< Zekaria 6 >

1 Kisha nikageuka na kuinua macho na nikaona vibandawazi vinne vya farasi vikija kutoka kati ya milima miwili; na milima hiyo ilikuwa imetengenezwa kwa shaba.
And I turned, and lifted up mine eyes, and looked, and, behold, four chariots coming out from between two mountains; and the mountains were brazen mountains.
2 Kibandawazi cha kwanza kilikuwa na farasi wekundu, kibandawazi cha pili kilikuwa na farasi weusi,
In the first chariot [were] red horses; and in the second chariot black horses;
3 kibandawazi cha tatu kilikuwa na farasi weupe, na kibandawazi cha nne kilikuwa na farasi wa kijivu.
and in the third chariot white horses; and in the fourth chariot piebald [and] ash-coloured horses.
4 Hivyo nikamwuliza malaika aliyesema nami, “Ni vitu gani hivi bwana wangu?”
And I answered and said to the angel that talked with me, What are these, my Lord?
5 Malaika akajibu na kuniambia, “Hizi ni pepo nne za mbinguni zisimamazo mbele ya Bwana wa dunia yote.
And the angel that talked with me answered and said, These are the four winds of heaven, [and] they are going forth to stand before the Lord of all the earth.
6 Lenye farasi weusi linakwenda nchi ya kaskazini; farasi weupe wanakwenda nchi ya magharibi; na farasi wa kijivu wanakwenda nchi ya kusini.”
[As for the chariot] in which were the black horses, they went out to the land of the north; and the white went out after them; and the piebald went out to the land of the south.
7 Farasi hawa wenye nguvu walitoka na wanatafuta kwenda na kuzunguka juu ya nchi, hivyo malaika akasema, “Nendeni na mzunguke juu ya nchi!” nao wakaenda juu ya dunia yote.
And the ash-coloured went out, and looked to go and compass the earth: and he said, Go, and compass the earth. And they compassed the earth.
8 Kisha akaniita na kuniambia, “Tazama wale wanaokwenda nchi ya kaskazini, wataituliza roho yangu juu nchi hiyo.”
And he cried out and spoke to me, saying, Behold, these go out to the land of the north, and they have quieted mine anger in the land of the north.
9 Hivyo neno la Yahwe likanijia kusema,
And the word of the Lord came to me, saying,
10 “Chukua sadaka kutoka kwa waliohamishwa - kutoka kwa Helidai, Tobiya na Yedaya - leo hii uende na kuipeleka katika nyumba ya Yosia mwana wa Zefania, aliyetoka Babeli.
Take the things of the captivity from the chief men, and from the useful men of it, and from them that have understood it; and you shall enter in that day into the house of Josias the son of Sophonias that came out of Babylon.
11 Kisha uchukue fedha na dhahabu, ufanye taji na uivike katika kichwa cha Yoshua mwana wa Yehosadaki kuhani mkuu.
And you shall take silver and gold, and make crowns, and you shall put [them] upon the head of Jesus the son of Josedec the high priest;
12 Ongea naye na useme, Yahwe wa majeshi asema hivi: Mtu huyu, jina lake Tawi! Naye atakuwa alipo na kisha atajenga hekalu la Yahwe!
and you shall say to him, Thus says the Lord Almighty; Behold the man whose name is The Branch; and he shall spring up from his stem, and build the house of the Lord.
13 Ndiye atakayejenga hekalu la Yahwe naye atauinua utukufu wake; kisha ataketi na kutawala katika kiti chake cha enzi. Atakuwa kuhani juu ya kiti cha enzi na ufahamu wa amani utakuwa kati ya vyote viwili.
And he shall receive power, and shall sit and rule upon his throne; and there shall be a priest on his right hand, and a peaceful counsel shall be between [them] both.
14 Taji itawekwa hekaluni mwa Yahwe kwa heshima ya Heldai, Tobiya na Yedaya na kama kumbukumbu ya ukarimu wa mwana wa Zefania.
And the crown shall be to them that wait patiently, and to the useful men of the captivity, and to them that have known it, and for the favour of the son of Sophonias, and for a psalm in the house of the Lord.
15 Ndipo waliombali watakapokuja na kulijenga hekalu la Yahwe, hivyo mtajua kuwa Yahwe wa majeshi amenituma kwenu; kwani ikiwa kweli mnaisikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu hili litatendeka!”
And they [that are] far from them shall come and build in the house of the Lord, and you shall know that the Lord Almighty has sent me to you: and [this] shall come to pass, if you will diligently listen to the voice of the Lord your God.

< Zekaria 6 >