozolimy, tak że nazwano to pole w ich języku Hakeldamach, to znaczy: Pole Krwi.
20 Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
Jest bowiem napisane w Księdze Psalmów: Niech jego dom będzie pusty, niech nikt w nim nie mieszka; oraz: Jego biskupstwo niech przejmie inny.
21 Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
Trzeba więc, aby jeden z tych mężczyzn, którzy z nami byli przez cały czas, kiedy Pan Jezus przebywał wśród nas;
22 Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni.”
Począwszy od chrztu Jana aż do dnia, w którym został wzięty od nas w górę, stał się wraz z nami świadkiem jego zmartwychwstania.
23 Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
I wybrali dwóch: Józefa, zwanego Barsabą, z przydomkiem Justus, i Macieja.
24 Kisha wakasali: “Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
I tak się modlili: Ty, Panie, który znasz serca wszystkich, wskaż z tych dwóch jednego, którego wybrałeś;
25 ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe.”
Aby zajął miejsce w tym posługiwaniu i apostolstwie, któremu sprzeniewierzył się Judasz, aby odejść na swoje miejsce.
26 Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.
I dali im losy, a los padł na Macieja. I został przyłączony do jedenastu apostołów.

< Matendo 1 >