< Warumi 11 >

1 Basi nasema, je, Mungu aliwakataa watu wake? Hata kidogo. Kwa kuwa mimi pia ni Mwiisraeli, wa ukoo wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
И тъй, казвам: Отхвърлил ли е Бог Своите люде? Да не бъде! Защото и аз съм израилтянин, от Авраамовото потомство, от Вениаминовото племе.
2 Mungu hakuwakataa watu wake, aliowajua tangu mwanzo. Je hamjui andiko linasema nini kuhusu Eliya, jinsi alivyomsihi Mungu juu ya Israeli?
Не е отхвърлил Бог людете Си, които е предузнал. Или не знаете що казва писанието за Илия? как вика към Бога против Израиля, казвайки:
3 “Bwana, wamewaua manabii wako, nao wamebomoa madhabahu zako. Mimi peke yangu nimesalia, nao wanatafuta uhai wangu.”
"Господи, избиха пророците Ти, разкопаха олтарите Ти, и аз останах сам; но и моя живот искат да отнемат".
4 Lakini jibu la Mungu lasema nini kwako? “Nimetunza kwa ajili yangu watu elfu saba ambao hawampigii magoti Baali.”
Но що му казва божественият отговор?
5 Hata hivyo, wakati huu wa sasa pia kuna walio salia kwa sababu ya uchaguzi wa neema.
Така и в сегашно време има остатък, избран по благодат
6 Lakini ikiwa ni kwa neema, si tena kwa matendo. Vinginevyo neema haitakuwa tena neema.
Но, ако е по благодат, не е вече от дела, иначе благодатта не е вече благодат [а ако е от делата, не е вече благодат, иначе делото не е вече дело].
7 Ni nini basi? Jambo ambalo Israeli alikuwa akitafuta, hakukipata, bali wateule walikipata, na wengine walitiwa uzito.
Тогава какво? Онова, което Израил търсеше, това не получи, но избраните го получиха, а останалите се закоравиха даже до днес:
8 Ni kama ilivyoandikwa: “Mungu amewapa roho ya ubutu, macho ili wasione, na masikio ili wasisikie, mpaka leo hii.”
както е писано: "Бог им даде дух на безчуствие, очи
9 Naye Daudi anasema, “Acha meza zao na ziwe wavu, mtego, sehemu ya kujikwaa, na kulipiza kisasi dhidi yao.
И Давид казва:
10 Acha macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona. Ukawainamishe migongo yao daima.”
Да се помрачат очите им, та да не виждат, И сгърби гърба им за винаги".
11 Basi nasema, “Je, wamejikwaa hata kuanguka?” Isiwe hivyo kamwe. Badala yake, kwa kushindwa kwao, wokovu umefika kwa Mataifa, ili wao wenyewe watiwe wivu.
Тогава казвам: Спънаха ли се, та да паднат? Да не бъде! Но чрез тяхното отклонение дойде спасението на езичниците, за да ги възбуди към ревност.
12 Sasa ikiwa kushindwa kwao ni utajiri wa ulimwengu, na kama hasara yao ni utajiri wa mataifa, ni kiasi gani zaidi itakuwa kukamilika kwao?
А, ако тяхното отклонение значи богатство за света и тяхното отпадане
13 Na sasa naongea nanyi watu wa Mataifa. Kwa kuwa nimekuwa mtume kwa watu wa Mataifa mengine, najivunia huduma yangu.
Защото на вас, които бяхте езичници, казвам, че понеже съм апостол на езичниците, аз славя моята служба,
14 Labda nitawatia wivu walio mwili mmoja na mimi. Labda tutawaokoa baadhi yao.
дано по някакъв начин възбудя към ревност тия, които са моя плът, и да спася накои от тях.
15 Maana ikiwa kukataliwa kwao ni maridhiano ya dunia, kupokelewa kwao kutakuwaje ila uhai toka kwa wafu?
Защото, ако тяхното отхвърляне значи примирение на света, какво ще бъде приемането им, ако не оживяване от мъртвите?
16 Kama matunda ya kwanza ni akiba, ndivyo ilivyo kwa donge la unga. Kama mzizi ni akiba, matawi nayo kadhalika.
А ако първото от тестото е свято, то и цялото засяване е свято; и ако коренът е свят, то и клоните са свети.
17 Lakini kama baadhi ya matawi yamekatwa, kama wewe, tawi pori la mzeituni, ulipandikizwa kati yao, na kama ulishiriki pamoja nao katika mizizi ya utajiri wa mzeituni,
Но, ако някои клони са били отрязани, и ти, бидейки дива маслина, си бил присаден между тях, и си станал съучастник с тях в тлъстия корен на маслината,
18 usijisifu juu ya matawi. Lakini kama unajisifu, si wewe ambaye unaisaidia mizizi, bali mizizi inakusaidia wewe.
