< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
For I would have you remember, brethren, how our forefathers were all of them sheltered by the cloud, and all got safely through the Red Sea.
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
All were baptized in the cloud and in the sea to be followers of Moses.
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
All ate the same spiritual food,
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
and all drank the same spiritual drink; for they long drank the water that flowed from the spiritual rock that went with them--and that rock was the Christ.
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
But with most of them God was not well pleased; for they were laid low in the Desert.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
And in this they became a warning to us, to teach us not to be eager, as they were eager, in pursuit of what is evil.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
And you must not be worshippers of idols, as some of them were. For it is written, "The People sat down to eat and drink, and stood up to dance."
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Nor may we be fornicators, like some of them who committed fornication and on a single day 23,000 of them fell dead.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
And do not let us test the Lord too far, as some of them tested Him and were destroyed by the serpents.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
And do not be discontented, as some of them were, and they were destroyed by the Destroyer.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
All this kept happening to them with a figurative meaning; but it was put on record by way of admonition to us upon whom the ends of the Ages have come. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
So then let him who thinks he is standing securely beware of falling.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
No temptation has you in its power but such as is common to human nature; and God is faithful and will not allow you to be tempted beyond your strength. But, when the temptation comes, He will also provide the way of escape; so that you may be able to bear it.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
Therefore, my dear friends, avoid all connection with the worship of idols.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
I speak as to men of sense: judge for yourselves of what I say.
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of blessing, which we bless, does it not mean a joint-participation in the blood of Christ? The loaf of bread which we break, does it not mean a joint-participation in the body of Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Since there is one loaf, we who are many are one body; we, all of us, share in that one loaf.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Look at the Israelites--the nation and their ritual. Are not those who eat the sacrifices joint-partakers in the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
Do I mean that a thing sacrificed to an idol is what it claims to be, or that an idol is a real thing?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
No, but that which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons, not to God; and I would not have you have fellowship with one another through the demons.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
You cannot drink the Lord's cup and the cup of demons: you cannot be joint-partakers both in the table of the Lord and in the table of demons.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Or are we actually arousing the Lord to jealousy. Are we stronger than He is?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
Everything is allowable, but not everything is profitable. Everything is allowable, but everything does not build others up.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Let no one be for ever seeking his own good, but let each seek that of his fellow man.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Anything that is for sale in the meat market, eat, and ask no questions for conscience' sake;
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
for the earth is the Lord's, and all that it contains.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
If an unbeliever gives you an invitation and you are disposed to accept it, eat whatever is put before you, and ask no questions for conscience' sake.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
But if any one tells you, "This food has been offered in sacrifice;" abstain from eating it--out of respect for him who warned you, and, as before, for conscience' sake.
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
But now I mean his conscience, not your own. "Why, on what ground," you may object, "is the question of my liberty of action to be decided by a conscience not my own?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
If, so far as I am concerned, I partake with a grateful heart, why am I to be found fault with in regard to a thing for which I give thanks?"
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether, then, you are eating or drinking, or whatever you are doing, let everything be done to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Do not be causes of stumbling either to Jews or to Gentiles, nor to the Church of God.
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
That is the way that I also seek in everything the approval of all men, not aiming at my own profit, but at that of the many, in the hope that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >