< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
For it is my desire, my brothers, that you may keep in mind how all our fathers were under the cloud, and they all went through the sea;
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
And they all had baptism from Moses in the cloud and in the sea;
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
And they all took the same holy food;
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
And the same holy drink: for they all took of the water from the holy rock which came after them: and the rock was Christ.
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
But with most of them God was not pleased: for they came to their end in the waste land.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
Now these things were for an example to us, so that our hearts might not go after evil things, as they did.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Then do not go after false gods, as some of them did; as it is said in the holy Writings, After resting and feasting, the people got up to take their pleasure.
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Again, let us not give way to the desires of the flesh, as some of them did, of whom twenty-three thousand came to their end in one day.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
And let us not put the Lord to the test, as some of them did, and came to their death by snakes.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
And do not say evil things against the Lord, as some of them did, and destruction overtook them.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Now these things were done as an example; and were put down in writing for our teaching, on whom the last days have come. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
So let him who seems to himself to be safe go in fear of a fall.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
You have been put to no test but such as is common to man: and God is true, who will not let any test come on you which you are not able to undergo; but he will make with the test a way out of it, so that you may be able to go through it.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
For this cause, my dear brothers, give no worship to false gods.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
What I am saying is for wise men, do you be the judges of it.
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we take, does it not give us a part in the blood of Christ? and is not the broken bread a taking part in the body of Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Because we, being a number of persons, are one bread, we are one body: for we all take part in the one bread.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
See Israel after the flesh: do not those who take as food the offerings of the altar take a part in the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
Do I say, then, that what is offered to images is anything, or that the image is anything?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
What I say is that the things offered by the Gentiles are offered to evil spirits and not to God; and it is not my desire for you to have any part with evil spirits.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
It is not possible for you, at the same time, to take the cup of the Lord and the cup of evil spirits; you may not take part in the table of the Lord and the table of evil spirits.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Or may we be the cause of envy to the Lord? are we stronger than he?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
We are free to do all things, but there are things which it is not wise to do. We are free to do all things, but not all things are for the common good.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Let a man give attention not only to what is good for himself, but equally to his neighbour's good.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Whatever meat may be had at the public market, take as food without question of right or wrong;
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
For the earth is the Lord's and all things in it.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
If a Gentile makes a feast for you, and you are pleased to go as a guest, take whatever is put before you, without question of right or wrong.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
But if anyone says to you, This food has been used as an offering, do not take it, on account of him who said it, and on account of his sense of right and wrong:
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
Right and wrong, I say, not for you, but for the other man; for the fact that I am free is not dependent on another man's sense of right or wrong.
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
But if I give praise to God for the food which I take, let no man say evil of me for that reason.
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
So then, if it is a question of food or drink, or any other thing, whatever you do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Give no cause of trouble to Jews, or to Greeks, or to the church of God.
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
Even as I give way to all men in all things, not looking for profit for myself, but for the good of others, that they may get salvation.

< 1 Wakorintho 10 >