не се хвали между клоните; но ако се хвалиш, знай, че ти не държиш корена, а коренът тебе.
19 Basi utasema, “Matawi yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika shina.”
Но ще речеш: Отрязаха се клони, за да се присадя аз.
20 Hiyo ni kweli. Kwa sababu ya kutoamini kwao walikatwa, lakini wewe ulisimama imara kwa sababu ya imani yako. Usijifikirie mwenyewe kwa hali ya juu sana, bali ogopa.
Добре, поради неверие те се отрязаха, а ти поради вяра стоиш. Не високоумствувай, но бой се.
21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, hatakuhurumia wewe pia.
Защото, ако Бог не пощади естествените клони, нито тебе ще пощади.
22 Angalia, basi, matendo mema na ukali wa Mungu. Kwa upande mmoja, ukali ulikuja juu ya Wayahudi ambao walianguka. Lakini kwa upande mwingine, wema wa Mungu huja juu yako, kama utadumu katika wema wake. Vinginevyo wewe pia utakatiliwa mbali.
Виж, прочее, благостта и строгостта Божии; строгост към падналите, а божествена благост към тебе, ако останеш в тая благост; иначе, и ти ще бъдеш отсечен.
23 Na pia, kama hawataendelea katika kutoamini kwao, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
Така и те, ако не останат в неверие, ще се присадят; защото Бог може пак да ги присади.
24 Kwa maana ikiwa ninyi mlikatwa nje kwa ulio kwa asili mzeituni mwitu, na kinyume cha asili mlipandikizwa katika mzeituni ulio mwema, si zaidi sana hawa Wayahudi, ambao ni kama matawi ya asili kuweza kupandikizwa tena ndani ya mzeituni wao wenyewe?
Понеже, ако ти си бил отсечен от маслина, по естество дива, и, против естеството, си бил присаден на питомна маслина, то колко повече ония, които са естествени клони, ще се присадят на своята маслина!
25 Kwa maana ndugu sitaki msijue, kuhusiana na siri hii, ili kwamba msiwe na hekima katika kufikiri kwenu wenyewe. Siri hii ni kwamba ugumu umetokea katika Israeli, hadi kukamilika kwa mataifa kutakapokuja.
Защото, братя, за да не се мислите за мъдри, искам да знаете тая тайна, че частично закоравяване сполетя Израиля, само докато влезе пълното число на езичниците.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka, kama ilivyoandikwa: “Kutoka Sayuni atakuja Mkombozi. Atauondoa uovu kutoka kwa Yakobo.
И така целият Израил ще се спаси, както е писано:
27 Na hili litakuwa agano langu pamoja nao, wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
И ето завета на Мене към тях: Когато отнема греховете им"
28 Kwa upande mmoja kuhusu injili, wanachukiwa kwa sababu yenu. Kwa upande mwingine kutokana na uchaguzi wa Mungu, wamependwa kwa sababu ya mababu.
Колкото за благовестието, те са неприятели, което е за наша полза, а колкото за избора, те са въблюбени заради бащите.
29 Kwa kuwa zawadi na wito wa Mungu haubadiliki.
Защото даровете и призванието от Бога са неотменими.
30 Kwa kuwa awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmeipokea rehema kwa sababu ya kuasi kwao.
Защото както вие някога се непокорявахте (Или: Неповярвахте
31 Kwa njia iyo hiyo, sasa hawa Wayahudi wameasi. Matokeo yake ni kwamba kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi wanaweza pia kupokea rehema.
също така и те сега се не покоряват.
32 Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi, ili aweze kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
Защото Бог затвори всички в непокорство, та към всички да покаже милост. (eleēsē g1653)
33 Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hazichunguziki hukumu zake, na njia zake hazigunduliki!
О колко дълбоко е богатството на премъдростта и знанието на Бога! Колко са непостижими Неговите съдби, и неизследими пътищата Му!
34 “Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani amekuwa mshauri wake?
Защото, "Кой е познал ума на Господа, Или, кой Му е бил съветник?"
35 Au ni nani kwanza aliyempa kitu Mungu, ili alipwe tena?”
или, "Кой от по-напред Му е дал нещо, Та да му се отплати?"
36 Kwa maana kutoka kwake, na kwa njia yake na kwake, vitu vyote vipo. Kwake uwe utukufu milele. Amina. (aiōn g165)
Защото всичко е от Него, чрез Него и за Него, Нему да бъде слава до векове. Амин. (aiōn g165)

< Warumi 11 >