< Zekaria 13 >

1 Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
In that dai an open welle schal be to the hous of Dauid, and to men dwellynge at Jerusalem, in to waischyng a wey of a synful man, and of womman defoulid in vnclene blood.
2 Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
And it schal be, in that dai, seith the Lord of oostis, Y schal distrie names of idols fro `the lond, and thei schulen no more be `thouyt on; and Y schal take awei fro erthe false profetis, and an vnclene spirit.
3 Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
And it schal be, whanne ony man schal profesie ouer, his fadir and modir that gendriden hym, schulen seie to hym, Thou schalt not lyue, for thou hast spoke leesyng in the name of the Lord; and his fadir and his modir, gendreris of hym, schulen `togidere fitche hym, whanne he hath profesied.
4 Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
And it schal be, in that dai profetis schulen be confoundid, ech of his visioun, whanne he schal profesie; nether thei schulen be hilid with mentil of sak, that thei lie;
5 Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
but `thei schulen seie, Y am not a profete; Y am a man `erthe tiliere, for Adam is myn ensaumple fro my yongthe.
6 Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
And it schal be seid to hym, What ben these woundis in the myddil of thin hondis? And he schal seie, With these Y was woundid in the hous of hem that louyden me.
7 Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
Swerd, be thou reisid on my scheepherde, and on a man cleuynge to me, seith the Lord of oostis; smyte thou the scheepherde, and scheep of the floc schulen be scaterid. And Y schal turne myn hond to the litle.
8 Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
And twei partis schulen be in ech lond, seith the Lord, and thei schulen be scaterid, and schulen faile, and the thridde part schal be left in it.
9 Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”
And Y schal lede the thridde part bi fier, and Y schal brenne hem, as siluer is brent, and Y schal preue hem, as gold is preuyd. He schal clepe to help my name, and Y schal graciously here him; and Y schal seie, Thou art my puple, and he schal seie, Thou art my Lord God.

< Zekaria 13 >