< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
And to the aungel of the chirche of Sardis write thou, These thingis seith he, that hath the seuene spiritis of God, and the seuene sterris. Y woot thi werkis, for thou hast a name, that thou lyuest, and thou art deed.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Be thou wakynge, and conferme thou othere thingis, that weren to diynge; for Y fynde not thi werkis fulle bifore my God.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
Therfor haue thou in mynde, hou thou resseyuedist, and herdist; and kepe, and do penaunce. Therfor if thou wake not, Y schal come as a nyyt theef to thee, and thou schalt not wite in what our Y schal come to thee.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
But thou hast a fewe names in Sardis, whiche han not defoulid her clothis; and thei schulen walke with me in whijt clothis, for thei ben worthi.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
He that ouercometh, schal be clothid thus with whijt clothis; and Y schal not do awei his name fro the book of lijf, and Y schal knoueleche his name bifore my fadir, and bifore hise aungels.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
He that hath eeris, here he, what the spirit seith to the chirchis.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
And to the aungel of the chirche of Filadelfie write thou, These thingis seith the hooli and trewe, that hath the keie of Dauid; which openeth, and no man closith, he closith, and no man openith.
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I woot thi werkis, and lo! Y yaf bifore thee a dore opened, which no man may close; for thou hast a litil vertu, and hast kept my word, and denyest not my name.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Lo! Y schal yyue to thee of the synagoge of Sathanas, whiche seien that thei ben Jewis, and ben not, but lyen. Lo! Y schal make hem, that thei come, and worschipe byfor thi feet; and thei schulen wite,
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
that Y louyde thee, for thou keptist the word of my pacience. And Y schal kepe thee fro the our of temptacioun, that is to comynge in to al the world, to tempte men that dwellen in erthe.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
Lo! Y come soone; holde thou that that thou hast, that no man take thi coroun.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
And hym that schal ouercome, Y schal make a pilere in the temple of my God, and he schal no more go out; and Y schal write on hym the name of my God, and the name of the citee of my God, of the newe Jerusalem, that cometh doun fro heuene of my God, and my newe name.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
He that hath eeris, here he, what the spirit seith to the chirchis.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
And to the aungel of the chirche of Laodice write thou, These thingis seith Amen, the feithful witnesse and trewe, which is bigynnyng of Goddis creature.
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I woot thi werkis, for nether thou art cold, nether thou art hoot; Y wolde that thou were could, ethir hoot;
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
but for thou art lew, and nether cold, nether hoot, Y schal bigynne to caste thee out of my mouth.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
For thou seist, That Y am riche, and ful of goodis, and Y haue nede of no thing; and thou wost not, that thou art a wretche, and wretcheful, `and pore, and blynde, and nakid.
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
Y counsele thee to bie of me brent gold, and preued, that thou be maad riche, and be clothid with whijt clothis, that the confusioun of thi nakidnesse be not seen; and anoynte thin iyen with a collerie, that thou se.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
Y repreue, and chastise whom Y loue; therfor sue thou goode men, and do penaunce.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Lo! Y stonde at the dore, and knocke; if ony man herith my voys, and openith the yate to me, Y shal entre to hym, and soupe with hym, and he with me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
And Y schal yyue to hym that schal ouercome, to sitte with me in my trone, as also Y ouercam, and sat with my fadir in his trone.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
He that hath eeris, here he, what the spirit seith to the chirchis.

< Ufunuo 3 >