< 1 Wakorintho 16 >

1 Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
Now concerning the offering for the saints, you also are to do as I directed the church of Galatia.
2 Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
On the first day of each week let each of you put aside something, keeping it in store as he may prosper, so that when I come there may be no collections going on.
3 Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
On my arrival I will send those whom you may accredit by letter to carry your bounty to Jerusalem.
4 Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
And if it is worth while for me to go too, they will accompany me.
5 Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia—maana nataraji kupitia Makedonia.
Now I shall come to you after I have gone through Macedonia.
6 Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
I shall remain some time with you; possibly spending the winter, in order that you may help me forward in whatever journey I take.
7 Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
For I do not wish at this present time to see you merely in passing; but if the Lord permits, I hope to remain some time with you.
8 Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
I am staying for the present in Ephesus, until Pentecost;
9 Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
for a door has opened to me, great and effectual, and the opponents are many.
10 Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
If Timothy come, see to it that he is among you without trepidation; for he is doing the Lord’s work, as I am, so let no one disparage him.
11 Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
Whenever he comes to me, send him on his way in peace, for I am expecting him with the other brothers.
12 Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
As for our Apollos, I have many times urged him to go to you with the others, but he was always unwilling to go to you at this time. He will come, however, whenever he has a good opportunity.
13 Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
Be watchful, stand firm in the faith, be manly, be strong.
14 Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
Let all that you do be done in love.
15 Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
I beg you this, my brothers - you know the household of Stephanus, that they were the first-fruits of Achaia, and that they devoted themselves to the service of the saints -
16 muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
so I want you also to show deference to such, and to every fellow worker, and laborer.
17 Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
I am glad that Stephanus and Fortunatus and Achaicus have arrived, for they have made up for your absence.
18 Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
They refresh my spirit as they do yours. So cultivate the acquaintance of such men.
19 Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
The churches of Asia greet you. Aquila and Priscilla (Prisca), with the church that meets in their house, greet you heartily in the Lord.
20 Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
All the brothers send greetings. Greet one another with a holy kiss.
21 Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
The greeting of me, Paul, with my own hand.
22 Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA—BWANA, njoo!
If any one does not love the Lord, let him be accursed. Our Lord is coming.
23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
The grace of our Lord Jesus be with you.
24 Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.
My love be with you all in Christ Jesus.

< 1 Wakorintho 16 >