< Warumi 4 >

1 Tutasema nini tena kwamba Abrahamu, baba yetu kwa jinsi ya mwili, amepatikana?
И тъй, какво ще кажем, че нашияо отец Авраам, е намерил по плът?
2 Kwa maana ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki kwa matendo, angekuwa na sababu ya kujisifu, lakini si mbele za Mungu.
Защото ако Авраам се е оправдал от дела, има с какво да се хвали, само не пред Бога.
3 Kwani maandiko yanasemaje? “Abrahamu alimwamini Mungu, na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
Понеже какво казва писанието: "Авраам повярва в Бога, и това му се вмени за правда".
4 Sasa kwa mtu afanyaye kazi, malipo yake hayahesabiwi kuwa ni neema, bali kuwa ni deni.
А на този, който върши дела, наградата му се не счита като благодеяние, но като дълг;
5 Lakini kwa mtu asiyefanya kazi bali anamwamini yeye ambaye amhesabia haki asiyekuwa mtaua, imani yake mtu huyo imehesabiwa kuwa haki.
а на този, който не върши дела, а вярва в Онзи, Който оправдава нечестивия, неговата вяра му се вменява за правда.
6 Daudi pia hunena baraka juu ya mtu ambaye Mungu amhesabia haki pasipo matendo.
Както и Давид говори за блаженството на човека, комуто Бог вменява правда независимо от дела:
7 Alisema, “Wamebarikiwa wale ambao maovu yao yamesamehewa na ambao dhambi zao zimefunikwa.
"Блажени ония, чиито беззакония са простени Чиито грехове са покрити;
8 Amebarikiwa mtu yule ambaye Bwana hamhesabii dhambi.”
Блажен е оня човек, комуто Господ няма да вмени грях".
9 Basi je baraka hizi ni kwa wale waliotahiriwa tu, au pia kwa wale wasiotahiriwa? Kwa maana twasema, “kwa Abrahamu imani yake ilihesabiwa kuwa ni haki.”
Прочее, това блаженство само за обрязаните ли е, или за необрязаните? Понеже казваме: "На Авраама вярата се вмени за правда".
10 Hivyo ilihesabiwaje basi? Wakati Abrahamu alikuwa katika tohara, au kabla hajatahiriwa? Haikuwa katika kutahiriwa, bali katika kutotahiriwa.
то как му се вмени? Когато беше обрязан ли, или необрязан? Не когато беше обрязан, но необрязан.
11 Abrahamu alipokea alama ya kutahiriwa. Huu ulikuwa muhuri wa ile haki ya imani aliyokuwa nayo tayari kabla hajatahiriwa. Matokeo ya ishara hii ni kwamba alifanyika kuwa baba wa wote waaminio, hata kama wapo katika kutotahiriwa. Hii ina maana kwamba haki itahesabiwa kwao.
И той обрязването като знак и печат на правдата от вяра, която имаше, когато беше необрязан, за да бъде той отец на всички, които вярват, ако и необрязани, за да се вмени правдата на тях.
12 Hii pia ilimaanisha kuwa Abrahamu alifanyika baba wa tohara si tu kwa wale wanaotokana na tohara, bali pia wale wanaozifuata nyayo za baba yetu Abrahamu. Na hii ndiyo imani aliyokuwa nayo kwa wasiotahiriwa.
и отец на ония обрязани, които не само са обрязани, но и ходят в стъпките на оная вяра, която нашият отец Авраам е имал, когато бе необрязан,
13 Kwa maana haikuwa kwa sheria kwamba ahadi ilitolewa kwa Abrahamu na uzao wake, ahadi hii ya kwamba watakuwa warithi wa dunia. isipokuwa, ilikuwa kupitia haki ya imani.
Понеже обещанието към Авраама или към потомството му, че ще бъде наследник на света, не стана чрез закон, но чрез правдата от вяра.
14 Kwa maana kama wale wa sheria ndio warithi, imani imekuwa bure, na ahadi imebatilika.
Защото, ако са наследници тия, които се облягат на закона, то вярата, то вярата е празна, и обещанието осуетено;
15 Kwa sababu sheria huleta ghadhabu, lakini pale ambapo hakuna sheria, pia hakuna kutotii.
понеже законът докарва, не обещание, а гняв; но гдето няма закон, там няма нито престъпление.
16 Kwa sababu hii hili hutokea kwa imani, ili iwe kwa neema. Matokeo yake, ahadi ni dhahiri kwa uzao wote. Na wazawa hawa si tu wale wanaojua sheria, bali pia wale ambao ni wa imani ya Abrahamu. Kwa maana yeye ni baba yetu sisi sote,
Затова наследството е от вяра, за да бъде по благодат, така щото обещанието да е осигурено за цялото потомство, не само за това, което се обляга на закона, но и за онова, което е от вярата на Авраама, който е отец на всички ни,
17 kama ilivyoandikwa, “Nimekufanya wewe kuwa baba wa mataifa mengi.” Abrahamu alikuwa katika uwepo wa yule aliyemwamini, yaani, Mungu ambaye huwapa wafu uzima na kuyaita mambo ambayo hayapo ili yaweze kuwepo.
(както е писано: "Направих те отец на много народи"), пред Бога Когото повярва, Който съживява мъртвите, и повиква в действително съществуване онова, което не съществува.
18 Licha ya hali zote za nje, Abrahamu kwa ujasiri alimuamini Mungu kwa siku zijazo. Hivyo akawa baba wa mataifa mengi, kulingana na kile kilichonenwa,”... Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”
Авраам, надявайки се без да има причина за надежда, повярва, за да стане отец на много народи, според реченото: "Толкова ще бъде твоето потомство".
19 Yeye hakuwa dhaifu katika imani. Abrahamu alikiri kwamba mwili wake mwenyewe ulikwisha kufa - alikuwa na umri wa karibu miaka mia moja. Pia alikubaliana na hali ya kufa ya tumbo la Sara.
Без да ослабне във вяра, той вземаше предвид, че тялото му е вече замъртвяло, като бе на около сто години, вземаше предвид и мъртвостта на Сарината утроба,
20 Lakini kwa sababu ya ahadi ya Mungu, Abrahamu hakusita katika kutokuamini. Bali, alitiwa nguvu katika imani na alimsifu Mungu.
обаче, относно Божието обещание не се усъмни чрез неверие, но се закрепи във вяра, и даде Богу слава,
21 Alikuwa akijua hakika ya kuwa kile ambacho Mungu ameahidi, alikuwa pia na uwezo wa kukikamilisha.
уверен, че това, което е обещал Бог, Той е силен да го изпълни.
22 Kwa hiyo hii pia ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.
Затова му се вмени за правда.
23 Sasa haikuandikwa tu kwa faida yake, kwamba ilihesabiwa kwake.
Това пък, че му се вмени за правда, не се написа само за него,
24 Iliandikwa kwa ajili yetu pia, kwa waliowekewa kuhesabiwa, sisi ambao tunaamini katika yeye aliyemfufua Bwana wetu Yesu kutoka wafu.
но и за нас, на които ще се вменява за правда, като вярваме в Този, Който е възкресил от мъртвите Исус, нашия Господ,
25 Huyu ni yule ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu na kufufuliwa ili tupate kuhesabiwa haki.
Който биде предаден за прегрешенията ни, и биде възкресен за оправданието ни.

< Warumi 4 >