< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
I urge you therefore, brothers, by the mercies of God, to present your bodies as living sacrifices, holy and acceptable to God, your reasonable religious service.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
Do not be conformed to this age, but be transformed by the renewing of your mind, so that you may determine what is the good, acceptable, and perfect will of God. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
For by the grace given to me I tell everyone among you not to think more highly of himself than he ought to think, but to think sensibly, in accordance with the measure of faith that God has distributed to each one of you.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
For just as in one body we have many members, and all the members do not have the same function,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
so we, who are many, are one body in Christ, and individually members of one another.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
We have different gifts according to the grace given to us. If someone's gift is prophecy, he should prophesy in proportion to his faith;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
if it is service, he should serve; if it is teaching, he should teach;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
if it is exhortation, he should exhort; if it is giving, he should do so generously; if it is leadership, he should do so diligently; if it is showing mercy, he should do so cheerfully.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Love must be without hypocrisy. Abhor what is evil; cling to what is good.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
Be devoted to one another in brotherly love. Take the lead in honoring one another.
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
Do not lack diligence in zeal, but be fervent in spirit, serving the Lord.
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
Rejoice in hope, persevere in tribulation, and persist in prayer.
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
Contribute to the needs of the saints, and pursue hospitality.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Bless those who persecute you; bless, and do not curse.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Rejoice with those who rejoice, and weep with those who weep.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Be of the same mind toward one another. Do not be haughty, but associate with the lowly. Do not be wise in your own estimation.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Repay no one evil for evil, but have regard for what is right in the sight of all.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
If possible, as far as it depends on you, be at peace with everyone.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Do not avenge yourselves, beloved, but leave room for the wrath of God, for it is written, “Vengeance is mine; I will repay, says the Lord.”
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Therefore, “if yoʋr enemy is hungry, feed him; if he is thirsty, give him something to drink; for by doing so, yoʋ will heap coals of fire on his head.”
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Do not be overcome by evil, but overcome evil with good.

< Warumi 12 >