< 1 Yohana 4 >

1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Umiłowani, nie wierzcie każdemu duchowi, ale badajcie duchy, czy są z Boga, gdyż wielu fałszywych proroków wyszło na świat.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
Po tym poznacie Ducha Bożego: każdy duch, który wyznaje, że Jezus Chrystus przyszedł w ciele, jest z Boga.
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
Każdy zaś duch, który nie wyznaje, że Jezus Chrystus przyszedł w ciele, nie jest z Boga. Jest to [duch] antychrysta, o którym słyszeliście, że nadchodzi i już teraz jest na świecie.
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
Dzieci, wy jesteście z Boga i zwyciężyliście ich, ponieważ ten, który [jest] w was, jest większy niż [ten, który] jest na świecie.
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
Oni są ze świata, dlatego mówią o świecie, a świat ich słucha.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
My jesteśmy z Boga. Kto zna Boga, słucha nas, kto nie jest z Boga, nie słucha nas. Po tym poznajemy ducha prawdy i ducha błędu.
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Umiłowani, miłujmy się wzajemnie, gdyż miłość jest z Boga i każdy, kto miłuje, narodził się z Boga i zna Boga.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
Kto nie miłuje, nie zna Boga, gdyż Bóg jest miłością.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
Przez to objawiła się miłość Boga ku nam, że Bóg posłał na świat swego jednorodzonego Syna, abyśmy żyli przez niego.
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
Na tym polega miłość, że nie my umiłowaliśmy Boga, ale że on nas umiłował i posłał swego Syna, [aby był] przebłaganiem za nasze grzechy.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
Umiłowani, jeśli Bóg tak nas umiłował, to i my powinniśmy się wzajemnie miłować.
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
Boga nikt nigdy nie widział, [ale] jeśli miłujemy się wzajemnie, Bóg w nas mieszka, a jego miłość jest w nas doskonała.
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
Po tym poznajemy, że w nim mieszkamy, a on w nas, że dał nam ze swego Ducha.
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
My zaś widzieliśmy i świadczymy, że Ojciec posłał Syna, aby był Zbawicielem świata.
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
Każdy, kto wyzna, że Jezus jest Synem Bożym, w tym mieszka Bóg, a on w Bogu.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
My poznaliśmy i uwierzyliśmy w miłość, którą ma Bóg do nas. Bóg jest miłością, a kto trwa w miłości, mieszka w Bogu, a Bóg w nim.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
W tym jest doskonała miłość w nas, abyśmy mieli ufność w dniu sądu, że jaki on jest, tacy i my jesteśmy na tym świecie.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
W miłości nie ma lęku, ale doskonała miłość usuwa lęk, bo lęk przynosi udrękę, [a] kto się boi, nie jest doskonały w miłości.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
My go miłujemy, ponieważ on pierwszy nas umiłował.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
Jeśli ktoś mówi: Miłuję Boga, a nienawidzi swego brata, jest kłamcą. Kto bowiem nie miłuje swego brata, którego widzi, jak może miłować Boga, którego nie widzi?
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
A takie przykazanie mamy od niego, aby ten, kto miłuje Boga, miłował też swego brata.

< 1 Yohana 4 >