< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
Por isso vos exorto, irmãos, pela misericórdia de Deus, a apresentar vossos corpos um sacrifício vivo, santo, aceitável a Deus, que é o vosso serviço espiritual.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
Não se conformem com este mundo, mas sejam transformados pela renovação de sua mente, para que possam provar qual é a boa, agradável e perfeita vontade de Deus. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
Pois eu digo através da graça que me foi dada, a todos que estão entre vós, não para pensar em vós mais do que devíeis pensar; mas para pensar razoavelmente, pois Deus atribuiu a cada pessoa uma medida de fé.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
Pois mesmo tendo muitos membros em um só corpo, e todos os membros não têm a mesma função,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
então nós, que somos muitos, somos um só corpo em Cristo, e individualmente membros uns dos outros,
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
tendo dons diferentes de acordo com a graça que nos foi dada: se profecia, profetizemos de acordo com a proporção de nossa fé;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
ou serviço, demo-nos ao serviço; ou aquele que ensina, ao seu ensino;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
ou aquele que exorta, à sua exortação; aquele que dá, que o faça com generosidade; aquele que governa, com diligência; aquele que mostra misericórdia, com alegria.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Let o amor seja sem hipocrisia. Abominem o que é maligno. Apegar-se ao que é bom.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
No amor aos irmãos sejam ternamente afetuosos uns com os outros; na honra prefiram um ao outro,
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
não se atrasem na diligência, fervorosos no espírito, servindo ao Senhor,
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
regozijando-se na esperança, resistindo aos problemas, continuando com firmeza na oração,
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
contribuindo para as necessidades dos santos, e dada à hospitalidade.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Abençoe aqueles que o perseguem; abençoe, e não amaldiçoe.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Alegre-se com aqueles que se regozijam. Chorem com os que choram.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Sejam da mesma opinião uns para com os outros. Não se ponham a pensar em coisas altas, mas associem-se com os humildes. Não seja sábio em seus próprios conceitos.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Não pague a ninguém o mal pelo mal. Respeite o que é honroso à vista de todos os homens.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
Se for possível, tanto quanto depender de você, esteja em paz com todos os homens.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Não procure vingança, amados, mas dê lugar à ira de Deus. Pois está escrito: “A vingança me pertence; eu retribuirei, diz o Senhor”.
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Therefore “Se seu inimigo está com fome, alimente-o. Se ele estiver com sede, dê-lhe uma bebida; pois, ao fazer isso, você amontoará brasas de fogo sobre sua cabeça”.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Não se deixe vencer pelo mal, mas vença o mal com o bem.

< Warumi 12 >