< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
То й благаю вас, браттє, щедротами Божими, представляйте тїла ваші (яко) жертву живу, сьвяту, угодну Богові; (се) розумне служеннє ваше.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
І не приладжуйтесь до віку сього, а переображуйтесь обновленнєм ума вашого, щоб довідуватись, що воля Божа добра й угодна і звершена. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
Глаголю бо благодаттю, даною мені, кожному між вами, щоб не думав більш про себе, ніж треба думати, а думав тверезо, як Бог кожному уділив міру віри.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
Бо яко ж в одному тїлї маємо многі члени, усі ж члени мають не одно діло,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
так многі ми - одно тіло в Христї, по одно му ж, один другому члени.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Маючи ж дарування по даній нам благодаті неоднакі: чи то пророцтво і (то й пророкуймо) по мірі віри;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
чи то служеннє (пильнуймо) в служенню; чи то навчає хто - в ученню;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
чи то напоминає хто - в напоминанню; хто дає, (давай) у простоті; хто старшинує, (старшинуй) з пильностю; хто милосердує, (милосердуй) з радістю.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Любов (нехай буде) нелицемірна. Ненавидячи лихе, прихиляйтесь до доброго.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
Братньою любовю (бувайте) один до одного ніжні; честю один одного більшим робіть;
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
у роботі не лїниві; духом горючі, Господеві служачі;
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
в надії веселі; в горю терпіливі; в молитві непереставаючі,
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
у потребинах сьвятих - подїльчиві; до гостинності охочі.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Благословляйте тих, хто гонить вас; благословляйте, а не кленїть.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Радуйте ся з тими, хто радуєть ся, і плачте з тими, хто плаче.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Однаково один з одним думайте. Високо про себе не думайте, а до смиренних нахиляйтесь. Не бувайте мудрі самі в себе.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Нікому злом за зло не оддавайте. Дбайте про добре перед усїма людьми.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
Коли можна, скільки (се) од вас, з усїма людьми майте мир.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Не відомщайте за себе, любі, а давайте місце гнїву (Божому), писано бо: Менї відомщеннє, я віддам, глаголе Господь.
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Оце ж, коли голодує ворог твій, нагодуй його; коли жаждує, напій його; се бо роблячи, уголлє огняне згребеш на голову його.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Не давай ся подужати злу, а подужуй зло добром.

< Warumi 12 >