< Zekaria 10 >

1 Mwombeni Yahwe mvua nyakati za kipupwe - Yahwe afanyaye mvua ya radi - naye hufanya mvua inyeshe kwa kila mmoja na uoto kondeni.
Lūdziet lietu no Tā Kunga vēlajā lietus laikā! Tas Kungs rada zibeņus; Viņš tiem dos lietus papilnam ikkatrai zālei laukā.
2 Kwani sanamu za wenye nyumba husema uongo; waganga hunena uongo; wanasema ndoto za udanganyifu na hutoa faraja tupu, hivyo wapotea kama kondoo na wanaumia kwa sababu hakuna mchungaji.
Jo dievekļi runā nelietību, un zīlnieki rauga viltību un runā melu sapņus un iepriecina ar niekiem. Tādēļ tie maldās kā avis, tie ir nospaidīti, jo tur nav gana.
3 Gadhabu yangu inawaka dhidi ya wachungaji; ni mabeberu - viongozi - nitakao waadhibu. Yahwe wa majeshi atalihudumia pia kundi la kondoo wake, nyumba ya Yuda, na kuwafanya kama farasi wake wa vita!
Pret tiem ganiem Mana bardzība iedegusies, un tos āžus Es piemeklēšu. Jo Tas Kungs Cebaot piemeklē Savu ganāmo pulku, Jūda namu, un to ieceļ Sev par goda zirgu karā.
4 Kutoka kwao litatoka jiwe kuu la pembeni; kutoka kwao kitatoka kigingi cha hema; kutoka kwao utatoka upinde wa vita; kutoka kwao watakuja viongozi wote kwa pamoja.
No viņa iznāks stūra akmens, nagla, kara stops un visi valdnieki līdz.
5 Watakuwa kama mashujaa wawakanyagao adui zao katika matope ya mitaani vitani; watafanya vita, kwa maana Yahwe yu pamoja nao, nao watawaabisha wapanda farasi wa vita.
Un tie būs kā varoņi, kas kaušanā samin ielas dubļus, un tie kausies, jo Tas Kungs būs ar viņiem, un tie liks kaunā zirgu jājējus.
6 Nitaitia nguvu nyumba ya Yuda na kuiokoa nyumba ya Yusufu; kwani nitawarejesha na kuwahurumia. Watakuwa kama nilikuwa sijawaondoa, kwani mimi ni Yahwe Mungu wao, nami nitawaitikia.
Un Es stiprināšu Jūda namu un atpestīšu Jāzepa namu, un Es tos atkal iestādīšu, jo Es par tiem esmu apžēlojies, un tie būs, tā kā Es tos nebūtu atmetis, jo Es esmu Tas Kungs, viņu Dievs, un tos paklausīšu.
7 Ndipo Efraimu atakapokuwa kama shujaa, na mioyo yao itafurahi kama kwa mvinyo; wana wao wataona na kufurahi. Mioyo yao itanifurahia!
Un Efraīms būs kā varonis un viņa sirds priecāsies kā no vīna. Un viņa bērni to redzēdami līksmosies, viņu sirds priecāsies iekš Tā Kunga.
8 Nitawanong'oneza na kuwakusanya, kwani nitawaokoa, nao watakuwa wakuu kama walivyokuwa mwanzo!
Un Es tos ataicināšu un sapulcēšu, jo Es tos gribu izpestīt, un tie vairosies, kā tie citkārt vairojās.
9 Niliwapanda kati ya watu, lakini watanikumbuka katika nchi ya mbali, hivyo wao na wana wao wataishi na kurejea.
Un Es tos sēšu starp tautām, un tie Mani pieminēs tālās zemēs, un tie dzīvos ar saviem bērniem un atgriezīsies.
10 Kwa maana nitawarejesha kutoka nchi ya Misri na kuwakusanya kutoka Ashuru. Nitawaleta katika nchi ya Gileadi na Lebanoni mpaka kutakapokuwa hakuna nafasi tena kwa ajili yao.
Un Es tos atvedīšu no Ēģiptes zemes un tos sapulcināšu no Asīrijas un tos vedīšu uz Gileāda zemi un Tībanu, ka viņam nepietiks vietas.
11 Nitapita katika bahari ya mateso yao; nitayapiga mawimbi ya bahari hiyo na nitavikausha vilindi vyote vya Nile. Utukufu wa Ashuru utashushwa chini, na fimbo ya Misri itakwenda mbali kutoka kwa Wamisri.
Un viņš iet caur bēdu jūru un sit viļņus jūrā, un visi upes dziļumi izsīks; tad Asura lepnība taps nogāzta, un Ēģiptes scepteris zudīs.
12 Nitawatia nguvu katika mimi mwenyewe, nao watatembea katika jina langu - asema Yahwe.
Un Es tos stiprināšu iekš Tā Kunga, un tie staigās Viņa vārdā, saka Tas Kungs.

< Zekaria 10 >