< 1 Wakorintho 16 >

1 Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
Now concerning the collection for the sanctified, as I arranged for the congregations of Galatia, so also do ye.
2 Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
Upon the first day of the week let each of you set something aside near himself, storing up whatever he may prosper, so that when I come no collections may be made then.
3 Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
And when I arrive, whomever ye may approve by letters, I will send these men to bring your gift to Jerusalem.
4 Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
And if it is fitting for me to go also, they will go with me.
5 Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia—maana nataraji kupitia Makedonia.
But I will come to you when I pass through Macedonia, for I do pass through Macedonia.
6 Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
And it may be that I will remain with you, or I will even spend winter, so that ye may set me on my way wherever I go.
7 Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
For I do not want to see you now in passing, but I hope to remain some time with you, if the Lord allows.
8 Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
But I will remain at Ephesus until Pentecost.
9 Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
For a great and effective door has opened to me, and yet there are many who are hostile.
10 Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
But if Timothy comes, see that he becomes without fear with you, for he works the work of the Lord, as I also.
11 Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
Let not any man therefore disparage him, but send him forth in peace, so that he may come to me, for I expect him with the brothers.
12 Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
And about Apollos the brother, I urged him much that he would come to you with the brothers, and it was not at all his will that he should come now, but he will come when he has opportunity.
13 Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
Watch ye, stand firm in the faith, act like men, be strong.
14 Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
Let all things of you be done in love.
15 Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
Now I beseech you, brothers (ye know the house of Stephanas, that it is the first fruit of Achaia, and that they committed themselves to service for the sanctified),
16 muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
that ye also be subject to such men, and to every man working together and laboring.
17 Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
And I rejoice at the coming of Stephanas and Fortunatus and Achaicus, because these men filled your lack.
18 Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
For they refreshed my spirit and yours. Therefore acknowledge ye such men.
19 Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
The congregations of Asia salute you. Aquila and Priscilla salute you much in the Lord, with the congregation associated with their house.
20 Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
All the brothers salute you. Salute each other by a holy kiss.
21 Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
The salutation of Paul by my hand.
22 Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA—BWANA, njoo!
If any man does not love the Lord Jesus Christ, let him be accursed. Maranatha.
23 Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
The grace of the Lord Jesus Christ is with you.
24 Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.
My love is with you all in Christ Jesus. Truly.

< 1 Wakorintho 16 >