< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
Je vous invite donc, frères, par les compassions de Dieu, à offrir vos corps comme un sacrifice vivant, saint et agréable à Dieu; c'est là le culte que vous devez raisonnablement rendre.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
Et ne vous modelez pas sur le siècle présent, mais soyez transfigurés par le renouvellement de votre intelligence, afin d'apprécier ce qu'est la volonté de Dieu, qui est bonne, agréable, et parfaite. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
Car, par la grâce qui m'a été donnée, j'invite chacun de vous à ne point nourrir des sentiments qui dépassent ceux qu'il faut avoir, mais à être animé de sentiments convenables, proportionnés à la mesure de foi que Dieu a départie à chacun.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
En effet, de même que, dans un seul corps, nous avons plusieurs membres, mais que tous les membres n'ont pas la même fonction,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
de même nous sommes, quoique plusieurs, un seul corps en Christ, tandis que nous sommes, chacun pris à part, les membres les uns des autres.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Ayant ainsi des dons différents selon la grâce qui nous a été donnée, soit de prophétie, exerçons-le selon la proportion de la foi;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
soit de ministère, exerçons-le dans le ministère; soit qu'il s'agisse de celui qui enseigne, qu'il se livre à l'enseignement,
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
ou de celui qui exhorte, qu'il se livre à l'exhortation; que celui qui distribue le fasse avec simplicité; que celui qui préside le fasse avec zèle; que celui qui compatit le fasse avec aménité.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Que la charité soit sans hypocrisie. Ayez en haine le mal, attachez-vous fortement au bien.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
Quant à l'amour fraternel, soyez pleins d'affection les uns pour les autres; quant aux égards, devancez-vous réciproquement; quant au zèle, ne soyez pas indolents. Soyez bouillants d'esprit, asservis au Seigneur,
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
joyeux par l'espérance, fermes dans la tribulation,
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
persévérants dans la prière.
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
Prenez part aux besoins des saints, exercez l'hospitalité.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Bénissez les persécuteurs, bénissez et ne maudissez pas.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Réjouissez-vous avec ceux qui se réjouissent; pleurez avec ceux qui pleurent.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Ayez, les uns pour les autres, des sentiments semblables. Ne visez pas aux grandeurs, mais laissez-vous attirer par ce qui est humble. Ne vous complaisez pas dans vos propres pensées.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Ne rendez à personne mal pour mal; ayez à cœur ce qui est bon en présence de tous les hommes.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
S'il est possible, pour autant que cela dépend de vous, soyez en paix avec tous les hommes.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Ne vous vengez point vous-mêmes, bien-aimés, mais laissez agir la colère; car il est écrit: « A Moi la vengeance; c'est Moi qui rétribuerai, dit le Seigneur.
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Mais si ton ennemi a faim, donne-lui à manger; s'il a soif donne-lui à boire; car en agissant ainsi tu entasseras des charbons de feu sur sa tête. »
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Ne sois pas subjugué par le mal, mais subjugue le mal par le bien.

< Warumi 12 >