< Zekaria 12 >

1 Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
This is a declaration of Yahweh's word concerning Israel—a declaration of Yahweh, who stretched out the skies and laid the foundation of the earth, who fashions the spirit of mankind within man,
2 “Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
“See, I am about to make Jerusalem into a cup causing all the peoples surrounding her to stagger about. It will also be like that for Judah during the siege against Jerusalem.
3 Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
On that day, I will make Jerusalem a heavy stone for all the peoples. Anyone trying to lift that stone will hurt himself very much, and all the nations of the earth will gather against that city.
4 Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
On that day—this is Yahweh's declaration—I will strike every horse with confusion and its rider with madness. Over the house of Judah I will open my eyes, but every horse of the peoples I will strike with blindness.
5 Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
Then the leaders of Judah will say in their hearts, 'The inhabitants of Jerusalem are our strength because of Yahweh of hosts, their God.'
6 Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
On that day I will make the leaders of Judah like firepots among wood and like a flaming torch among standing grain, for they will consume all the surrounding peoples on their right and on their left. Jerusalem will again live in her own place.”
7 Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
Yahweh will save the tents of Judah first, so that the honor of the house of David and the honor of those who live in Jerusalem may not be greater than the rest of Judah.
8 Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
On that day Yahweh will be the defender of the inhabitants of Jerusalem, and on that day those who are weak among them will be like David, while the house of David will be like God, like the angel of Yahweh in front of them.
9 “Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
“On that day that I will begin to destroy all the nations that come against Jerusalem.
10 Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
But I will pour out a spirit of compassion and pleading on the house of David and the inhabitants of Jerusalem, so they will look on me, the one they have pierced. They will mourn for me, as one mourns for an only son; they will bitterly lament for him like those who lament the death of a firstborn son.
11 Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
On that day the laments in Jerusalem will be like the laments at Hadad Rimmon in the plain of Megiddo.
12 Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
The land will mourn, each clan separate from other clans. The clan of the house of David will be separate and their wives will be separate from the men. The clan of the house of Nathan will be separate and their wives will be separate from the men.
13 Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
The clan of the house of Levi will be separate and their wives will be separate from the men. The clan of the Shimeites will be separate and their wives will be separate from the men.
14 Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.
Every clan of the remaining clans—each clan will be separate and the wives will be separate from the men.”

< Zekaria 12 >