< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
I beseech you therefore, brethren, by the mercies of God, to present your bodies a living sacrifice, holy, well-pleasing to God, which is your spiritual worship;
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
and be not conformed to the fashion of this world, but be transformed by the renewal of your mind, that ye may learn by experience what is the will of God, what is good, and well-pleasing, and perfect. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
For through the grace given to me I warn every one among you, not to think of himself more highly than he ought to think, but to think soberly, according to the measure of faith which God hath imparted to each.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
For as in one body we have many members, and the members have not all the same office,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
so we, though many, form one body in Christ, and each of us is a member of it in common with the rest.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Having then gifts which dither according to the grace which hath been bestowed upon us, if we have prophecy, let us prophesy according to the proportion of our faith;
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
or if service, let us attend to the service; he that teacheth, let him attend to teaching;
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
or he that exhorteth, to exhortation; he that giveth, let him do it with liberality; he that presideth over others, with diligence; he that doeth deeds of mercy, with cheerfulness.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Let your love be unfeigned. Abhor that which is evil, cleave to that which is good.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
In brotherly love, be affectionate to one another; in honor, give each other the preference.
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
Be not backward in zeal; be fervent in spirit; serving the Lord.
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
Rejoice in hope; be patient in affliction; persevere in prayer.
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
Relieve the wants of the holy; be given to hospitality.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Bless those who persecute you; bless, and curse not.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Rejoice with those who rejoice; weep with those who weep.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Be of one mind among yourselves. Set not your minds on high things, but content yourselves with what is humble. Be not wise in your own conceits.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Render to no one evil for evil; have regard to what is honorable in the sight of all men.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
If it be possible, as far as dependeth on you, be at peace with all men.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Dearly beloved, avenge not yourselves, but rather make room for wrath; for it is written, “Vengeance is mine; I will repay, saith the Lord.”
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Therefore, “if thy enemy hunger, feed him; if he thirst, give him drink. For in so doing thou wilt heap coals of fire on his head.”
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Be not overcome by evil, but overcome evil with good.

< Warumi 12 >