< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
aparaM sArddisthasamite rdUtaM pratIdaM likha, yo jana Ishvarasya saptAtmanaH sapta tArAshcha dhArayati sa eva bhAShate, tava kriyA mama gocharAH, tvaM jIvadAkhyo. asi tathApi mR^ito. asi tadapi jAnAmi|
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
prabuddho bhava, avashiShTaM yadyat mR^itakalpaM tadapi sabalIkuru yata Ishvarasya sAkShAt tava karmmANi na siddhAnIti pramANaM mayA prAptaM|
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
ataH kIdR^ishIM shikShAM labdhavAn shrutavAshchAsi tat smaran tAM pAlaya svamanaH parivarttaya cha| chet prabuddho na bhavestarhyahaM stena iva tava samIpam upasthAsyAmi ki ncha kasmin daNDe upasthAsyAmi tanna j nAsyasi|
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
tathApi yaiH svavAsAMsi na kala NkitAni tAdR^ishAH katipayalokAH sArddinagare. api tava vidyante te shubhraparichChadai rmama sa Nge gamanAgamane kariShyanti yataste yogyAH|
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
yo jano jayati sa shubhraparichChadaM paridhApayiShyante, aha ncha jIvanagranthAt tasya nAma nAntardhApayiShyAmi kintu matpituH sAkShAt tasya dUtAnAM sAkShAchcha tasya nAma svIkariShyAmi|
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
yasya shrotraM vidyate sa samitIH pratyuchyamAnAm AtmanaH kathAM shR^iNotu|
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
apara ncha philAdilphiyAsthasamite rdUtaM pratIdaM likha, yaH pavitraH satyamayashchAsti dAyUdaH ku njikAM dhArayati cha yena mochite. aparaH ko. api na ruNaddhi ruddhe chAparaH ko. api na mochayati sa eva bhAShate|
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
tava kriyA mama gocharAH pashya tava samIpe. ahaM muktaM dvAraM sthApitavAn tat kenApi roddhuM na shakyate yatastavAlpaM balamAste tathApi tvaM mama vAkyaM pAlitavAn mama nAmno. asvIkAraM na kR^itavAMshcha|
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
pashya yihUdIyA na santo ye mR^iShAvAdinaH svAn yihUdIyAn vadanti teShAM shayatAnasamAjIyAnAM kAMshchid aham AneShyAmi pashya te madAj nAta Agatya tava charaNayoH praNaMsyanti tva ncha mama priyo. asIti j nAsyanti|
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
tvaM mama sahiShNutAsUchakaM vAkyaM rakShitavAnasi tatkAraNAt pR^ithivInivAsinAM parIkShArthaM kR^itsnaM jagad yenAgAmiparIkShAdinenAkramiShyate tasmAd ahamapi tvAM rakShiShyAmi|
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
pashya mayA shIghram AgantavyaM tava yadasti tat dhAraya ko. api tava kirITaM nApaharatu|
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
yo jano jayati tamahaM madIyeshvarasya mandire stambhaM kR^itvA sthApayisyAmi sa puna rna nirgamiShyati| apara ncha tasmin madIyeshvarasya nAma madIyeshvarasya puryyA api nAma arthato yA navInA yirUshAnam purI svargAt madIyeshvarasya samIpAd avarokShyati tasyA nAma mamApi nUtanaM nAma lekhiShyAmi|
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
yasya shrotraM vidyate sa samitIH pratyuchyamAnAm AtmanaH kathAM shR^iNotu|
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
apara ncha lAyadikeyAsthasamite rdUtaM pratIdaM likha, ya Amen arthato vishvAsyaH satyamayashcha sAkShI, Ishvarasya sR^iShTerAdishchAsti sa eva bhAShate|
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
tava kriyA mama gocharAH tvaM shIto nAsi tapto. api nAsIti jAnAmi|
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
tava shItatvaM taptatvaM vA varaM bhavet, shIto na bhUtvA tapto. api na bhUtvA tvamevambhUtaH kadUShNo. asi tatkAraNAd ahaM svamukhAt tvAm udvamiShyAmi|
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
ahaM dhanI samR^iddhashchAsmi mama kasyApyabhAvo na bhavatIti tvaM vadasi kintu tvameva duHkhArtto durgato daridro. andho nagnashchAsi tat tvayA nAvagamyate|
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
tvaM yad dhanI bhavestadarthaM matto vahnau tApitaM suvarNaM krINIhi nagnatvAt tava lajjA yanna prakAsheta tadarthaM paridhAnAya mattaH shubhravAsAMsi krINIhi yachcha tava dR^iShTiH prasannA bhavet tadarthaM chakShurlepanAyA njanaM mattaH krINIhIti mama mantraNA|
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
yeShvahaM prIye tAn sarvvAn bhartsayAmi shAsmi cha, atastvam udyamaM vidhAya manaH parivarttaya|
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
pashyAhaM dvAri tiShThan tad Ahanmi yadi kashchit mama ravaM shrutvA dvAraM mochayati tarhyahaM tasya sannidhiM pravishya tena sArddhaM bhokShye so. api mayA sArddhaM bhokShyate|
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
aparamahaM yathA jitavAn mama pitrA cha saha tasya siMhAsana upaviShTashchAsmi, tathA yo jano jayati tamahaM mayA sArddhaM matsiMhAsana upaveshayiShyAmi|
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
yasya shrotraM vidyate sa samitIH pratyuchyamAnam AtmanaH kathAM shR^iNotu|

< Ufunuo 3 >