< 1 Yohana 4 >

1 Wapenzi wangu, msimsadiki kila mtu asemaye kwamba ana Roho wa Mungu, bali chunguzeni kwa makini kama huyo mtu anaongozwa na Roho wa Mungu au la, Maana manabii wengi wa uongo wamezuka ulimwenguni.
Beloved, do not believe every spirit, but examine the spirits, whether they are of God, because many false prophets have gone out into the world.
2 Hii ndiyo njia ya kujua kama mtu anaongozwa na Roho wa Mungu: Kila anayekiri kwamba Kristo alikuja, akawa binadamu, mtu huyo anaye Roho wa Mungu.
By this ye know the Spirit of God: every spirit that confesses Jesus Christ having come in flesh is of God,
3 Lakini mtu yeyote asiyemkiri Kristo hivyo, hana huyo Roho atokaye kwa Mungu. Mtu huyo ana roho ambaye ni wa Adui wa Kristo; nanyi mlikwisha sikia kwamba anakuja, na sasa tayari amekwisha wasili ulimwenguni!
and every spirit that does not confess Jesus Christ has come in flesh is not of God. And this is that of the antichrist, which ye have heard that it comes, and is now in the world already.
4 Lakini ninyi, watoto, ni wake Mungu na mmekwisha washinda hao manabii wa uongo; maana Roho aliye ndani yenu ana nguvu zaidi kuliko roho aliye ndani ya hao walio wa ulimwengu.
Ye are of God, little children, and ye have overcome them, because greater is he in you than he in the world.
5 Wao husema mambo ya ulimwengu, nao ulimwengu huwasikiliza kwani wao ni wa ulimwengu.
They are of the world. Because of this they speak of the world, and the world hears them.
6 Lakini sisi ni wake Mungu. Mtu anayemjua Mungu hutusikiliza, mtu asiye wa Mungu hatusikilizi. Basi, kwa njia hiyo tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho wa uongo.
We are of God. He who knows God hears us. He who is not of God does not hear us. From this we know the spirit of truth, and the spirit of error.
7 Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu.
Beloved, we should love each other. Because love is of God, and every man who loves has been begotten of God, and knows God.
8 Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo.
He who does not love does not know God, because God is love.
9 Na Mungu alionyesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uzima kwa njia yake.
By this the love of God was made known in us, because God sent his Son, the only begotten, into the world so that we might live through him.
10 Hivi ndivyo upendo ulivyo: si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu.
In this is love, not that we loved God, but that he loved us, and sent his Son, an atonement for our sins.
11 Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.
Beloved, if God so loved us, we also are obligated to love each other.
12 Hakuna mtu aliyekwisha mwona Mungu kamwe; lakini kama tukipendana Mungu anaishi katika muungano nasi, na upendo wake unakamilika ndani yetu.
No man has ever seen God. If we love each other, God abides in us, and his love is in us, having been fully perfected.
13 Tunajua kwamba tunaishi katika umoja na Mungu, naye Mungu anaishi katika umoja nasi, kwani yeye ametupa Roho wake.
In this we know that we abide in him and he in us, because he has given us from his Spirit.
14 Sisi tumeona na kuwaambia wengine kwamba Baba alimtuma Mwanae awe Mwokozi wa ulimwengu.
And we have seen and testify that the Father has sent the Son, a Savior of the world.
15 Kila mtu anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu anaishi katika muungano na mtu huyo, naye anaishi katika muungano na Mungu.
Whoever acknowledges that Jesus is the Son of God, God abides in him, and he in God.
16 Basi, sisi tunajua na tunaamini upendo alio nao Mungu kwetu sisi. Mungu ni upendo, na kila mtu aishiye katika upendo, anaishi katika muungano na Mungu, na Mungu anaishi katika muungano naye.
And we know, and have believed the love that God has in us. God is love, and he who abides in love abides in God, and God abides in him.
17 Upendo umekamilika ndani yetu kusudi tuweze kuwa na ujasiri Siku ile ya Hukumu; kwani maisha yetu hapa duniani ni kama yale ya Kristo.
By this love has been fully perfected with us, so that we may have boldness in the day of judgment, because just as that man is, we also are in this world.
18 Palipo na upendo hapana uoga; naam, upendo kamili hufukuza uoga wote. Basi, mtu mwenye uoga hajakamilika bado katika upendo, kwani uoga huhusikana na adhabu.
Fear is not in love, but perfect love casts out fear, because fear holds punishment, and he who is afraid has not been fully perfected in love.
19 Sisi tuna upendo kwa sababu Mungu alitupenda kwanza.
We love him, because he first loved us.
20 Mtu akisema kwamba anampenda Mungu, hali anamchukia ndugu yake, huyo ni mwongo. Maana mtu asiyempenda ndugu yake ambaye anamwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hamwoni.
If any man says, I love God, and hates his brother, he is a liar. For he who does not love his brother whom he has seen, how can he love God whom he has not seen?
21 Basi, hii ndiyo amri aliyotupa Kristo: Anayempenda Mungu anapaswa pia kumpenda ndugu yake.
And we have this commandment from him, so that he who loves God will also love his brother.

< 1 Yohana 4 >