< Zekaria 12 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
La respuesta de la Palabra de Yavé en lo relacionado con Israel: Yavé, Quien extiende el cielo, pone el cimiento de la tierra y forma el espíritu del hombre dentro de él, dice:
2 “Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
Ciertamente Yo convierto a Jerusalén en copa que hará temblar a todos los pueblos de alrededor. Cuando esté sitiada Jerusalén, también estará contra Judá.
3 Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
Aquel día Yo pondré a Jerusalén como piedra pesada a todos los pueblos. Todos los que se la carguen serán despedazados. Y todas las naciones de la tierra se juntarán contra ella.
4 Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
Aquel día, dice Yavé, golpearé con pánico todo caballo y a todo jinete con locura. Pero abriré mis ojos con favor sobre la Casa de Judá y heriré con ceguera todo caballo de las naciones oponentes.
5 Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
Entonces los jefes de Judá dirán en su corazón: Los habitantes de Jerusalén son un fuerte apoyo para nosotros por medio de Yavé de las huestes, su ʼElohim.
6 Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
Aquel día pondré a los jefes de Judá como brasero encendido entre la leña y como antorcha de fuego entre los conjuntos de espigas, pues devorarán a derecha y a izquierda a todos los pueblos vecinos. Los de Jerusalén vivirán otra vez con seguridad en Jerusalén, su lugar.
7 Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
Pero Yavé salvará primero las tiendas de Judá para que la altivez de la casa de David y de los habitantes de Jerusalén no se exalte sobre Judá.
8 Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
Aquel día Yavé defenderá al habitante de Jerusalén. El que de ellos sea débil será como David, y la casa de David será como ʼElohim, como el Ángel de Yavé delante de ellos.
9 “Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
Aquel día me propondré destruir a todas las naciones que lleguen contra Jerusalén.
10 Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
Derramaré Espíritu de gracia y de súplica sobre la casa de David y sobre los habitantes de Jerusalén. Mirarán a Mí, a Quien traspasaron. Llorarán como se llora por Hijo Unigénito, y se afligirán por Él como el que se aflige por el primogénito.
11 Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
Aquel día habrá gran llanto en Jerusalén, como el llanto de Hadad-rimón en la llanura de Meguido.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
La tierra lamentará, cada familia aparte. La familia de la casa de David por separado, y sus esposas aparte. La familia de la casa de Natán por separado, y sus esposas aparte.
13 Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
La familia de la casa de Leví por separado, y sus esposas aparte. La familia de Simei por separado, y sus esposas aparte.
14 Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.
Todas las otras familias, cada familia por separado, y sus esposas aparte.

< Zekaria 12 >