< Sefania 1 >

1 Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana Hezekia, katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda. “
The word of Yahweh which came unto Zephaniah, son of Cushi, son of Gedaliah, son of Amariah, son of Hezekiah, —in the days of Josiah son of Amon, king of Judah.
2 Nitaangamiza kabisa kila kitu kutoka usoni mwa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
I will take clean away everything from off the face of the ground, Declareth Yahweh.
3 Nitamwangamiza mtu na mnyama; Nitawaangamiza ndege wa mbinguni na samaki wa baharini, uharibifu pamoja na waovu. Hivyo nitamfutilia mbali mtu kutoka uso wa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
I will take away man and beast, I will take away the bird of the heavens and the fishes of the sea, and the stumblingblocks, even them who are lawless, —and will cut off mankind, from off the face of the ground, Declareth Yahweh.
4 Nitafika kwa mkono wangu juu ya Yuda na wote wenyeji wa Yerusalemu. Nitafutilia mbali kila mabaki ya Baali kutoka sehemu hii na majina ya watu waabuduo sanamu miongoni mwa makuhani,
And I will stretch out my hand—over Judah, and over all the inhabitants of Jerusalem, —and will cut off out of this place, the name of Baal, the name of the priestlings, with the priests;
5 watu ambao juu ya nyumba huabudu miili ya mbinguni, na watu ambao huabudu na kuapa kwa Yahwe bali ambao pia huapa kwa mfalme wao.
And them who bow down upon the housetops to the host of the heavens, —and them who bow down—who swear to Yahweh, and swear by Milcom;
6 Nitawafutilia mbali pia wale ambao wamegeuka nyuma kutoka kumfuata Yahwe, wale ambao pia humtafuta Yahwe pasipo kuuliza ulinzi wake.
And them who turn away from following Yahweh, —and have neither sought Yahweh, nor enquired for him.
7 Uwe kimya mbele ya Bwana Yahwe! Kwa kuwa siku ya Yahwe ni karibu, Yahwe ameandaa dhabihu na amewatenga wageni wake.
Hush! at the presence of My Lord, Yahweh, —for, near, is the day of Yahweh, for Yahweh hath prepared his sacrifice, hath hallowed his guests.
8 “Itakuja katika siku ya dhabihu ya Bwana, hivyo nitawapiga wakuu na wana wa mfalme, na kila mmoja aliyevikwa mavazi ya kigeni.
And it shall come to pass, in the day of Yahweh’s sacrifice, that I will punish the rulers, and the sons of the king, —and all such as are clothed with foreign apparel;
9 Katika siku hiyo nitawapiga wote wale ambao huruka juu ya kizingiti, wale ambao hujaza nyumba ya bwana wao kwa vurugu na udanganyifu.
And I will punish every one who leapeth over the threshold, in that day, —those who fill the house of their lords with violence and deceit.
10 Itakuwa katika siku ile - hili ni tangazo la Yahwe - kwamba kilio cha huzuni kitakuja kutoka kwenye mlango wa samaki, ikipiga yowe kutoka Wilaya ya Pili, na sauti ya kishindo kikuu kutoka vilimani.
And there shall come to be, in that day, declareth Yahweh, The noise of an outcry from the fish-gate, and of a howling out of the new city, —and of a great crashing, from the hills.
11 Pigeni yowe, wenyeji wa Soko la Wilaya, kwa wote wafanyabiashara watakuwa wameharibiwa, wote wale ambao hupima fedha watakuwa wamefutiliwa mbali.
Howl, ye inhabitants of the lower city, —because destroyed are all the people of traffic, cut off are all they who were laden with silver.
12 Itakuwa katika siku ile nitaitafuta Yerusalemu kwa taa na kuwapiga wanaume ambao watakuwa wamekaa kwenye mvinyo wao na kusema mioyoni mwao, 'Yahwe hatafanya chochote, ama kizuri au kiovu.'.
And it shall come to pass, at that time, that I will search through Jerusalem, with lamps, —and will punish the men who are thickened upon their lees, who are saying in their heart, Yahweh, will not give blessing, neither will he bring calamity.
13 Mali zao zitakuja kuporwa, na nyumba zao zitakuwa zimetelekezwa kwa maangamizi! Watajenga nyumba lakini hawataishi humo, na kupanda mizabibu lakini hawatakunywa mvinyo wake.
Therefore shall their goods become a booty, and their houses, a desolation, —and they shall build houses, but not inhabit them, and plant vineyards, but not drink the wine thereof.
14 Siku kubwa ya Yahwe ni karibu, karibu na inaharakisha upesi! Sauti ya siku ya Yahwe itakuwa ya kilio cha uchungu wa kishujaa!
Near is the great day of Yahweh, near, and very speedy, —The noise of the day of Yahweh, a strong man—there!—bitterly crying out!
15 Siku hiyo itakuwa siku ya ghadabu, siku ya huzuni na uchungu, siku ya dhoruba na maangamizi, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene.
A day of indignation, —that day! day of danger and distress, day of rush, and of crash, day of obscurity, and deep gloom, day of cloud, and thick darkness;
16 Itakuwa siku ya parapanda na kengele dhidi ya ngome mijini na buruji ndefu.
day of horn, and war-shout, —against the fortified cities, and against the high towers.
17 Hivyo nitaleta dhiki juu ya wanadamu, kwa hiyo watatembea karibu kama wanaume vipofu tangu walipofanya dhambi dhidi ya Yahwe. Damu yao itamwagwa kama vumbi, na sehemu zao za ndani kama kinyesi.
And I will bring distress to mankind, and they shall walk like them who are blind, because, against Yahweh, have they sinned, —and their blood, shall be poured out, as dust, and their bowels like dung.
18 Wala fedha zao wala dhahabu zao hazitaweza kuwaokoa juu ya ghadhabu ya Yahwe. Ndani ya moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, hivyo ataleta ukamilifu, miwisho wa kutisha kwa wote wakaao duniani.”
Neither their silver nor yet their gold, shall be able to deliver them, in the day of the indignation of Yahweh, but, in the fire of his jealousy, shall the whole earth be consumed; For, a destruction, surely a terrible one, will he make, with all them who dwell in the earth.

< Sefania 1 >