< Warumi 3 >

1 Kisha ni faida gani aliyo nayo Myahudi? Na faida ya tohara ni nini?
Quel est donc l’avantage du Juif, ou quel est le profit de la circoncision?
2 Ni vyema sana kwa kila njia. Awali ya yote, Wayahudi walikabidhiwa ufunuo kutoka kwa Mungu.
– Grand de toute manière, et d’abord en ce que les oracles de Dieu leur ont été confiés.
3 Lakini, itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa na imani? Je, kutokuamini kwao kutafanya uaminifu wa Mungu kuwa batili?
Quoi donc? Si quelques-uns n’ont pas cru, leur incrédulité annulera-t-elle la fidélité de Dieu?
4 La hasha. Badala yake, acha Mungu aonekane kuwa kweli, hata kama kila mtu ni mwongo. Kama ilivyokuwa imeandikwa, “Ya kwamba uweze kuonekana kuwa mwenye haki katika maneno yako, na uweze kushinda uingiapo katika hukumu.”
Qu’ainsi n’advienne! mais que Dieu soit vrai et tout homme menteur, selon ce qui est écrit: « En sorte que tu sois justifié dans tes paroles, et que tu aies gain de cause quand tu es jugé ».
5 Lakini ikiwa uovu wetu unaonesha haki ya Mungu, tuseme nini? Mungu si dhalimu atoapo ghadhabu yake, je yupo hivyo? Naongea kutokana na mantiki ya kibinadamu.
Mais si notre injustice constate la justice de Dieu, que dirons-nous? Dieu est-il injuste quand il donne cours à la colère? – Je parle selon l’homme.
6 La hasha! Ni jinsi gani basi Mungu atauhukumu ulimwengu?
– Qu’ainsi n’advienne! puisqu’[alors], comment Dieu jugera-t-il le monde?
7 Lakini ikiwa kweli ya Mungu kupitia uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado nahukumiwa kama mwenye dhambi?
Car si la vérité de Dieu dans mon mensonge a abondé pour sa gloire, pourquoi moi aussi suis-je encore jugé comme pécheur?
8 Kwa nini tusiseme, kama tulivyosingiziwa na kama wengine wanavyothibitisha kwamba tunasema, “Tufanye uovu, ili mema yaje”? Hukumu juu yao ni ya haki.
Et non, comme nous sommes calomnieusement accusés et que quelques-uns prétendent que nous disons: Faisons du mal, afin qu’arrive le bien? – desquels le jugement est juste.
9 Ni nini basi? Tunajitetea wenyewe? Hapana kabisa. Kwa kuwa sisi tayari tumewatuhumu Wayahudi na Wayunani wote pamoja, ya kuwa wapo chini ya dhambi.
Quoi donc? Sommes-nous plus excellents? Nullement. Car nous avons déjà accusé et Juifs et Grecs d’être tous sous [le] péché,
10 Hii ni kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwenye haki, hata mmoja.
selon qu’il est écrit: « Il n’y a point de juste, non pas même un seul;
11 Hakuna mtu ambaye anaelewa. Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu.
il n’y a personne qui ait de l’intelligence, il n’y a personne qui recherche Dieu;
12 Wote wamegeuka. Wao kwa pamoja wamekuwa hawana maana. Hakuna atendaye mema, la, hata mmoja.
ils se sont tous détournés, ils se sont tous ensemble rendus inutiles; il n’y en a aucun qui exerce la bonté, il n’y en a pas même un seul »;
13 Makoo yao ni kaburi lililo wazi. Ndimi zao zimedanganya. Sumu ya nyoka ipo chini ya midomo yao.
« c’est un sépulcre ouvert que leur gosier; ils ont frauduleusement usé de leurs langues »; « il y a du venin d’aspic sous leurs lèvres »;
14 Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
« et leur bouche est pleine de malédiction et d’amertume »;
15 Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
« leurs pieds sont rapides pour verser le sang;
16 Uharibifu na mateso yapo katika njia zao.
la destruction et la misère sont dans leurs voies,
17 Watu hawa hawajajua njia ya amani.
et ils n’ont point connu la voie de la paix »;
18 Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao.”
« il n’y a point de crainte de Dieu devant leurs yeux ».
19 Sasa tunajua kwamba chochote sheria isemacho, husema na wale walio chini ya sheria. Hii ni ili kwamba kila kinywa kifungwe, na hivyo kwamba ulimwengu wote uweze kuwajibika kwa Mungu.
Or nous savons que tout ce que la loi dit, elle le dit à ceux qui sont sous la loi, afin que toute bouche soit fermée, et que tout le monde soit coupable devant Dieu.
20 Hii ni kwa sababu hakuna mwili utakaohesabiwa haki kwa matendo ya sheria mbele za macho yake. Kwa kuwa kupitia Sheria huja ufahamu wa dhambi.
C’est pourquoi nulle chair ne sera justifiée devant lui par des œuvres de loi, car par [la] loi est la connaissance du péché.
21 Lakini sasa pasipo sheria, haki ya Mungu imejulikana. Ilishuhudiwa kwa sheria na Manabii,
Mais maintenant, sans loi, [la] justice de Dieu est manifestée, témoignage lui étant rendu par la loi et [par] les prophètes,
22 hiyo ni, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo kwa wale wote wanaoamini. Maana hakuna tofauti.
[la] justice, dis-je, de Dieu par [la] foi en Jésus Christ envers tous, et sur tous ceux qui croient; car il n’y a pas de différence,
23 Kwa kuwa wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
car tous ont péché et n’atteignent pas à la gloire de Dieu,
24 Wamehesabiwa haki bure kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu.
– étant justifiés gratuitement par sa grâce, par la rédemption qui est dans le christ Jésus,
25 Kwa maana Mungu alimtoa Kristo Yesu awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake. Alimtoa Kristo kama ushahidi wa haki yake, kwa sababu ya kuziachilia dhambi zilizopita
lequel Dieu a présenté pour propitiatoire, par la foi en son sang, afin de montrer sa justice à cause du support des péchés précédents dans la patience de Dieu,
26 katika uvumilivu wake. Haya yote yalitokea ili kuonesha haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kujithibitisha mwenyewe kuwa haki, na kuonesha kwamba humhesabia haki mtu yeyote kwa sababu ya imani katika Yesu.
afin de montrer, [dis-je], sa justice dans le temps présent, en sorte qu’il soit juste et justifiant celui qui est de la foi de Jésus.
27 Kuwapi basi kujisifu? Kumetengwa. Kwa misingi ipi? Misingi ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani.
Où donc est la vanterie? – Elle a été exclue. – Par quelle loi? – celle des œuvres? – Non, mais par la loi de la foi;
28 Hivyo tunahitimisha kwamba mtu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
car nous concluons que l’homme est justifié par [la] foi, sans œuvres de loi.
29 Au Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Je yeye si Mungu wa watu wa Mataifa pia? Ndiyo, wa mataifa pia.
[Dieu] est-il seulement le Dieu des Juifs? ne l’est-il pas aussi des nations? – Certes, aussi des nations;
30 Ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja, atawahesabia haki walio wa tohara kwa imani, na wasiotahiriwa kwa njia ya imani.
puisque c’est un seul Dieu qui justifiera la circoncision sur le principe de [la] foi et l’incirconcision par la foi.
31 Je sisi twaibatilisha sheria kwa imani? La hasha! Kinyume cha hayo, sisi twaithibitisha sheria.
Annulons-nous donc [la] loi par la foi? Qu’ainsi n’advienne! au contraire, nous établissons [la] loi.

< Warumi 3 >