< 3 Yohana 1 >

1 Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
A ham loh thintlo Kaiyu te ka yaak sak. Anih he kai loh oltak neh ka lungnah.
2 Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
Thintlo aw, na hinglu loh a hoeikhang vanbangla, a cungkuem dongah nang hoeikhang sak ham neh sading sak ham ka thangthui.
3 Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
Oltak dongah na pongthoh vanbangla, manuca aka pawk rhoek loh oltak ah na om te khaw a phong uh dongah bahoeng ka omngaih.
4 Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
Ka ca rhoek te oltak dongah pongpa uh tila ka yaak vaengah, hekah lakah a lenngai omngaihnah ka khueh moenih.
5 Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
Thintlo aw, manuca rhoek neh olpuei la yinlai rhoek ham na saii te khaw uepom la saii.
6 Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
Amih loh hlangboel hmaiah nang kah lungnah a phong uh. Pathen neh a tingtawk la amih thak ham te a then la saii.
7 Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
Boeipa ming ham cet uh dae namtom rhoek taengkah a bawn uh moenih.
8 Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
Mamih loh tebang te doo ham a kuek tangloeng. Te daengah ni oltak dongah bibipuei la n'om uh eh.
9 Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
Hlangboel ham bet ka daek dae amih ah aka tanglue Diotrephi loh mamih n'doe moenih.
10 Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
Te dongah, ka pawk atah, anih kah a saii khoboe te ka thoelh ni. Mamih te rhaithae olka m'pup thil. He nen khaw a rhaemhal kolla manuca rhoek te a doe moenih. Te phoeiah doe ham aka cai rhoek te a paa sak dongah hlangboel lamkah a thaek.
11 Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
Thintlo rhoek, a thae te awt boel lamtah a then te awtuh. Aka then tah Pathen kah la om. Aka thae loh Pathen te a hmuh moenih.
12 Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
Demetrius te a cungkuem neh oltak amah lamloh a phong coeng. Te dongah mamih khaw m'phong uh. Te vaengah mamih kah laipainah tah oltak ni tila na ming uh.
13 Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
Nang taengah daek ham muep ka khueh dae nang ham cahang neh cacung neh daek ham ka ngaih moenih.
14 Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.
Tedae nangmih te tlek hmuh ham ka ngaiuep. Te vaengah ka neh ka rhoi te n'thui bitni. Nang taengah ngaimongnah om seh. Paya rhoek loh nang toidal uh. Paya rhoek te a ming neh toidal lah.

< 3 Yohana 1 >