< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
En effet je ne veux pas que vous ignoriez, frères, que nos pères étaient tous sous la nuée et que tous ils ont traversé la mer,
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
et que tous ils ont été baptisés en Moïse dans la nuée et dans la mer,
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
et que tous ils ont mangé le même aliment spirituel,
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
et que tous ils ont bu le même breuvage spirituel, car ils s'abreuvaient à un rocher spirituel qui les suivait, or ce rocher était Christ.
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
Toutefois ce ne fut pas au plus grand nombre d'entre eux que Dieu prit plaisir, car ils demeurèrent gisants dans le désert.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
Or toutes ces choses ont eu lieu pour nous servir d'exemples, afin que nous ne convoitions point de mauvaises choses, comme eux-mêmes l'ont fait.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Ne devenez pas non plus idolâtres, comme quelques-uns d'entre eux, selon qu'il est écrit: « Le peuple s'assit pour manger et boire, et ils se levèrent pour jouer. »
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Ne nous livrons pas non plus à l'impudicité, comme s'y livrèrent quelques-uns d'entre eux, et ils périrent en un seul jour au nombre de vingt-trois mille.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
Ne tentons pas non plus le Seigneur, comme le tentèrent quelques-uns d'entre eux, et ils étaient tués par les serpents.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
Ne murmurez pas non plus, comme murmurèrent quelques-uns d'entre eux, et ils furent tués par l'exterminateur.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Or ces choses leur arrivaient figurément, mais elles ont été écrites pour notre instruction, pour nous, auxquels a abouti la fin des siècles; (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
ainsi donc que celui qui s'imagine rester debout prenne garde qu'il ne tombe!
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
Vous n'avez pas été exposés à des tentations surhumaines, et, Dieu, qui est fidèle, ne permettra pas que vous soyez tentés au delà de vos forces; au contraire, avec la tentation Il vous donnera le moyen d'en sortir, afin que vous puissiez la supporter.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
C'est pourquoi, mes bien-aimés, fuyez l'idolâtrie.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
Je vous parle comme à des gens sensés; jugez vous-mêmes de ce que je dis:
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
La coupe de la bénédiction que nous bénissons, n'est-elle pas une participation au sang de Christ? Le pain que nous rompons, n'est-il pas une participation au corps de Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Car, comme il y a un seul pain, de même notre pluralité ne forme qu'un seul corps, car tous nous participons à ce seul pain.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Voyez l'Israël selon la chair: est-ce que ceux qui se nourrissent des sacrifices n'entrent pas en partage avec l'autel?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
Que dis-je donc? Que la viande sacrifiée aux idoles est quelque chose, ou bien qu'une idole est quelque chose? Non,
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
mais que ce qu'ils sacrifient, c'est à des démons, et non à Dieu, qu'ils le sacrifient; or je ne veux pas que vous entriez en partage avec les démons;
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
vous ne pouvez boire la coupe du seigneur et la coupe des démons; vous ne pouvez prendre part à la table du seigneur et à la table des démons.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Ou bien, voulons-nous provoquer le Seigneur? Est-ce que nous sommes plus forts que Lui?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
Tout est permis, mais tout ne convient pas; tout est permis, mais tout n'édifie pas.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Que personne ne recherche son propre intérêt, mais celui d'autrui.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Mangez de tout ce qui se vend au marché, sans vous enquérir de rien par motif de conscience,
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
car c'est au Seigneur qu'appartient la terre et tout ce qui la remplit.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
Si un incrédule vous invite et que vous vouliez y aller, mangez de tout ce qui est servi, sans vous enquérir de rien par motif de conscience;
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
mais si quelqu'un vous dit: « Ceci a été offert en sacrifice, » n'en mangez pas à cause de celui qui vous en a averti, et de la conscience,
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
non que ce soit de votre conscience que je parle, mais de celle de l'autre. En effet, pourquoi ma liberté serait-elle jugée par une conscience étrangère?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
Si moi-même je prends part au repas avec action de grâces, pourquoi serais-je calomnié à propos de ce dont je rends grâces?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Ainsi donc, soit que vous mangiez, soit que vous buviez, soit que vous fassiez quelque chose, faites tout pour la gloire de Dieu.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Ne soyez en scandale ni aux Juifs, ni aux Grecs, ni à l'église de Dieu,
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
comme moi-même je m'applique en toutes choses à plaire à tous, ne recherchant point mon avantage particulier, mais celui du plus grand nombre, afin qu'ils soient sauvés.

< 1 Wakorintho 10 >