< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
Moreover, brethren, I would not that ye should be ignorant, that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea;
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
And were all baptized to Moses in the cloud and in the sea;
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
And all ate the same spiritual food;
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
And all drank the same spiritual drink: (for they drank of that spiritual Rock that followed them: and that Rock was Christ.)
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
But with many of them God was not well pleased: for they were overthrown in the wilderness.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
Now these things were our examples, to the intent we should not lust after evil things, as they also lusted.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Neither be ye idolaters, as [were] some of them: as it is written, The people sat down to eat and drink, and rose up to play.
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Neither let us commit lewdness, as some of them committed, and fell in one day three and twenty thousand.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
Neither let us tempt Christ, as some of them also tempted, and were destroyed by serpents.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
Neither murmur ye, as some of them also murmured, and were destroyed by the destroyer.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Now all these things happened to them for examples: and they are written for our admonition, upon whom the ends of the world are come. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
Wherefore let him that thinketh he standeth, take heed lest he fall.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
There hath no temptation taken you but such as is common to man: but God [is] faithful, who will not suffer you to be tempted above what ye are able; but will with the temptation also make a way to escape, that ye may be able to bear [it].
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
Wherefore, my dearly beloved, flee from idolatry.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
I speak as to wise men; judge ye what I say.
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, is it not the communion of the blood of Christ? The bread which we break, is it not the communion of the body of Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
For we [being] many are one bread, [and] one body: for we are all partakers of that one bread.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Behold Israel after the flesh: are not they who eat of the sacrifices, partakers of the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
What then do I say? that the idol is any thing, or that which is offered in sacrifice to idols is any thing?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
But [I say], that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons, and not to God: and I would not that ye should have fellowship with demons.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
Ye cannot drink the cup of the Lord, and the cup of demons: ye cannot be partakers of the Lord's table, and of the table of demons.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Do we provoke the Lord to jealousy? are we stronger than he?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
All things are lawful for me, but all things are not expedient: all things are lawful for me, but all things edify not.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Let no man seek his own, but every man another's [wealth].
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Whatever is sold in the provision market, [that] eat, asking no question for conscience' sake:
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
For the earth [is] the Lord's, and its fullness.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
If any of them that believe not invites you [to a feast], and ye are disposed to go; whatever is set before you, eat, asking no question on account of conscience.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
But if any man shall say to you, This is offered in sacrifice to idols, eat not for his sake that showed it, and for conscience' sake: for the earth [is] the Lord's, and its fullness:
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
Conscience, I say, not thy own, but of the other: for why is my liberty judged by another [man's] conscience?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
For if I by grace am a partaker, why am I evil spoken of for that for which I give thanks?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether therefore ye eat or drink, or whatever ye do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Give no offense, neither to the Jews, nor to the Gentiles, nor to the church of God:
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
Even as I please all [men] in all [things], not seeking my own profit, but the [profit] of many, that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >