< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
Moreover, brothers, I would not that you should be ignorant, how that all our fathers were under the cloud, and all passed through the sea;
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
And were all baptized to Moses in the cloud and in the sea;
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
And did all eat the same spiritual meat;
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
And did all drink the same spiritual drink: for they drank of that spiritual Rock that followed them: and that Rock was Christ.
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
But with many of them God was not well pleased: for they were overthrown in the wilderness.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
Now these things were our examples, to the intent we should not lust after evil things, as they also lusted.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Neither be you idolaters, as were some of them; as it is written, The people sat down to eat and drink, and rose up to play.
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Neither let us commit fornication, as some of them committed, and fell in one day three and twenty thousand.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
Neither let us tempt Christ, as some of them also tempted, and were destroyed of serpents.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
Neither murmur you, as some of them also murmured, and were destroyed of the destroyer.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Now all these things happened to them for ensamples: and they are written for our admonition, on whom the ends of the world are come. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
Why let him that thinks he stands take heed lest he fall.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
There has no temptation taken you but such as is common to man: but God is faithful, who will not suffer you to be tempted above that you are able; but will with the temptation also make a way to escape, that you may be able to bear it.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
Why, my dearly beloved, flee from idolatry.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
I speak as to wise men; judge you what I say.
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, is it not the communion of the blood of Christ? The bread which we break, is it not the communion of the body of Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
For we being many are one bread, and one body: for we are all partakers of that one bread.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Behold Israel after the flesh: are not they which eat of the sacrifices partakers of the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
What say I then? that the idol is any thing, or that which is offered in sacrifice to idols is any thing?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
But I say, that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to devils, and not to God: and I would not that you should have fellowship with devils.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
You cannot drink the cup of the Lord, and the cup of devils: you cannot be partakers of the Lord’s table, and of the table of devils.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Do we provoke the Lord to jealousy? are we stronger than he?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
All things are lawful for me, but all things are not expedient: all things are lawful for me, but all things edify not.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Let no man seek his own, but every man another’s wealth.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Whatever is sold in the shambles, that eat, asking no question for conscience sake:
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
For the earth is the Lord’s, and the fullness thereof.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
If any of them that believe not bid you to a feast, and you be disposed to go; whatever is set before you, eat, asking no question for conscience sake.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
But if any man say to you, This is offered in sacrifice to idols, eat not for his sake that showed it, and for conscience sake: for the earth is the Lord’s, and the fullness thereof:
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
Conscience, I say, not your own, but of the other: for why is my liberty judged of another man’s conscience?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
For if I by grace be a partaker, why am I evil spoken of for that for which I give thanks?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether therefore you eat, or drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Give none offense, neither to the Jews, nor to the Gentiles, nor to the church of God:
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
Even as I please all men in all things, not seeking my own profit, but the profit of many, that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >