< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
I Beseech you therefore brethren, by the mercies of God, that yee giue vp your bodies a liuing sacrifice, holy, acceptable vnto God, which is your reasonable seruing of God.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
And fashion not your selues like vnto this worlde, but bee yee changed by the renewing of your minde, that ye may prooue what that good, and acceptable and perfect will of God is. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
For I say through the grace that is giuen vnto me, to euery one that is among you, that no man presume to vnderstande aboue that which is meete to vnderstand, but that he vnderstande according to sobrietie, as God hath dealt to euery man the measure of faith.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
For as wee haue many members in one body, and all members haue not one office,
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
So we being many are one body in Christ, and euery one, one anothers members.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Seeing then that we haue gifts that are diuers, according to the grace that is giuen vnto vs, whether we haue prophecie, let vs prophecie according to the portion of faith:
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
Or an office, let vs waite on the office: or he that teacheth, on teaching:
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
Or he that exhorteth, on exhortation: he that distributeth, let him doe it with simplicitie: he that ruleth, with diligence: he that sheweth mercie, with cheerefulnesse.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Let loue be without dissimulation. Abhorre that which is euill, and cleaue vnto that which is good.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
Be affectioned to loue one another with brotherly loue. In giuing honour, goe one before another,
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
Not slouthfull to do seruice: seruent in spirit seruing the Lord,
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
Reioycing in hope, pacient in tribulation, continuing in prayer,
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
Distributing vnto the necessities of the Saintes: giuing your selues to hospitalitie.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Blesse them which persecute you: blesse, I say, and curse not.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Reioyce with them that reioyce, and weepe with them that weepe.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Be of like affection one towardes another: be not hie minded: but make your selues equall to them of the lower sort: be not wise in your selues.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
Recompence to no man euill for euill: procure things honest in the sight of all men.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
If it bee possible, as much as in you is, haue peace with all men.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Dearely beloued, auenge not your selues, but giue place vnto wrath: for it is written, Vengeance is mine: I will repay, saith the Lord.
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Therefore, if thine enemie hunger, feede him: if he thirst, giue him drinke: for in so doing, thou shalt heape coales of fire on his head.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Bee not ouercome of euill, but ouercome euill with goodnesse.

< Warumi 12 >