< Ufunuo 8 >

1 Wakati Mwanakondoo alipofungua muhuri ya saba, kukawa na ukimya mbinguni takribani nusu saa.
Et lorsqu’il ouvrit le septième sceau, il se fit un silence au ciel d’environ une demi-heure.
2 Kisha nikaona malaika saba wasimamao mbele za Mungu, na wakapewa tarumbeta saba.
Et je vis les sept anges qui se tiennent devant Dieu, et il leur fut donné sept trompettes.
3 Malaika mwingine akaja, ameshikilia bakuli ya dhahabu yenye uvumba, amesimama madhabahuni. Akapewa uvumba mwingi ili kwamba autoe pamoja na maombi ya waamini wote katika madhabahu ya dhahabu mbele ya kiti cha enzi.
Et un autre ange vint et se tint debout devant l’autel, ayant un encensoir d’or; et beaucoup de parfums lui furent donnés, pour donner [efficace] aux prières de tous les saints, sur l’autel d’or qui est devant le trône.
4 Moshi wa ule uvumba, pamoja na maombi ya waamini, ukapanda juu mbele za Mungu kutoka mkononi mwa malaika.
Et la fumée des parfums monta avec les prières des saints, de la main de l’ange devant Dieu.
5 Malaika akatwaa bakuli la uvumba na akalijaza moto kutoka kwenye madhabahu. Kisha akalitupa chini juu ya nchi, na kukatokea sauti za radi, miale ya radi na tetemeko la nchi.
Et l’ange prit l’encensoir et le remplit du feu de l’autel; et il jeta [le feu] sur la terre; et il y eut des voix et des tonnerres et des éclairs et un tremblement de terre.
6 Wale malaika saba ambao walikuwa na tarumbeta saba wakawa tayari kuzipiga.
Et les sept anges qui avaient les sept trompettes se préparèrent pour sonner de la trompette.
7 Malaika wa kwanza akaipiga tarumbeta yake, na kukatokea mvua ya mawe na moto uliochanganyikana na damu. Vikatupwa chini katika nchi ili kwamba theluthi yake iungue, theluthi ya miti ikaungua na nyasi zote za kijani zikaungua.
Et le premier sonna de la trompette: et il y eut de la grêle et du feu, mêlés de sang, et ils furent jetés sur la terre; et le tiers de la terre fut brûlé; et le tiers des arbres fut brûlé, et toute herbe verte fut brûlée.
8 Malaika wa pili akaipiga tarumbeta yake, na kitu kama mlima mkubwa uliokuwa unaungua kwa moto ukatupwa baharini. Theluthi ya bahari ikawa damu,
Et le second ange sonna de la trompette: et comme une grande montagne toute en feu fut jetée dans la mer; et le tiers de la mer devint du sang,
9 theluthi ya viumbe hai katika bahari vikafa, na theluthi ya meli zikaharibiwa.
et le tiers des créatures qui étaient dans la mer et qui avaient vie mourut, et le tiers des navires fut détruit.
10 Malaika wa tatu akaipiga tarumbeta yake, na nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, ikimulika kama kurunzi, juu ya theluthi ya mito na chemichemi za maji.
Et le troisième ange sonna de la trompette: et il tomba du ciel une grande étoile, brûlant comme un flambeau; et elle tomba sur le tiers des fleuves et sur les fontaines des eaux.
11 Jina la nyota ni pakanga. Theluthi ya maji ikawa pakanga, na watu wengi wakafa kutokana na maji yaliyokuwa machungu.
Et le nom de l’étoile est Absinthe; et le tiers des eaux devint absinthe, et beaucoup d’hommes moururent par les eaux, parce qu’elles avaient été rendues amères.
12 Malaika wa nne alipiga tarumbeta yake, na theluthi ya jua ikapigwa, pamoja na theluthi ya mwezi na theluthi ya nyota. Kwa hiyo theluthi ya vyote ikageuka kuwa giza; theluthi ya mchana na theluthi ya usiku havikuwa na mwanga.
Et le quatrième ange sonna de la trompette: et le tiers du soleil fut frappé, et le tiers de la lune, et le tiers des étoiles, afin que le tiers de ces [astres] soit obscurci, et que le jour ne paraisse pas pour le tiers de sa [durée], et de même pour la nuit.
13 Nilitazama, na nikasikia tai aliye kuwa anaruka katikati ya anga, akiita kwa sauti kuu, “Ole, ole, ole, kwa wale wakaao katika nchi, kwa sababu ya mlipuko wa tarumbeta iliyosalia ambayo imekaribia kupigwa na malaika watatu.”
Et je vis: et j’entendis un aigle qui volait par le milieu du ciel, disant à haute voix: Malheur, malheur, malheur, à ceux qui habitent sur la terre, à cause des autres voix de la trompette des trois anges qui vont sonner de la trompette!

< Ufunuo 8 >