< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
IO vi esorto adunque, fratelli, per le compassioni di Dio, che voi presentiate i vostri corpi, il vostro razional servigio, [in] ostia vivente, santa, accettevole a Dio.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
E non vi conformiate a questo secolo, anzi siate trasformati per la rinnovazion della vostra mente; acciocchè proviate qual [sia] la buona, accettevole, e perfetta volontà di Dio. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
Perciocchè io, per la grazia che mi è stata data, dico a ciascuno che è fra voi: che non abbia alcun sentimento sopra ciò che conviene avere; anzi senta a sobrietà, secondo che Iddio ha distribuita a ciascuno la misura della fede.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
Perciocchè, siccome in uno stesso corpo abbiam molte membra, e tutte le membra non hanno una medesima operazione,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
così [noi, che siam] molti, siamo un medesimo corpo in Cristo; e ciascun [di noi è] membro l'uno dell'altro.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Ora, avendo noi doni differenti, secondo la grazia che ci è stata data, se [abbiam] profezia, [profetizziamo] secondo la proporzion della fede;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
se ministerio, [attendiamo] al ministerio; parimente il dottore [attenda] all'insegnare;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
e colui che esorta, [attenda] all'esortare; colui che distribuisce, [faccialo] in semplicità; colui che presiede, con diligenza; colui che fa opere pietose, con allegrezza.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
LA carità [sia] senza simulazione; abborrite il male, ed attenetevi fermamente al bene.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
[Siate] inclinati ed avervi gli uni agli altri affezione per amor fraterno; prevenite gli uni gli altri nell'onore.
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
Non [siate] pigri nello zelo; [siate] ferventi nello Spirito, serventi al Signore;
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
allegri nella speranza, pazienti nell'afflizione, perseveranti nell'orazione;
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
comunicanti a' bisogni de' santi, procaccianti l'ospitalità.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Benedite quelli che vi perseguitano; benedite[li], e non [li] maledite.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Rallegratevi con quelli che sono allegri, piangete con quelli che piangono.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Abbiate fra voi un medesimo sentimento; non abbiate l'animo alle cose alte, ma accomodatevi alle basse; non siate savi secondo voi stessi.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Non rendete ad alcuno male per male; procurate cose oneste nel cospetto di tutti gli uomini.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
S' [egli è] possibile, e quanto [è] in voi, vivete in pace con tutti gli uomini.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Non fate le vostre vendette, cari [miei]; anzi date luogo all'ira [di Dio]; perciocchè egli è scritto: A me la vendetta, io renderò la retribuzione, dice il Signore.
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Se dunque il tuo nemico ha fame, dagli da mangiare; se ha sete, dagli da bere; perciocchè, facendo questo, tu raunerai de' carboni accesi sopra il suo capo.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Non esser vinto dal male, anzi vinci il male per il bene.

< Warumi 12 >