< 1 Wathesalonike 3 >

1 Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
Wherefore, being no longer able to contain ourselves, we thought it good to be left at Athens alone;
2 na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
and we sent Timothy our brother and minister of God in the gospel of the Christ, in order that he might strengthen and comfort you with respect to your faith,
3 kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
that no one be moved by these afflictions; for you yourselves know that we are appointed to this:
4 Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
for even when we were with you, we told you beforehand that we were about to be afflicted, as it also came to pass, and as you know.
5 Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
For this reason, when I could no longer contain myself, I sent to know your faith, lest by any means the tempter had tempted you, and our labor should be in vain.
6 Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
But now, since Timothy has come to us from you, and has told us the good news of your faith and love, and that you have a good remembrance of us at all times, greatly desiring to see us, as indeed we desire to see you,
7 Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
for this reason we are comforted concerning you, brethren, in all our distress and affliction, by your faith:
8 kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
for now we live, if you stand firm in the Lord.
9 Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
For what thanks can we render to God for you, for the great joy with which we rejoice on your account before our God,
10 Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
night and day praying exceedingly that we may see your face, and perfect that which is lacking in your faith?
11 Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
Now, may God himself, even our Father, and the Lord Jesus Christ, direct our way to you.
12 Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
And may the Lord cause you to increase and abound in love to one another and to all, even as we toward you,
13 Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.
in order that he may establish your hearts blameless in holiness, in the presence of our God and Father, at the coming of our Lord Jesus Christ with all his saints.

< 1 Wathesalonike 3 >