< 2 Wakorintho 12 >

1 Nitajivuna basi, ingawa haifai! Lakini sasa nitasema juu ya maono na ufunuo alivyonijalia Bwana.
(Really, to me boasting is not helpful.) For I will come to visions and revelations of the Lord.
2 Namjua mtu mmoja Mkristo, ambaye miaka kumi na minne iliyopita alinyakuliwa mpaka katika mbingu ya tatu. (Sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
I know a man in Christ, fourteen years ago (whether in body, I know not, or whether outside the body, I know not, God knows) such a man was caught up as far as the third heaven.
3 Narudia: najua kwamba mtu huyo alinyakuliwa mpaka peponi. (Lakini sijui kama alikuwa huko kwa mwili au kwa roho; Mungu ajua.)
And I know such a man (whether in body, or whether outside the body, I know not, God knows)
4 Huko akasikia mambo ya siri ambayo binadamu hastahili kuyatamka.
that he was caught up into the paradise, and heard inexpressible sayings that are not permitted for a man to utter.
5 Basi, nitajivunia juu ya mtu wa namna hiyo, na si juu yangu mimi binafsi, isipokuwa tu juu ya udhaifu wangu.
For such a man I will boast, but for myself I will not boast, except in my weaknesses.
6 Kama ningetaka kujivuna singekuwa mpumbavu hata kidogo, maana ningekuwa nasema ukweli mtupu. Lakini sitajivuna; sipendi mtu anifikirie zaidi ya vile anavyoona na kusikia kutoka kwangu.
For if I should want to boast, I will not be foolish, for I will speak the truth. But I refrain lest any man should reckon to me above what he sees of me or hears anything from me.
7 Lakini, kusudi mambo haya makuu niliyofunuliwa yasinifanye nilewe majivuno, nilipewa maumivu mwilini kama mwiba, mjumbe wa Shetani mwenye kunipiga nisijivune kupita kiasi.
And so that I might not be over exalted by the extraordinariness of the revelations, there was given to me a thorn in the flesh, an agent of Satan so that he would buffet me, so that I would not be over exalted.
8 Nilimsihi Bwana mara tatu kuhusu jambo hili ili linitoke.
I besought the Lord thrice about this, that it might depart from me.
9 Lakini akaniambia: “Neema yangu inatosha kwa ajili yako; maana uwezo wangu hukamilishwa zaidi katika udhaifu.” Basi, ni radhi kabisa kujivunia udhaifu wangu ili uwezo wake Kristo ukae juu yangu.
And he said to me, My grace is sufficient for thee, for my power is made fully perfect in weakness. More gladly therefore I will boast in my weaknesses, so that the power of the Christ may reside in me.
10 Kwa hiyo nakubali kwa radhi udhaifu, madharau, taabu, udhalimu na mateso, kwa ajili ya Kristo; maana ninapokuwa dhaifu, ndipo ninapokuwa na nguvu.
Therefore I am pleased in weaknesses, in injuries, in necessities, in persecutions, in restrictions, for the sake of Christ. For when I am weak, then I am strong.
11 Nimekuwa kama mpumbavu, lakini, ninyi mmenilazimisha kuwa hivyo. Ninyi ndio mngalipaswa kunisifu. Maana, ingawa mimi si kitu, kwa vyovyote, mimi si mdogo zaidi kuliko hao “mitume wakuu.”
I have become foolish, boasting. Ye compelled me, for I ought to have been commended by you. For I came short in nothing of those, superlative apostles, even though I am nothing.
12 Miujiza na maajabu yaonyeshayo wazi kwamba mimi ni mtume yalifanyika miongoni mwenu kwa uvumilivu wote.
Indeed the signs of the apostle were performed among you in all perseverance, in signs and wonders and mighty works.
13 Je, mlipungukiwa nini zaidi kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi kwa upande wangu sikuwasumbueni kupata msaada wenu? Samahani kwa kuwakoseeni haki hiyo!
For what is there which ye were inferior to the other congregations? Except that I myself was not burdensome to you? Forgive me this wrong.
14 Sasa niko tayari kabisa kuja kwenu mara ya tatu, na sitawasumbua. Maana ninachotafuta si mali zenu, bali ni ninyi wenyewe. Ni kawaida ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba, na si watoto kuwawekea wazazi wao.
Behold, a third time I fare readily to come to you, and I will not be burdensome to you, for I seek not the things of you, but you. For the children ought not lay up for the parents, but the parents for the children.
15 Mimi ni radhi kabisa kutumia nilicho nacho, na hata kujitolea mimi mwenyewe kabisa, kwa faida ya roho zenu. Je, mtanipenda kidogo ati kwa kuwa mimi nawapenda ninyi mno?
And I most gladly will spend, and will be spent for your souls. Even though more earnestly loving you, the worse I am loved.
16 Basi, mtakubali kwamba sikuwa mzigo kwenu. Lakini labda mtu mwingine atasema: “Kwa vile Paulo ni mwerevu, amewafanyieni ulaghai.”
But let it be. I did not burden you. Nevertheless, being clever, I caught you with bait.
17 Je, mimi niliwanyonyeni kwa njia ya mjumbe yeyote niliyemtuma kwenu?
Any man of whom I have sent to you, did I exploit you through him?
18 Mimi nilimwita Tito, nikamtuma kwenu na ndugu yetu mwingine. Je, Tito aliwanyonyeni? Je, hamjui kwamba sisi tumekuwa tukiongozwa na roho yuleyule, na mwenendo wetu ni mmoja?
I encouraged Titus, and I sent the brother with him. Did Titus exploit you in anything? Did we not walk in the same spirit, not in the same steps?
19 Labda mnafikiri kwamba mpaka sasa tumekuwa tukijitetea wenyewe mbele yenu! Lakini, tunasema mambo haya mbele ya Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo. Mambo hayo, yote, wapenzi wangu, ni kwa ajili ya kuwajenga ninyi.
Again, do ye think that we are making defense to you? In the sight of God we speak in Christ. But all things, beloved, are for your edification.
20 Naogopa, huenda nitakapokuja kwenu nitawakuta katika hali nisiyopenda, nami itanilazimu kuwa katika hali msiyoipenda. Naogopa huenda kukawa na ugomvi, wivu, uhasama, ubishi, masengenyano, kunong'ona, majivuno na fujo kati yenu.
For I fear lest somehow, having come, I may find you not such as I want, and I may be found by you such as ye do not want, lest somehow there be strifes, envyings, wraths, selfish ambitions, slanderings, whisperings, puffings up, turmoils,
21 Naogopa huenda hapo nitakapokuja safari ijayo Mungu wangu atanifanya niaibike mbele yenu, nami nitaomboleza kwa ajili ya wengi wa wale waliotenda dhambi lakini hawakujutia huo uchafu, tamaa zao mbaya na uzinzi waliokuwa wamefanya.
lest having come again my God will make me low toward you, and I will bewail many of those who have sinned previously, and who did not repent from the trash and fornication and licentiousness that they committed.

< 2 Wakorintho 12 >