< Ruth 4 >

1 Ndipo Boazi akaenda kwenye lango la Bethelehemu na kukaa chini. Muda mfupi tu akaja ndugu wa karibu ambaye Boazi alimuongelea. Boazi akamwambia, “Rafiki yangu, njoo hapa na uketi. Kisha mtu huyo akaja na kuketi.
And Boaz hath gone up to the gate, and sitteth there, and lo, the redeemer is passing by of whom Boaz had spoken, and he saith, 'Turn aside, sit down here, such a one, such a one;' and he turneth aside and sitteth down.
2 Ndipo Boazi akakusanya viongozi kumi wa mji na kusema, “Katini hapa.” Hivyo wakaketi.
And he taketh ten men of the elders of the city, and saith, 'Sit down here;' and they sit down.
3 Boazi alimwambia yule jamaa wa karibu, “Naomi aliyerudi kutoka mji wa Moabu, anauza sehemu ya aridhi ambayo ilikuwa ni miliki ya kaka yetu Elimeleki.
And he saith to the redeemer, 'A portion of the field which [is] to our brother, to Elimelech, hath Naomi sold, who hath come back from the fields of Moab;
4 Nilifikiria kukujulisha na kukwambia, 'Inunue mbele ya hawa waliokaa hapa, na mbele ya viongozi wa watu wangu.' Ikiwa utapenda kuikomboa, ikomboe. Lakini ikiwa hauhitaji kuikomboa, uniambie, ili nijue, kwa kuwa hakuna mwingine wa kuikomboa isipokuwa wewe, na mimi ni mdogo wako.” Ndipo huyo mtu mwingine akasema, “Nitalikomboa.”
and I said, I uncover thine ear, saying, Buy before the inhabitants, and before the elders of my people; if thou dost redeem — redeem, and if none doth redeem — declare to me, and I know, for there is none save thee to redeem, and I after thee.' And he saith, I redeem [it].'
5 Kisha Boazi akasema, “Ile siku utakayonunua shamba kutoka mkononi mwa Naomi, yakupasa pia kumchukua Ruth Mmoabu, mjane wa mtoto wa Elimeleki, ili kuliinua jina la marehemu kama urithi wake.”
And Boaz saith, 'In the day of thy buying the field from the hand of Naomi, then from Ruth the Moabitess, wife of the dead, thou hast bought [it], to raise up the name of the dead over his inheritance.'
6 Ndipo yule jamaa wa karibu akasema, “Mimi siwezi kuikomboa ardhi kwa ajili yangu bila kuleta athari kwenye urithi wangu binafsi. Nakupa wewe haki ya kuikomboa kwa ajili yako mwenyewe, kwa kuwa mimi sitoweza.”
And the redeemer saith, 'I am not able to redeem [it] for myself, lest I destroy mine inheritance; redeem for thyself — thou — my right of redemption, for I am not able to redeem.'
7 Hii ilikuwa ni desturi ya zamani ya Israeli kuhusu ukombozi na kubadilishana mazuri. Kudhibitisha mambo haya yote, mtu huyu alivua kiatu chake na kumpatia jirani yake; hii ilikuwa ni namna ya kufanya makubaliano ya kisheria katika Israeli.
And this [is] formerly in Israel for redemption and for changing, to establish anything: a man hath drawn off his sandal, and given [it] to his neighbour, and this [is] the testimony in Israel.
8 Kwa hiyo huyu jamaa wa karibu akamwambia Boazi, “Inunue mwenyewe.” Kisha akavua kiatu chake.
And the redeemer saith to Boaz, 'Buy [it] for thyself,' and draweth off his sandal.
9 Ndipo Boazi akawaambia viongozi na watu wote, “Ninyi ni mashaidi kuwa nimenunua kila kilichokuwa cha Elimeleki na kila kilichokuwa na Kileoni na Mahilon kutoka kwenye mikono ya Naomi.
