< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
Käre bröder, jag vill icke dölja för eder, att våre fäder voro alle under skyn, alle gingo de genom hafvet;
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
Och alle vordo de under Mose döpte, i skynom, och i hafvet.
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
Och hafva alle enahanda andelig mat ätit;
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
Och alle enahanda andelig dryck druckit; ty de drucko af den andeliga klippan, som dem medföljde; hvilken klippa var Christus.
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
Men månge af dem voro icke Gudi behagelige; ty de vordo nederslagne i öknene.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
Men detta är oss skedt till exempel; att vi icke skole hafva begärelse till det ondt är, såsom de begärelse hade.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Varer icke heller afgudadyrkare, såsom somliga af dem, som skrifvet är: Folket satte sig ned att äta och dricka, och stodo upp till att leka.
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Låter oss icke heller drifva horeri, såsom somlige af dem besmittade sig med horeri; och föllo på en dag tre och tjugu tusend.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
Låter oss ock icke fresta Christum, såsom somlige af dem frestade honom; och vordo dräpne af ormar.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
Knorrer ock icke, såsom somlige af dem knorrade; och vordo dräpne af förderfvarenom.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Allt sådant verderfors dem till ett exempel; men det är oss skrifvet till en förvarning, på hvilka verldenes ände kommen är. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
Derföre, den som låter sig tycka han står, han se till, att han icke faller.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
Eder hafver ingen frestelse ännu påkommit, utan den mennisklig är; men Gud är trofast, som icke låter eder frestas öfver edra förmågo; utan gör med frestelsen en utgång, så att I kunnen dragat.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
Derföre, mine käreste, flyr ifrån afgudadyrkan.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
Jag talar såsom med förståndigom; betrakter I hvad jag säger:
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
Välsignelsens kalk, den vi välsigne, är icke han Christi blods delaktighet? Det brödet, som vi bryte, är icke det Christi lekamens delaktighet?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Ty det är ett bröd; så äre vi månge en lekamen, efter vi alle af eno bröde delaktige äre.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Ser på Israel efter köttet; de som äta offren, äro de icke delaktige af altaret?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
Hvad skall jag då säga: Är afguden något? Eller är det något, som afgudom offras? Nej.
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
Men det säger jag, att hvad Hedningarna offra, det offra de djeflom, och icke Gudi. Nu vill jag icke, att I skolen delaktige varda med djeflomen.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
I kunnen icke dricka Herrans kalk, och djeflarnas kalk. I kunnen icke delaktige vara af Herrans bord, och djeflarnas bord.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Eller vilje vi reta Herran? Månn vi vara starkare än han?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
Jag hafver magt till allt, men det kommer icke allt till förbättring.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Ingen söke sitt, utan annars bästa.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Allt det falt är i köttboden, det äter, och fråger intet derefter för samvetets skull;
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
Ty jorden är Herrans, och allt det derpå är.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
När nu en otrogen bjuder eder till gäst, och I viljen gå till honom, så äter allt det eder förelägges, och fråger intet derefter för samvetets skull.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
Men om då någor säger till eder: Detta är offradt afgudom, så äter icke, för hans skull som det underviste, och för samvetets skull; ty jorden är Herrans, och allt det derpå är.
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
Samvetet, säger jag; icke ditt, utan dens andras; ty hvarföre skulle jag låta döma mina frihet af ens annars samvet?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
Ty om jag äter deraf med tacksägelse, hvi skulle jag då lastad varda för det jag tackar före?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Hvad I nu äten eller dricken, eller hvad I gören, så gören allt Gudi till äro.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Varer sådane, att I ingen förargen, hvarken Juda, eller Grek, eller Guds församling;
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
Såsom ock jag i all ting är allom till vilja, icke sökandes min, utan mångs mans nytto, att de måga varda salige.

< 1 Wakorintho 10 >