< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
I beseech you therefore, brethren, through the compassions of God, to present your bodies a living, holy sacrifice, unto God acceptable, —your rational divine service;
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
And be not configuring yourselves unto this age, but be transforming yourselves by the renewing of your mind, to the end ye may be proving what is the thing willed by God—the good and acceptable and perfect. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
For I say, through the favour which hath been given me, unto every one who is among you, —not to think of himself more highly than he ought to think, but so to think as to think soberly—as, unto each one, God hath dealt a measure of faith.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
For, just as in one body we have many members, yet, all the members, have not the same office,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
So, we, the many, are one body in Christ, yet, severally, members one of another.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Now, having gifts of favour, according to the favour given unto us, differing—whether prophesying, [let us use it] according to the proportion of our faith,
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
Or ministering, [use it] in our ministering, or he that teacheth, [let him use his gift] in his teaching,
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
Or he that exhorteth, in his exhorting, he that imparteth, [let it be] with liberality, he that taketh a lead, with diligence, he that sheweth mercy, with cheerfulness.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Your love, [be] without hypocrisy, —loathing that which is wicked, cleaving to that which is good;
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
In your brotherly love, unto one another, being tenderly affectioned, in honour, unto one another, giving preference;
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
In business, not slothful, in spirit, fervent, to the Lord, doing service,
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
In hope, rejoicing, in tribulation, enduring, in prayer, persevering,
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
With the needs of the saints, having fellowship, —hospitality, pursuing.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Bless them that persecute, bless, and do not curse.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Rejoice with them that rejoice, weep with them that weep:
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
The same thing, one to another regarding, —not the lofty things regarding, but, by the lowly, being led along. Be not getting presumptuous in your own opinion:
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Unto no one, evil for evil rendering: providing honourable things before all men:
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
If possible—so far as dependeth on you, with all men being at peace:
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Not avenging, yourselves, beloved, but give place unto their anger; for it is written—Mine, is avenging, I, will recompense; —saith the Lord;
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
But—if thine enemy hunger, be feeding him, if he thirst, be giving him drink; for, this doing, coals of fire, shalt thou heap upon his head.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Be not overcome by evil, but overcome evil with good.

< Warumi 12 >