< Zekaria 13 >

1 Katika siku hiyo kijito kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wenyeji wa Yerusalemu, kwa ajili ya dhambi na uchafu wao.
In that day every place shall be opened to the house of David and to the inhabitants of Jerusalem for removal and for separation.
2 Katika siku hiyo - asema Yahwe wa majeshi - kwamba nitaondoa majina ya sanamu katika nchi ili kwamba yasikumbukwe tena. Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu
And it shall come to pass in that day, says the Lord of hosts, [that] I will utterly destroy the names of the idols from off the land, and there shall be no longer [any] remembrance of them: and I will cut off the false prophets and the evil spirit from the land.
3 Ikiwa mtu yeyote ataendelea kutoa unabii, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, 'Hautaishi, kwa kuwa umenena uongo kwa jina la Yahwe! Ndipo baba na mama waliomzaa watakapomchoma wakati akitabiri.
And it shall come to pass, if a man will yet prophesy, that his father and his mother which gave birth to him shall say to him, You shall not live; for you has spoken lies in the name of the Lord: and his father and his mother who gave him birth shall bind him as he is prophesying.
4 Katika siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake aelekeapo kutoa unabii. Manabii hawa hawatavaa tena vazi la singa, ili kuwadanganya watu.
And it shall come to pass in that day, [that] the prophets shall be ashamed every one of his vision when he prophesies; and they shall clothe themselves with a garment of hair, because they have lied.
5 Kwa maana kila mmoja atasema, 'Mimi siyo nabii! mimi ni mkulima, kwa maana ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu!
And [one] shall say, I am not a prophet, for I am a tiller of the ground, for a man brought me up [thus] from my youth.
6 Lakini mtu mwingine atamwambia, 'Majeraha haya kati ya mikono yako ni ya nini?' naye atajibu, nilijeruhiwa na waliokuwa katika nyumba ya rafiki zangu.”
And I will say to him, What are these wounds between your hands? and he shall say, [Those] with which I was wounded in my beloved house.
7 Upanga! inuka mwenyewe dhidi ya mchungaji wangu, mtu asimamaye karibu nami - hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi. Mpige mchungaji, na kondoo watatawanyika! Kwa maana nitageuza mkono wangu dhidi ya wadogo.
Awake, O sword, against my shepherds, and against the man [who is] my citizen, says the Lord Almighty: strike the shepherds, and draw out the sheep: and I will bring mine hand upon the little ones.
8 Kisha itakuwa kwamba katika nchi yote - hivi ndivyo asemavyo Yahwe - kwamba theluthi mbili yake itaondolewa! Watu hao wataangamia; theluthi moja tu ndiyo itakayosalia.
And it shall come to pass, [that] in all the land, says the Lord, two parts thereof shall be cut off and perish; but the third shall be left therein.
9 Nitaipitisha hiyo ya tatu motoni na kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo. Wataliitia jina langu nami nitawajibu na kusema, 'Hawa ni watu wangu!' nao watasema, Yahwe ndiye Mungu wangu!”
And I will bring the third [part] through the fire, and I will try them as silver is tried, and I will prove them as gold is proved: they shall call upon my name, and I will hear them, and say, This is my people: and they shall say, The Lord [is] my God.

< Zekaria 13 >