< 1 Wakorintho 5 >

1 Ziko habari za kuaminika kwamba kuna uzinzi miongoni mwenu; tena ni uzinzi mbaya ambao haujapata kuwako hata kati ya watu wasiomjua Mungu. Nimeambiwa eti mmoja wenu anaishi na mke wa baba yake!
Fornication is actually heard among you, and such fornication that is not even named among the Gentiles, for some man to have his father's wife.
2 Mnawezaje kujivuna? Ingekuwa afadhali kwenu kuomboleza, na huyo aliyefanya kitu hicho aondolewe miongoni mwenu.
And ye are puffed up and did not rather mourn, so that he who committed this deed might be taken away from the midst of you.
3 Nami, kwa upande wangu, ingawa kwa mwili niko mbali nanyi, hata hivyo kwa roho niko hapo pamoja nanyi: na hivyo, kama vile nipo hapo, nimekwisha mhukumu huyo aliyefanya jambo hilo la aibu.
For I truly, as being absent in the body but present in the spirit, I have already, as though present, judged the man who committed this thing this way.
4 Wakati mnapokusanyika pamoja kwa jina la Bwana Yesu, nami nikiwa pamoja nanyi kwa roho, basi, kwa uwezo wa Bwana wetu Yesu,
In the name of our Lord Jesus Christ, when ye are gathered together, and my spirit with the power of our Lord Jesus Christ,
5 mkabidhini mtu huyo kwa Shetani ili mwili wake uharibiwe na roho yake iweze kuokolewa Siku ile ya Bwana.
to deliver such a man to Satan for destruction of the flesh, so that the spirit might be saved in the day of the Lord Jesus.
6 Majivuno yenu hayafai! Je, hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge lote la unga?
Your boasting is not good. Know ye not that a little leaven leavens the whole lump?
7 Jitakaseni, mkatupe mbali chachu ya kale ili mpate kuwa donge jipya lisilotiwa chachu kama mnavyopaswa kuwa; maana, Kristo, Pasaka yetu, amekwisha tolewa tambiko.
Purge out the old leaven, so that ye may be a new lump, since ye are unleavened. For also Christ our Passover was sacrificed for us.
8 Basi, tufanye karamu hiyo si kwa chachu ile ya kale, chachu ya ubaya na uovu, bali kwa mkate usiotiwa chachu, mkate wa usafi na kweli.
Therefore we should feast, not by old leaven, nor by leaven of evil and wickedness, but by non-leaven of sincerity and truth.
9 Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi.
I wrote to you in the letter not to associate with fornicators,
10 Ukweli ni kwamba sikuwa na maana ya watu wote duniani walio wazinzi, wachoyo, walaghai na wenye kuabudu sanamu. Maana, ili kuwaepa hao wote ingewalazimu ninyi kuihama dunia hii kabisa!
and not at all with the fornicators of this world, or with greedy men, or with predators, or with idolaters, since then ye would need to go out of the world.
11 Nilichoandika ni hiki: msishirikiane na ndugu Mkristo aliye mzinzi, mchoyo, mwenye kuabudu sanamu, mchongezi mlevi na mlaghai. Mtu wa namna hiyo, hata kula msile naye.
But now I write to you not to associate if any man who is called a brother is a fornicator, or a greedy man, or an idolater, or a slanderer, or a drunkard, or a predator, not even to eat with such kind.
12 Je, ni shauri langu kuwahukumu watu walio nje? Hao Mungu atawahukumu. Je, ninyi hampaswi kuwahukumu wale walio katika jamii yenu ninyi wenyewe?
For what is in me to also judge those outside? Do ye not judge those inside?
13 Mfukuzeni mbali nanyi huyo mwovu!
But God judges those outside. And ye yourselves shall drive out the evil man from you.

< 1 Wakorintho 5 >