< 1 Yohana 4 >

1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Dear friends, don't trust every spirit, but put the spirits to the test to find out whether they're from God, for there are many false prophets out there in the world.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
How can you recognize God's Spirit? Every spirit that accepts Jesus Christ came with a human body is from God;
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
while every spirit that doesn't accept Jesus, that spirit isn't from God. In fact it is the spirit of the antichrist which you heard was coming, and which is already in the world.
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
But you belong to God, my friends, and you have defeated them, for the one who is in you is greater than the one who is in the world.
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
They belong to the world, so they speak like people of the world, and the world listens to them.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
We belong to God and whoever knows God listens to us, while whoever doesn't belong to God doesn't listen to us. This is how we can distinguish the spirit of truth from the spirit of deception.
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Dear friends, let's go on loving one another, for love comes from God. All those who love are born of God and know God.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
Those who don't love don't know God, for God is love.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
How was God's love shown to us? God sent his one and only Son into the world so that we could live through him.
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
This is love! It's not that we loved God, but that he loved us, and he sent his Son to be the reconciliation for our sins.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
Friends, if this is the way God loves us, we ought to love one another like this too.
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
No one has ever seen God. However, if we love one another then God lives in us, and his love is fulfilled in us.
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
How can we know that we live in him, and that he lives in us? He's given us the ability to love by his Spirit.
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
For we are witnesses to what we have seen and testify that the Father sent the Son as the Savior of the world.
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
God lives in everyone who declares that Jesus is the Son of God, and they live in God.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
We have experienced and trusted in the love that God has for us. God is love, and those who live in love, live in God, and God lives in them.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
This is how love is made complete in us so that we can be confident on judgment day: by the fact that we live just like him in this world.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
Where there is love there can be no fear. God loves us completely, and this love drives all our fears away. If we do fear, it's because we fear being punished, and this shows that we have not been fully re-made by the completeness of God's love.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
We love because he loved us first.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
Anyone who says, “I love God,” but hates a Christian brother or sister, is a liar. Anyone who doesn't love a brother whom they can see, can't love God whom they can't see.
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
This is the command he gave to us: those who love God love their brothers and sisters too.

< 1 Yohana 4 >