< 1 Yohana 4 >

1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Bien-aimés, ne croyez pas tout esprit, mais éprouvez les esprits, pour savoir s'ils sont de Dieu, car beaucoup de faux prophètes sont sortis dans le monde.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
C'est à ceci que vous connaissez l'Esprit de Dieu: tout esprit qui confesse que Jésus-Christ est venu en chair est de Dieu,
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
et tout esprit qui ne confesse pas que Jésus-Christ est venu en chair n'est pas de Dieu; c'est là l'esprit de l'Antéchrist, dont vous avez appris la venue. Or, il est déjà dans le monde.
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
Vous êtes de Dieu, petits enfants, et vous les avez vaincus, parce que celui qui est en vous est plus grand que celui qui est dans le monde.
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
Ils sont du monde. C'est pourquoi ils parlent du monde, et le monde les écoute.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
Nous, nous sommes de Dieu. Celui qui connaît Dieu nous écoute. Celui qui n'est pas de Dieu ne nous écoute pas. C'est à cela que nous connaissons l'esprit de vérité et l'esprit d'erreur.
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Bien-aimés, aimons-nous les uns les autres, car l'amour vient de Dieu; et quiconque aime est né de Dieu et connaît Dieu.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
Celui qui n'aime pas ne connaît pas Dieu, car Dieu est amour.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
C'est par cela que l'amour de Dieu s'est révélé en nous, que Dieu a envoyé son Fils unique dans le monde, afin que nous vivions par lui.
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
En ceci consiste l'amour, non pas que nous ayons aimé Dieu, mais qu'il nous ait aimés et ait envoyé son Fils comme sacrifice expiatoire pour nos péchés.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
Bien-aimés, si Dieu nous a aimés de cette manière, nous devons aussi nous aimer les uns les autres.
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
Personne n'a jamais vu Dieu. Si nous nous aimons les uns les autres, Dieu demeure en nous, et son amour est parfait en nous.
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
Nous savons par là que nous demeurons en lui et lui en nous, parce qu'il nous a donné de son Esprit.
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
Nous avons vu et nous témoignons que le Père a envoyé le Fils comme Sauveur du monde.
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
Quiconque confesse que Jésus est le Fils de Dieu, Dieu demeure en lui, et lui en Dieu.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
Nous savons et nous avons cru à l'amour que Dieu a pour nous. Dieu est amour, et celui qui demeure dans l'amour demeure en Dieu, et Dieu demeure en lui.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
En cela, l'amour a été rendu parfait parmi nous, afin que nous ayons de l'assurance au jour du jugement, car ce qu'il est, nous le sommes aussi dans ce monde.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
Il n'y a pas de crainte dans l'amour; mais l'amour parfait chasse la crainte, car la crainte a un châtiment. Celui qui craint n'est pas parfait dans l'amour.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
Nous l'aimons, parce qu'il nous a aimés le premier.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
Si quelqu'un dit: « J'aime Dieu », et qu'il haïsse son frère, c'est un menteur; car celui qui n'aime pas son frère qu'il a vu, comment peut-il aimer Dieu qu'il n'a pas vu?
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
Nous tenons de lui ce commandement: que celui qui aime Dieu aime aussi son frère.

< 1 Yohana 4 >