< 1 Wakorintho 10 >

1 Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
Now, brethren, I do not wish you to be ignorant, that all our fathers were under the cloud, and that all passed through the sea,
2 Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
and were all immersed into Moses, in the cloud and in the sea;
3 Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
and did all eat the same spiritual food,
4 wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
and did all drink the same spiritual drink: for they drank of that spiritual Rock that followed them, and that Rock was the Christ.
5 Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
But with the most of them God was not well pleased, for they were overthrown in the wilderness.
6 Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
Now these things took place as examples for us, that we should not desire evil things, as they, also, desired.
7 Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: “Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza.”
Neither be you idolaters, as some of them were, as it is written: Tho people sat down to eat and to drink, and rose up to engage in idolatrous sport.
8 Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Nor let us be guilty of lewdness, as some of them were guilty, and fell, in one day, twenty-three thousand.
9 Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
Nor let us tempt the Christ, as some of them also tempted, and were destroyed by serpents.
10 Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
Nor do you murmur, as some of them also murmured, and were destroyed by the destroyer.
11 Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili. (aiōn g165)
Now all these things happened to them as examples, and they are written for the instruction of us, upon whom the ends of the ages have come. (aiōn g165)
12 Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
Wherefore, let him that thinks he stands, take heed lest he foil.
13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
No trial has come upon you but such as is common to man: but God is faithful, who will not suffer you to be tried more than you are able to bear; but he will, with the trial, make a way to escape, so that you be able to bear up under it.
14 Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
Wherefore, my beloved, flee from idolatry.
15 Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
I speak as to wise men; judge you what I say.
16 Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
The cup of blessing which we bless, is it not the participation of the blood of the Christ? The bread which we break, is it not the participation of the body of the Christ?
17 Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
Because the loaf is one, we, the many, are one body, for we are all partakers of the one loaf.
18 Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
Look at Israel according to the flesh: are not those who eat the sacrifices partakers with the altar?
19 Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
What, then, do I say? That an idol is any thing? or, that what is sacrificed to an idol is any thing?
20 Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
But I say, that the things which the Gentiles sacrifice, they sacrifice to demons, and not to God. I do not wish you to be partakers with demons.
21 Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
You can not drink the cup of the Lord, and the cup of demons: you can not be partakers of the table of the Lord, and of the table of demons.
22 Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
Do we provoke the Lord to jealousy? Are we stronger than he?
23 Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
All meats are lawful for me; but all are not profitable; all are lawful, but all do not edify.
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
Let no one seek his own, but each the welfare of the other.
25 Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
Any thing that is sold in the market, eat, asking no questions on account of conscience:
26 maana Maandiko yasema: “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”
for the earth and its fullness are the Lord’s.
27 Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
If any one of the unbelievers invites you to a feast, and you are disposed to go, eat any thing that is set before you, asking no questions for conscience sake.
28 Lakini mtu akiwaambieni: “Chakula hiki kimetambikiwa sanamu,” basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
But if any one say to you: This is sacrificed to idols; eat not, for the sake of him that pointed it out, and for conscience sake:
29 Nasema, “kwa ajili ya dhamiri,” si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: “Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
conscience, I say, not your own, but that of the other. Why, then, is my liberty judged by the conscience of another?
30 Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?”
If I partake with thanksgiving, why am I evil spoken of on account of that for which I give thanks?
31 Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
Whether, therefore, you eat or drink, or whatever you do, do all to the glory of God.
32 Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
Give no occasion for stumbling, either to the Jews, or to the Greeks, or to the church of God;
33 Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
even as I please all men in all things, not seeking my own good, but that of the many, in order that they may be saved.

< 1 Wakorintho 10 >