< Ruth 3 >

1 Naomi, mama mkwe wake, alimwambia, “Mwanangu, hainilazimu kutafuta mahali pa wewe kupumzika, ili kwamba mambo yako yaende vizuri?
And she said to her Naomi mother-in-law her O daughter my ¿ not will I seek for you a resting place that it will go well for you.
2 Naye Boazi, mtu ambaye umekuwa pamoja na wasichana wake wa kazi, yeye si jamaa yetu? Tazama, jioni hii atakuwa akikung'uta shairi katika sakafu ya kupuria.
And therefore ¿ not [is] Boaz relative our whom you were with female servants his there! he [will be] winnowing [the] threshing floor of the barley this night.
3 Kwa hiyo, oga, jipake mafuta, uvae nguo zako nzuri, na ushuke kwenda kwenye sakafu ya kupuria. Lakini usijulikane kwa mtu huyu mpaka atakapo maliza kula na kunywa.
And you will wash - and you will anoint yourself and you will put (garments your *QK) on yourself (and you will go down *QK) the threshing floor may not you make yourself known to the man until finishes he to eat and to drink.
4 Na uhakikishe kuwa, atakapo lala chini, ukumbuke mahali alipo lala ili kwamba baadaye uende kwake, ufunue miguu yake, na ulale hapo. Kisha atakuambia cha kufanya.”
And let it be when lies down he and you will take note of the place where he will lie down there and you will go and you will uncover feet his (and you will lie down *Qk) and he he will tell to you [that] which you will do!
5 Ruth alimwambia Naomi, “Nitafanya kila kitu ulicho sema.”
And she said to her all that (you are saying to me *QK) I will do.
6 Alishuka kwenda kwenye sakafu ya kupuria, na alifuata maelekezo aliyopewa na mama mkwe wake.
And she went down the threshing floor and she did according to all that she had commanded her mother-in-law her.
7 Boazi alipomaliza kula na kunywa na moyo wake ulikuwa na furaha, alienda kulala chini mwisho wa sehemu ya kuhifadhia nafaka. Kisha Ruth akaenda taratibu, akaaifunua miguu ya Boazi, na kulala hapo chini.
And he ate Boaz and he drank and it was good heart his and he went to lie down at [the] end of the heap and she came in secrecy and she uncovered feet his and she lay down.
8 Panapo usiku wa manane Boazi alisituka. Akajigeuza, na hapo mwanamke alikuwa amelala katika miguu yake!
And it was in [the] middle of the night and he trembled the man and he twisted and there! a woman [was] lying down feet his.
9 Akamwambia, “Wewe ni nani?” Akajibu, “Mimi ni Ruth, mtumishi wako wa kike. Nifunike shuka lako mimi mtumishi wako wa kike, kwa kuwa wewe ni jamaa wa karibu.”
And he said who? [are] you and she said I [am] Ruth maidservant your and you will spread out skirt your over maidservant your for [are] a kinsman-redeemer you.
10 Boazi akamwambia, “Mwanangu, Yahweh akubariki. Umeonyesha wema mwishoni kuliko mwazoni, kwa sababu hukwenda kwa wanaume vijana, awe tajiri au masikini.
And he said [be] blessed you by Yahweh O daughter my you have made good loyalty your latter more than former to not to go after the young men whether poor and or rich.
11 Na sasa, mwanangu, usiogope! Nitakufanyia yote unayosema, kwa sababu mji wa watu wangu wote wanajua kuwa wewe ni mwanamke unayestahili.
And therefore O daughter my may not you fear all that you are saying I will do for you for [is] knowing all [the] gate of people my that [are] a woman of ability you.
12 Nikweli kuwa mimi ni jamaa wa karibu; hata hivyo, kuna jamaa wa karibu kuliko mimi.
And therefore for truly that [am] a kinsman-redeemer I and also there [is] a kinsman-redeemer near more than I.
13 Baki hapa usiku huu, na asubuhi, ikiwa atafanya jukumu lake la jamaa wa karibu, vizuri, muache afanye jukumu lake la kindugu. lakini kama hata fanya jukumu la kindugu kwako, ndipo mimi nitafanya, kama Yahweh aishivyo. Lala mpaka asubuhi.”
Stay - this night and it will be in the morning if he will redeem you good let him redeem and if not he will be willing to redeem you and I will redeem you I [by] [the] life of Yahweh lie down until the morning.
14 Kwa hiyo Ruth alilala kwenye miguu ya Boazi hadi asubuhi. Lakini aliamka mapema kabla ya yeyote kuweza kumtambua mtu mwingine. Kwa kuwa alikwisha mwambia, “Isijulikane kuwa mwanamke alikuja kwenye sakafu ya kupuria.”
And she lay down (feet his *QK) until the morning and she arose (before *QK) he recognized anyone neighbor his and he said may not it be known that she came the woman the threshing floor.
15 Kisha Boazi akamwambia, lete mtandio wako na uushikilie.” Alipo fanya hivyo, alipima vipimo vikubwa sita vya shairi katika mtandio na kumtwisha Ruth. Kisha Boazi akaenda mjini.
And he said give the shawl which [is] on you and take hold on it and she took hold on it and he measured out six barley and he put [it] on her and he came the city.
16 Ruth aliporudi kwa mama mkwe wake, alisema, “Ulifanyaje, mwanangu?” Ndipo Ruth akamwambia mambo yote aliyotendewa na mtu huyo.
And she came to mother-in-law her and she said who? [are] you O daughter my and she told to her all that he had done for her the man.
17 Alimwambia, “Hivi vipimo sita vya shairi ni vile alivyonipa yeye, kwa kuwa alisema, 'Usiende mikono mitupu kwa mama mkwe wako.'”
And she said [the] six the barley these he gave to me for (he said to me *QK) may not you go empty to mother-in-law your.
18 Kisha Naomi akasema, “Baki hapa, mwanangu, mpaka utakapojua yatakavyo kuwa, kwa kuwa Boazi hata pumzika mpaka atakapolimaliza jambo hili leo.”
And she said sit down O daughter my until that you will know! how? will it fall out a matter for not he will be at peace the man that except he has finished the matter this day.

< Ruth 3 >