And Boaz saith to the elders, and [to] all the people, 'Witnesses [are] ye to-day that I have bought all that [is] to Elimelech, and all that [is] to Chilion and Mahlon, from the hand of Naomi;
10 Zaidi ya hayo kumhusu Ruth Mmoabu, mke wa Mahlon: nimempa kibali cha kuwa mke wangu, ili kuendeleza jina na urithi wa marehumu, ili kwamba jina lake lisipotee kati ya ndugu zake na lango la watu wake. Ninyi ni mashahidi leo.”
and also Ruth the Moabitess, wife of Mahlon, I have bought to myself for a wife, to raise up the name of the dead over his inheritance; and the name of the dead is not cut off from among his brethren, and from the gate of his place; witnesses ye [are] to-day.'
11 Watu wote na viongozi waliokuwa katika lango, walisema, “Tu mashahidi. Yahweh amfanye mwanamke huyu ambaye amekuja nyumbani kwako kama Raheli na Leya, ambao wawili hawa wameijenga nyumba ya Israeli. Na ubarikiwe katika Efrata na kuwa mashuhuri katika Bethelehem.
And all the people who [are] in the gate say — also the elders — 'Witnesses! Jehovah make the woman who is coming in unto thy house as Rachel and as Leah, both of whom built the house of Israel; and do thou virtuously in Ephrathah, and proclaim the Name in Beth-Lehem;
12 Na nyumba yako kama nyumba ya Peres, ambaye Tamari alimzalia yuda, kupitia uzao ambao Yahweh atakupatia pamoja na msichana huyu.”
and let thy house be as the house of Pharez (whom Tamar bare to Judah), of the seed which Jehovah doth give to thee of this young woman.'
13 Hivyo Boazi alimchukua Ruth, na akawa mke wake. Boazi alilala naye, na Yahweh alimruhusu kupata mimba, na alizaa mtoto wa kiume.
And Boaz taketh Ruth, and she becometh his wife, and he goeth in unto her, and Jehovah giveth to her conception, and she beareth a son.
14 Wanamke huyu akamwambia Naomi, “Yahweh abarikiwe, ambaye hajakuacha bila ndugu wa karibu, yaani mtoto huyu. Jina lake na liwe maarufu katika Israeli.
And the women say unto Naomi, 'Blessed [is] Jehovah who hath not let a redeemer cease to thee to-day, and his name is proclaimed in Israel,
15 Na awe kwako mrutubishaji wa maisha na mwenye ruzuku uzeeni mwako, kwa kuwa mtoto wako mkwe, ambaye anakupenda, ambaye ni bora kwako kuliko watoto wa kiume saba, amemzaa.
and he hath been to thee for a restorer of life, and for a nourisher of thine old age, for thy daughter-in-law who hath loved thee — who is better to thee than seven sons — hath borne him.'
16 Kisha naomi akamchukua mtoto, akamlaza kifuani pake, na kumhudumia.
And Naomi taketh the lad, and layeth him in her bosom, and is to him for a nurse;
17 Na majirani wa yule mwanamke, wakampa jina, wakisema, “Mtoto amezaliwa kwa Naomi.” Wakawita Obedi. Ambaye alikuja kuwa baba yake na Jese, ambaye alikuja kuwa baba yake na Daudi.
and the neighbouring women give to him a name, saying, 'There hath been a son born to Naomi,' and they call his name Obed; he [is] father of Jesse, father of David.
18 Hiki kilikuwa ni kizazi cha Peresi: Peres alimzaa Hezroni,
And these are genealogies of Pharez: Pharez begat Hezron,
19 Hezroni akamzaa Ram, Ram akamzaa Aminadabu,
and Hezron begat Ram, and Ram begat Amminidab,
20 Aminadabu akamzaa Nashon, Nashon akamzaa Salmon,
and Amminidab begat Nahshon, and Nahshon begat Salmon,
21 Salmon akamzaa Boazi, Boazi akamzaa Obed,
and Salmon begat Boaz, and Boaz begat Obed,
22 Obedi akamzaa Jese, na Jese akamzaa Daudi.
and Obed begat Jesse, and Jesse begat David.

< Ruth 4 >