< 1 Yohana 4 >

1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Beloved, believe not every spirit, but try the spirits whether they are of God: because many false prophets have gone out into the world.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
By this ye know the Spirit of God: Every spirit that confesseth that Jesus Christ hath come in the flesh, is from God:
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
And every spirit that confesseth not that Jesus Christ is come in the flesh, is not from God. And this is that [spirit] of antichrist, of which ye have heard that it should come; and even now already it is in the world.
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
Ye are of God, little children, and have overcome them: because greater is he that is in you, than he that is in the world.
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
They are of the world: therefore they speak from the world, and the world heareth them.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
We are of God. He that knoweth God, heareth us; he that is not of God, heareth not us. By this we know the spirit of truth, and the spirit of error.
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Beloved, let us love one another: for love is from God; and every one that loveth is born of God, and knoweth God.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
He that loveth not, knoweth not God; for God is love.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
In this was manifested the love of God towards us, because that God sent his only begotten Son into the world, that we might live through him.
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
In this is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son [to be] the propitiation for our sins.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
Beloved, if God so loved us, we ought also to love one another.
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
No man hath seen God at any time. If we love one another, God dwelleth in us, and his love is perfected in us.
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
By this we know that we dwell in him, and he in us, because he hath given us of his Spirit.
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
And we have seen and do testify, that the Father sent the Son [to be] the Savior of the world.
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
Whoever shall confess that Jesus is the Son of God, God dwelleth in him, and he in God.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
And we have known and believed the love that God hath to us. God is love: and he that dwelleth in love, dwelleth in God, and God in him.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
In this is our love made perfect, that we may have boldness in the day of judgment: because as he is, so are we in this world.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
There is no fear in love; but perfect love casteth out fear: because fear hath torment. He that feareth, is not made perfect in love.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
We love him, because he first loved us.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
If a man sayeth, I love God, and hateth his brother, he is a liar. For he that loveth not his brother, whom he hath seen, how can he love God, whom he hath not seen?
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
And this commandment have we from him, That he who loveth God, love his brother also.

< 1 Yohana 4 >