< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
For I wish not ye should be ignorant, brethren, that, all our fathers, were, under the cloud, and, all, passed through the sea, —
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
And, all, immersed themselves into Moses, in the cloud, and in the sea;
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
And, all, did eat [the same] spiritual food,
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
And, all, drank, the same spiritual drink, —for they continued to drink of the spiritual rock that followed them, and, the rock, was the Christ: —
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
Nevertheless, with the most of them, God, was not well-pleased, for they were strewed along in the desert.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
But, in these things, they became, ensamples for us, to the end we should not be covetous of evil things, even as, they, also coveted;
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Neither become ye, idolaters, as some of them, —as it is written—The people sat down to eat and drink, and rose up to be making sport;
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Neither let us commit fornication, as, some of them, committed fornication, and there fell, in one day, three and twenty thousand;
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
Neither let us be putting the Lord to the test, as, some of them, put him to the test, and, by the serpents, were perishing;
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
Neither be ye murmuring, even, as some of them, murmured, and perished by the destroyer.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
But, these things, by way of type, were happening unto them, and were written with a view to our admonition, unto whom, the ends of the ages, have reached along. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
So that, he that thinketh he is standing, let him take heed lest he fall.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
Trial, hath not taken you, save such as man can bear; faithful, moreover is God, who will not suffer you to be tried above what ye are able, but will make, with the trial, also the way of escape, that ye may be able to hold out.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
Wherefore, my beloved, flee from idolatry, —
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
As, to prudent men, I speak, —judge, ye, what I say: —
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, is it not, a sharing together of the blood of the Christ? The loaf which we break, is it not, a sharing together of the body of the Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Because, one loaf, one body, we, the many, are, for we, all, of the one loaf, partake.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Be looking at Israel after the flesh: —are not, they who eat the sacrifices, joint partakers with the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
What, then, am I saying?—that, an idol-sacrifice, is anything? or that, an idol, is anything?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
On the contrary—that, the things which the nations sacrifice, unto demons, and not unto God, they sacrifice; and I wish not that ye should become, sharers together with the demons!
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
Ye cannot be drinking—a cup of the Lord, and a cup of demons; ye cannot be partaking of, a table of the Lord, and a table of demons.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Or are we to provoke the Lord to jealousy? Are we mightier than he?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
All things are allowable—but, not all things, are profitable, —all things are allowable—but, not all things, upbuild.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Let, no one, be seeking, what concerneth himself, but that which concerneth some one else.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Whatsoever, in the market, is sold, eat, —asking no question, for conscience sake;
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
For, unto the Lord, belongeth the earth, and the fullness thereof.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
If one of them who believe not invite you, and ye are disposed to go, whatsoever is set before you, eat, —asking no question, for conscience sake.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
But, if anyone should say unto you, —This, is, a holy sacrifice, do not eat, for that man’s sake who disclosed it, and for conscience sake: —
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
But, conscience, I mean, not thine own, but the other’s, —for why is my freedom to be judged by another’s conscience?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
If, I, with gratitude, partake, why am I to be defamed, as to that for which, I, give thanks?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether, therefore, ye eat or drink, or whatsoever ye do, do, all things to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Give no occasion of stumbling—whether to Jews, or to Greeks, or to the assembly of God:
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
Even as, I also, in all things do please all, not seeking my own profit, but that of the many, that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >