< 1 Wathesalonike 3 >

1 Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
Wherefore, no longer concealing our anxiety, we were well-pleased to be left in Athens, alone,
2 na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
And sent Timothy—our brother, and God’s minister in the glad-message of the Christ—that he might confirm and console you over your faith,
3 kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
That, no one, might be shrinking back in these tribulations. For ye, yourselves, know, that, hereunto, are we appointed;
4 Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
For, even when we were with you, we told you beforehand—we are destined to suffer tribulation! even as it also came to pass, and ye know.
5 Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
For this cause, I also, no longer concealing my anxiety, sent, that I might get to know your faith, lest by any means he that tempteth, should have tempted you, and, in vain, should have been our toil.
6 Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
But, when, just now, Timothy came unto us, from you, and brought us good tidings of your faith and love, —and that ye have good remembrance of us, continually, longing to see, us, —even as, we also, to see you,
7 Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
For this cause, were we consoled, brethren, over you, in all our necessity and tribulation, through your faith;
8 kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
Because, now, we live, —if only, ye, stand fast in the Lord.
9 Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
For what thanksgiving can we render back, unto God, concerning you, on occasion of all the joy wherewith we rejoice, for your sakes, before our God?—
10 Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
Night and day, making very abundant entreaties, that we may see your face, and fit in the things which are lacking in your faith?
11 Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
Now may, our God and Father himself and our Lord Jesus, make straight our way unto you:
12 Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
And, you, may the Lord cause to abound and excel in your love one toward another, and toward all, —even as, we, do toward you:
13 Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.
To the end he may confirms your hearts, faultless in holiness, before our God and Father, in the Presence of our Lord Jesus with all his saints.

< 1 Wathesalonike 3 >